Pambana utimize ahadi, uaminifu ukiondoka haurudi

Darren2019

JF-Expert Member
Nov 23, 2019
1,112
2,379
Uaminifu uko katika mambo mbalimbali ila mimi ntajikita hasa kwenye mambo ya fedha.

Nimekuwa muhanga wa kuumizwa na jamaa zangu mara kwa mara hadi najiona boya sasa, si kwamba nina pesa no ila katika hizihizi senti mbili tatu.

Unamwamini mtu unamwazimisha fedha tena unamwambia si zako, anakuhakikshia hatokuangusha nawe unampa kwa bashasha eti umemsaidia jamaa ako, mwisho wa siku matokeo yake unakuja kulipa mwenyewe na urafiki unakufa.

Visa vipo vingi ila vingne ni hivi vya kurejesha deni nusunusu kinyume na makubaliano, tunavurugiana mipango bhana.

Mtu nimempa elfu 50 January kwa makubaliano arudishe mwisho wa mwezi, ulipofika mwisho wa mwezi akanifuata anaomba nimvumilie atarejesha mwisho wa February, nikakaza roho nkakubali, leo anakuja na elfu 20 eti nimvumilie hadi wiki ijayo kuna hela anasubiri kwa jamaa ake. Nimepokea ila nimefanya somo.

Ukitaka kupoteza marafiki jitie kiherehere wa kukopesha ovyo. Natambua kila mtu ana chance ya kupata shida ila tujitahidi kuthamini wanaotusaidia si kwamba wanazo sana.
 
Watanzania wengi hawana kabisa UAMINIFU, wanachukulia poa tu na ni wagumu sana wa kuheshimu makubaliano kama ilivyo muda.
 
Jamani acheni kabisa hizi maada za madeni huwa zinanifanya niheme juu juu nadai karibia laki nne nikisema nisikopeshe najikuta wamenipiga sound.
 
Mie kwenye madeni acha tyuuh, yaan nalizwa hadi baas.

Mtu una mkopesha vizuri tyuuh tena kwa wema, baadae ana muambia mchumba ake "yule fulan simlipi hela yake kamwe" afu yule mchuba ake anakuja kukupa in4 hiyo.

Nikaacha na kudai kabisaa, nimemuachia Jah tyuuh.
 
Hivi mtu unakopesha je mtu pesa wewe ni "micro finance credit facility", ni ushamba nafikra za ujamaa, na kuendekeza wizi kwa ndungu na marafiki, pesa ni 'asset' kama nyumba kama mke utawezaje kukopesha mtu kienyeji hivyo eti nirafiki au ndg, mimi ukiwa na shida ya fedha nakuchangia au na kujazia form za benki upate mkopo, au na kuombea kwa Mungu akusaidie tu. Ila sikopeshe mtu, Mjomba ngu alikufa kwa huruma kama hizo za kipumbavu, kamwe siwezi tena. Watanzania ni jamii ya watu wa ajabu sana likija suala la pesa.
 
Back
Top Bottom