PAPA Francis awatembelea makahaba

PAPA Francis awatembelea makahaba

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,276
View attachment 381365Papa Francis kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani amekaa kwa zaidi ya saa moja na makahaba waishio nchini Italia ambao walisafiri kutoka nchi mbalimbali duniani.

Papa mwenye umri wa miaka 79 amekuwa akikemea vitendo vya kutoka taifa moja kwenda lingine ili kuwatumikisha katika biashara za ngono.

Akiwa na wanawake 20 waishio katika moja ya jengo linalomilikiwa na kanisa katoliki katika mji mkuu wa Italia, kiongozi huyo akizungumza na wanawake hao akitaka kujua namna walivyoingia biashara hiyo haramu.

Wanawake hao wenye umri unaokadiriwa kuwa kati ya miaka 30 walitekwa na mwanamme mmoja, miongoni mwao wapo wanaigeria saba, waromania sita, na wengine wanne kutoka Albania, huku watatu wakitoka Italia, Tunisia na Ukraine.

Aidha, wamekiri sababu ya kubwa inayopelekea kwenda huko ni ajira ambapo wafanyabiashara Italia na nchi nyingine kutoka mataifa ya ulaya huwachukua kwa kuwaahidi kuwapa kazi na wakifika huko hulazimishwa kufanya ukahaba.

Papa Francis amewatia moyo makahaba hao wenye nia ya kuachana na biashara hiyo, wanapoanza maisha mapya kwa usaidizi wa kituo cha Papa Yohana wa pili.

Chanzo :Mpekuzi blog.
 
Hii imekaa poa sana maana, "... na asiye na dhambi miongoni mwenu na awe kwanza wa kumrushia jiwe ...". Mambo ya kukatana vichwa eti unasimamia mafundisho ya dini yamepitwa na wakati uta kuta hata hilo lililoshikilia upanga kuchinja wenzake lina dhambi za ajabu ni kwa vile mambo ya moyoni ni siri ya mhusika na mungu wake.

"... hata mimi sikuhumu, enenda zako wala usitende dhambi tena ...", hiyo ndiyo aina ya Injili ninayoifahamu, hilo ndilo Neno la Mungu wa kweli. Abarikiwe sana His Holiness.
 
Zamani nilipokuwa kijana nilikuwa na tabia ya kwenda kuwatembelea kila ijumaa na jumamosi.
 
Ni ukarimu tu na kuwajulia hali zao
Kwa hiyo uliamua kuchagua kwa makahaba kama mahali pa kuonesha ukarimu wako? Ungeniambia kwa wagonjwa mahospitalini na wafungwa magerezani ningekuelewa.
 
Kwa upande Wa maninja huko ni mwiko.. Wakikuona wanakukata kichwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom