Wanajamvi nimekutwa na swaib moja, xgirlfriend wangu ambae tuliachana kama miaka minne nyuma kipindi hicho tukiwa ndo kwanza tumeanza tu chuo leo anadai bado ananipenda,
nakumbuka tulipomaliza A'level mimi nilipangiwa Udsm, yeye akapata Tumaini,
sasa mwanzoni tu baada ya kuingia chuoni yeye akadai hawezi mapenzi ya mbali so tutengane tuu maana hata weza kuniamini,kwakuwa hatukua na ugomvi na hapo ni baada ya kumsisitiza kuniamini kushindwa nikaridhia kwa moyo mmoja, yeye kule akaanza mahusiano na mimi kwa upande wangu nikapata dem mwingine. Tulikuwa tukiwasiliana kwa nadra sana kama marafiki lakini ikafika kipindi akanikataza nisiwasiliane nae kwani, anampenda sana mtu wake na hataki kumkwaza, wakati mwingine nikawa namfwata mkoani akiwa likizo ili japo nimwone sababu nilimpenda sana, na siku za mwanzo nilifikiri uhusiano wangu mpya ungenifariji kumbe ikawa ngumu maana bado nilimpenda yeye, lakini hakuwa tayari kurudisha moyo nyuma.
Ishu ikaja mwaka jana mwanzoni nikapata mishe iliyoniwezesha kutoka Bongo nakuja state, alichelewa kufahamu kama sipo nchini sasa majuzi kati tukakutana kwenye FaceBook, na tukawasiliana,ishu inakuja anadai ananipenda sana na yuko tayari kubrake na jamaa yake,
Kwakweli kila nikipima naona huyu ni walewale maana nini sasa kinamfanya anipende leo?
Je jamaa yake aliyenae itakuwaje? huu si ubinafsi? wandugu nishaurini.
she loves u now cos ure in states that is all about!