Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,027
- 144,382
Ngugu zangu wapenda mabadiliko,leo naomba mtanisamehe kwani wakati mwingine inabidi tuelezane ukweli na ikiwezekana tujisahihishe pale tunapokosea vinginevyo tutabaki kulalamika tu miaka yote.
Ni hivi,wakati tunalalamikia kitendo cha raia mmoja kwenda mahakamani kupinga ukomo wa vipindu viwili vya uraisi,tujiulize sisi wapenda mabadiliko, je, na sisi hatuwezi kwenda mahakamani kupinga tume ya uchaguzi kutokuwa huru kama ibara ya 74(7) ya katiba inavyoagiza?
Je,hatuwezi kwenda mahakamani kujenga hoja kuiomba mahakama iizuei tume hii kuendesha uchaguzi wowote ule mpaka kesi ya msingi tutakayofungua kupinga tume kutokuwa huru itolewe uamuzi na mahakama?
Je, na sisi hatuwezi kwenda mahakamanini na kuiomba mahakama itamke kuwa matokeo ya uraisi kutopingwa mahakamani ni kinyume na matakwa ya katiba yetu inayotambua mahakama kama chombo pekee chenye mamlaka ya kutoa haki(kutafsi sheria)?
Nambo niweke wazi kuwa mimi si mwanasheria na wala si mtaalamu wa mambo ya katiba ila kwa kusoma tu katiba yetu naona bado na sisi tunaweza kwenda mahakamani kupinga au kuhoji baadhi ya ibara za katiba yetu ambazo baadhi ni wazi zina kasoro na zingine hazifai kuendelea kuwepo katka katiba hii inayotambuwa uwepo wa mfumo wa vyama vingi kama vile ibara ya 74(1) inayompa Raisi anaetokana na chama kimojawapo cha siasa kuteua mwenyekiti na watendaji wengine wa tume ya uchaguzi.
Mambo haya nimeyasema sana kupitia hapa JF ila hatushituki hivyo wacheni wenzetu watumie haki yao maana sisi tunajisahau sana.
Na mwisho huwa najiuliza hivi haiwezekani kwenda mahakamani na kuiomba mahakama iagize serikalli kukamilisha mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya?
kama tunavyopigania ubunge wa Lissu mahakamanini na kama tunavyopigania mambo mengine kupitia mahakama hizi hizi tulizona na mashaka nazo,basi tufanye hivyo kupigani mambo haya ya msingi yaliyo kikwazo katika swala zima la upinzani kutimiza azima yake ya kushika dola na tukifanya hivi, hata wananchi watuona tuko serious na si watu wa kulalamika tu unless maombi haya ninayoyapendekeza hayawezi kufunguliwa mahakamani(wanasheria mtanisaidia).
Nliowahi kuhoji/kushauri ni haya:
Ni hivi,wakati tunalalamikia kitendo cha raia mmoja kwenda mahakamani kupinga ukomo wa vipindu viwili vya uraisi,tujiulize sisi wapenda mabadiliko, je, na sisi hatuwezi kwenda mahakamani kupinga tume ya uchaguzi kutokuwa huru kama ibara ya 74(7) ya katiba inavyoagiza?
Je,hatuwezi kwenda mahakamani kujenga hoja kuiomba mahakama iizuei tume hii kuendesha uchaguzi wowote ule mpaka kesi ya msingi tutakayofungua kupinga tume kutokuwa huru itolewe uamuzi na mahakama?
Je, na sisi hatuwezi kwenda mahakamanini na kuiomba mahakama itamke kuwa matokeo ya uraisi kutopingwa mahakamani ni kinyume na matakwa ya katiba yetu inayotambua mahakama kama chombo pekee chenye mamlaka ya kutoa haki(kutafsi sheria)?
Nambo niweke wazi kuwa mimi si mwanasheria na wala si mtaalamu wa mambo ya katiba ila kwa kusoma tu katiba yetu naona bado na sisi tunaweza kwenda mahakamani kupinga au kuhoji baadhi ya ibara za katiba yetu ambazo baadhi ni wazi zina kasoro na zingine hazifai kuendelea kuwepo katka katiba hii inayotambuwa uwepo wa mfumo wa vyama vingi kama vile ibara ya 74(1) inayompa Raisi anaetokana na chama kimojawapo cha siasa kuteua mwenyekiti na watendaji wengine wa tume ya uchaguzi.
Mambo haya nimeyasema sana kupitia hapa JF ila hatushituki hivyo wacheni wenzetu watumie haki yao maana sisi tunajisahau sana.
Na mwisho huwa najiuliza hivi haiwezekani kwenda mahakamani na kuiomba mahakama iagize serikalli kukamilisha mchakato wa kupatikana kwa katiba mpya?
kama tunavyopigania ubunge wa Lissu mahakamanini na kama tunavyopigania mambo mengine kupitia mahakama hizi hizi tulizona na mashaka nazo,basi tufanye hivyo kupigani mambo haya ya msingi yaliyo kikwazo katika swala zima la upinzani kutimiza azima yake ya kushika dola na tukifanya hivi, hata wananchi watuona tuko serious na si watu wa kulalamika tu unless maombi haya ninayoyapendekeza hayawezi kufunguliwa mahakamani(wanasheria mtanisaidia).
Nliowahi kuhoji/kushauri ni haya:
Katiba ya mwaka 77, haiji-contradict kuongelea suala la Tume Huru ya Uchaguzi na hapo hapo kumruhusu Rais kuteua viongozi na watendaji wa tume hiyo?
Hebu tusome hii ibara ya 74 ya katiba inaohusu Tume ya Uchaguzi alafu tuone kama katiba hii haiji-contradict kwa kumpa mamalaka Raisi wa nchi ambae anatokana na chama cha siasa kuteua viongozi na watendaji wa hii Tume(Ibara ya 74(1) na wakati huo huo katiba hiyo hiyo inaongelea swala la tume...
www.jamiiforums.com
CHADEMA, fungueni kesi kupinga uhalali wa Tume ya Uchaguzi na muiombe mahakama iizuei Tume kusimamua chaguzi zote zijazo
Kwanza naomba niweke wazi kuwa mimi si mwanasheria na wala si mtaalamu wa mambo ya Katiba. Pamoja na mimi kuwa si mwanasheria ila nafahamu kabisa ni jambo la kawaida watu kufungua kesi mahakamani kuhoji uhalali wa sheria ambazo kwa mtazamo wao sheria hizo zina mapungufu au zinakiuka katiba ya...
www.jamiiforums.com
Wapinzani tumefanya vya kutosha kudai Tume ya Uchaguzi kupitia mahakama licha ya mashaka tulionayo kuhusu mahakama zetu?
Binafsi najiuliza sana kama tunapambana vya kutosha kudai Tume Huru kupitia mhimili wa mahakama kama tunavyofanya katika kupigania/kudai haki zetu zingine kupitia mahakama hizi hizi ambazo wakati mwingine zinaonekana kutotundea haki(mfano ni kuhusu dhamana katika kesi za kina Lema,Mbowe na...
www.jamiiforums.com