Matanga
JF-Expert Member
- Nov 13, 2019
- 2,281
- 3,973
Mazungumzo baina ya Bwana Sixto na Sembela ambao ni marafiki wakubwa sana.
Sixto: Naumwa sana rafiki yangu Sembela nimelazwa wiki ya pili sasa sina pesa kabisa.
Sembela: Unaumwa nini Kaka?
Sixto: Homa imenibana kweli aisee na naona pesa za kugharimia matibabu zinaniishia kabisa.
Sembela: Ningekusaidia bro bahati mbaya kuna kiwanja tulipatana na muuzaji majuzi ndo nataka kesho nikanunue.
Sixto: Sawa Kaka, ila siko vizuri kabisa. Nisaidie walau kidogo ndugu yangu.
Sembela: Iko hivi bajeti zote tunazopanga Mimi na mke wangu, huwa hazivunjwi ndugu yangu. Nimebakiwa na hiyo milioni tano ya kiwanja.
Sixto: Ukinisaidia hata laki mbili tu inatosha. Nikipona nitakulipa, nitazirudisha.
Sembela: Hapo ngumu kidogo na vipi umejaribu kuupigia Uongozi wa Chama chetu cha wafanyabiashara?
Sixto: Ndio, wamenichangia 30000.
Sembela: Anzia hata hiyo bro. Get well soon.
BAADA YA SIXTO KUFARIKI
Sembela: Sixto alikuwa rafiki yangu tuliyeshirikiana katika mambo mengi sana hivyo Mimi kama rafiki aliyekuwa zaidi ya ndugu natoa mchango Milioni moja.
Chama cha Wafanyabiashara: Tumehuzunishwa sana na taarifa hii, kwani alikuwa mtu muhimu sana katika chama chetu.
Sisi tutagharamia gharama zote za hapa kuanzia chakula, usafiri hadi mazishi.
UJUMBE WANGU KWENU
Naomba ifikie kipindi tu tubadilike kwa kuanza kuthamini mgonjwa kuliko Maiti, yaani Mtu akishafariki.
Maana kuthamini Maiti kuliko Mgonjwa ni unafiki uliopitiliza.
Huenda huyo Mtu angesaidiwa kwa nguvu kubwa kama inayoonekana kwenye mazishi asingekufa.
Kibaya zaidi ni pale ambapo Mtu hakuwahi kwenda hospitali kumjulia hali Mgonjwa makusudi kabisa, lakini anajifanya yeye ndo Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi.
MUNGU atuhurumie. Tujitafakari saana na Tubadilike jamani!
Sixto: Naumwa sana rafiki yangu Sembela nimelazwa wiki ya pili sasa sina pesa kabisa.
Sembela: Unaumwa nini Kaka?
Sixto: Homa imenibana kweli aisee na naona pesa za kugharimia matibabu zinaniishia kabisa.
Sembela: Ningekusaidia bro bahati mbaya kuna kiwanja tulipatana na muuzaji majuzi ndo nataka kesho nikanunue.
Sixto: Sawa Kaka, ila siko vizuri kabisa. Nisaidie walau kidogo ndugu yangu.
Sembela: Iko hivi bajeti zote tunazopanga Mimi na mke wangu, huwa hazivunjwi ndugu yangu. Nimebakiwa na hiyo milioni tano ya kiwanja.
Sixto: Ukinisaidia hata laki mbili tu inatosha. Nikipona nitakulipa, nitazirudisha.
Sembela: Hapo ngumu kidogo na vipi umejaribu kuupigia Uongozi wa Chama chetu cha wafanyabiashara?
Sixto: Ndio, wamenichangia 30000.
Sembela: Anzia hata hiyo bro. Get well soon.
BAADA YA SIXTO KUFARIKI
Sembela: Sixto alikuwa rafiki yangu tuliyeshirikiana katika mambo mengi sana hivyo Mimi kama rafiki aliyekuwa zaidi ya ndugu natoa mchango Milioni moja.
Chama cha Wafanyabiashara: Tumehuzunishwa sana na taarifa hii, kwani alikuwa mtu muhimu sana katika chama chetu.
Sisi tutagharamia gharama zote za hapa kuanzia chakula, usafiri hadi mazishi.
UJUMBE WANGU KWENU
Naomba ifikie kipindi tu tubadilike kwa kuanza kuthamini mgonjwa kuliko Maiti, yaani Mtu akishafariki.
Maana kuthamini Maiti kuliko Mgonjwa ni unafiki uliopitiliza.
Huenda huyo Mtu angesaidiwa kwa nguvu kubwa kama inayoonekana kwenye mazishi asingekufa.
Kibaya zaidi ni pale ambapo Mtu hakuwahi kwenda hospitali kumjulia hali Mgonjwa makusudi kabisa, lakini anajifanya yeye ndo Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi.
MUNGU atuhurumie. Tujitafakari saana na Tubadilike jamani!