Pambazuko jipya Tanganyika! Hatimaye Rais Samia kajitua furushi zito sana

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,640
697,994
Kwanza habari za kifo cha Prof J ni za uongo hivyo zipuuzeni..Imebidi nifanye masahihisho ya haraka kwenye hiki kifungu cha kwanza

Pili nipende mno kumpongeza Mama Samia Suluhu kwa kujitua furushi zito lililomlemea sana tangu alipotwishwa na hao wenye agenda zao. Hatimaye ukweli amekuja kuuona na kwa dhati ya moyo na uthubutu wa hali ya juu kabisa kaamua kufanya ambacho wengi wasingethubutu kukifanya.. Mama yu kwenye mchakato wa maridhiano na chama kikuu pendwa na maarufu Afrika na duniani CHADEMA

Tatu nimpongeze wakili msomi na mwanasiasa machachari Tundu Lissu kwa kazi kubwa aliyofanya akiwa nje uhamishoni kwa muda wote aliokuwa huko .. Kitu kilichopelekea kusababisha na kuchagiza haya yanayotarajiwa kutokea.. Maridhiano na kufungua ukurasa mpya..

Nne nimpongeze kwa dhati ya moyo mwenyekiti shupavu wa CHADEMA kwa kusimama imara hata katika kipindi cha kuumizwa na kutikiswa kisiasa, kiuchumi na kijamii Lakini bado akabaki imara kama chuma cha pua..! Kukichwa hatimaye hupambazuka.. !

Tano niwapongeze wanachama, wapenzi, mashabiki nk wote wa chama kikuu cha upinzani Tanzania kwa kushikamana, kutiana moyo kusaidiana katika kipindi chote cha mapito yote waliyopitia.. Hakika wamekuwa jasiri na shupavu kwa kiwango cha juu kabisa..pongezi hizi ziwaendee na viongozi wote pia

Sita niwapongeze CCM ...!

Mama aliposhika hatamu ilikuwa ni kipindi cha usemi maarufu wa KUUPIGA MWINGI..! Tulimsifu na kumsifia kila upande na kila kona.. Lakini mara ghafla bin vuu akazongwa na kutwishwa furushi zito lililomuelemea kwa kipindi chote hicho.. Muda hauongopi na muda ni hakimu mzuri.. Uongo hupanda lift na kufika haraka bali ukweli hukwea ngazi na kufika baadae!

Tunatambua yote haya mapya yanayotrend sana hayakutokea ghafla bin vuu.. Ni mengi yamefanyika nyuma ya macho ya hadhira.. Tunda lake la kwanza kuonekana likitarajiwa kuwa tar 18.02.2022...Likitokea kama linavyotarajiwa kutokea basi ni mwanzo mwema sana
Natambua kuna kesi zinaweza kufutwa.. Watuhumiwa wakaachiwa huru lakini hapo hapo wakakamatwa tena! Hili tuliweke kiporo

Natambua pia kuna covid 19.. Namna vile homa inavyopanda na kushuka!

Natambua pia hii ni wiki ya RED CLOLOR... Rangi angavu inayoashiria bahati,nguvu na mamlaka kwa baadhi ya tamaduni.. Rangi ya upendo na wapendao. Rangi ya Timu kubwa Afrika SIMBA SPORTS CLUB.. IMEPIGA MTU 3:0, KISHA IKAPIGA MWINGINE 7:0.. Tafuta kiroho tafsiri ya namba 3 na 7 na nguvu zake.. Utajua CHADEMA ni nani.. Na SIMBA ninini..!!!!


Ni hayo tuu..!
 

Attachments

  • FB_IMG_1645021031371.jpg
    FB_IMG_1645021031371.jpg
    45.9 KB · Views: 57
natamani niseme kitu,
ila nikishakumbuka tu kuwa siasa ni game kama magame mengine ambayo unahitaji strategies nzuri zaidi ya mpinzani wako ili umknot down....
napata kigugumizi🤣🤣

"ngoja waje wanipe muongozo"

cc.Mahondaw
🤣
 
,
Samia na Lissu walijikita hapa;

1.Kesi ya Mbowe-iondolewe

2.Zuio la vyama vya siasa kufanya mikutano na shughuli za kisiasa

3.Katiba mpya na Chaguzi huru

4.Usalama wake na wenzake waliopo uhamishoni,Haki zake za matibabu na mafao nk

Rais atoe kauli ya kumkaribisha nyumbani na kumpatia passport mpya baada ya kuibiwa ujerumani

Assurance kwa Lema na Wenje

5.Wabunge wa Covid-19

Rais aponye makovu ya nchi,ana jukumu la kuongoza chi kwa kurejesha mshikamano,atekeleze ahadi aliyotoa bungeni na kwenye barua kuwa atakutana na viongozi wa vyama vya siasa.

Raisi ameyapokea na Lissu ameshukuru kwa jambo hili.

Kuwa tayari kuondoa masuala yanayotatiza nchi na kuwe na nia ya DHATI Kujenga upya nchi kisheria,haki na maendeleo.
 
Naunga mkono maridhiano yenye manufaa kwa Taifa.

Na hapo mwishoni naomba niungane na wewe kusema "Thimba guvu moya" Yule Bocco tuliye mkashifu na kumkejeli, ghafla amegeuka na kuwa tena shujaa wa timu!
 
Tunatambua yote haya mapya yanayotrend sana hayakutokea ghafla bin vuu.. Ni mengi yamefanyika nyuma ya macho ya hadhira.. Tunda lake la kwanza kuonekana likitarajiwa kuwa tar 18.02.2022...Likitokea kama linavyotarajiwa kutokea basi ni mwanzo mwema sana
Natambua kuna kesi zinaweza kufutwa..
Naamini kuna watu hawalali tangu kesi ya kina Mbowe ilipoairishwa hapo majuzi, usigizi ukakata zaidi baada ya Maza kukutana na Lissu jana ambaye licha ya kuwa mama alishajua uzandiki wa Kina Kingai na Sirro kwenye kesi hii, Lissu atakuwa amempa uchambuzi wa kina na rejea hasa ushahahidi mwepesi ambao Kina Swila, Ndowo, Mahita, Jumanne na wengine wamepwaya mno kuthibitisha ukweli wa tuhuma hizo!

kwa kweli yajayo ni furaha
 
Naunga mkono maridhiano yenye manufaa kwa Taifa.

Na hapo mwishoni naomba niungane na wewe kusema "Thimba guvu moya" Yule Bocco tuliye mkashifu na kumkejeli, ghafla amegeuk na kuwa tena shujaa wa timu!
Waliomkashifu na kumkejeli walikuwa mamluki
Screenshot_20220217-095427.jpg
 
DAS Mbeya unaona Rais amewakosea sio? Basi subiri arudi akosee tena kwenye uteuzi wako! Huna adabu kabisa.
Mshana Jr hawa watu wa aina hii ndio waliokuwa wanamtwisha mama zigo lisilokuwa na faida, apitishe tuu fyekeo
Sijui sasa hivi hili likiwezekana watafanyaje.. Kuna yule aliyesema covid 19 ni halali.. Subiri uone atajua hajui
 
Natambua kuna kesi zinaweza kufutwa.. Watuhumiwa wakaachiwa huru lakini hapo hapo wakakamatwa tena! Hili tuliweke kiporo
God is good HALIJATOKEA
 
Back
Top Bottom