Behaviourist
JF-Expert Member
- Apr 8, 2016
- 39,901
- 95,385
Kenya acheni mzaha na kiswahili mara moja!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
"Aliyebanduliwa, habandikiki"Nitajitahidi kumbandika tena.
Naona hapo aliona wanaenda kumbandua bila wese akaone akagome kwanza ikabidi nguvu ya ziada itumike.Hii picha nadhani ni baada ya kubanduliwaView attachment 1621782
🙄🙄🙄Naona hapo aliona wanaenda kumbandua bila wese akaone akagome kwanza ikabidi nguvu ya ziada itumike.
Umenoa jombaa, nchini Kenya ukizungumza kuhusu kubanduliwa watu watajua unamaanisha maana kamili ya neno kubanduliwa. Wala hamna matumizi mengine ya neno hilo zaidi ya hapo. Sasa hapo utasemaje kwamba wamechemsha?Kikubwa kinachoangaliwa na kuzingatiwa katika matumizi ya lugha siyo matumizi sahihi ya neno bali hilo neno watu wamezoea kulitumia zaidi wapi na kwa wakati gani.Hiki ndicho ambacho huwa Kenya kinawapiga chenga kila siku katika kutumia kiswahili.Kwa hiyo hapo mmechemka!
kenya waseme tupeleke wajuzi bwanaKenya acheni mzaha na kiswahili mara moja!View attachment 1620275
Kama nguzo, au plaste
Nakuhakikishia kwamba hapo Citizen Tv hakuna anayefahamu kwamba 'kubanduliwa' lina maana nyingine, tofauti na walichonuia kwenye caption yao hiyo. Jombaa ni jambo la kawaida sana kwa lugha yeyote ile kuwa na maneno au matumizi ya maneno yanayotofautiana kwenye maeneo tofauti. Kwa mfano Kiswahili cha visiwani Lamu, Manda na Kiwayuu kinatofautiana na cha Mombasa, Malindi na Kilifi au hata Taveta. Hivyo hivyo kwa kiswahili cha Zenji, Pemba na kile cha Dar, Tanga na Tz bara kwa ujumla.Kwani hiyo TV channel inaonekana Kenya peke yake?Kwa kuwa inaonekana Afrika mashariki nzima kutokana na ukuaji wa mawasiliano kupitia digital ni lazima TV husika itumie neno la kiswahili kulingana na vile majority hulitumia neno hilo katika eneo ambalo wanarusha matangazo yao.
Nadhani umeelewa hoja yangu vizuri tu, sina maelezo mengine ya ziada kuhusu suala hilo. Ila unafaa ufahamu kwamba kwenye kiswahili, sawa na lugha yeyote nyingine, kuna maneno ambayo yana maana zaidi ya moja. Tena nadhani 'kubanduliwa' kama mnavolitumia nyie ni kama 'slang' na maana yake hiyo sio rasmi. Huwezi ukawalaumu Citizen Tv kwa kulitumia neno hilo, kisa eti lina maana nyingine kwa lugha ya mitaa. Kuna mifano mingine mingi tu kwenye kiswahili sanifu. K.m Kupiga pambaja- Kukumbatia, Mwendazake- Marehemu, Nyanya- Bibi n.k, n.k.Nakuhakikishia kwamba hapo Citizen Tv hakuna anayefahamu kwamba 'kubanduliwa' lina maana nyingine, tofauti na walichonuia kwenye caption yao hiyo?Kwa hiyo wao wanatumia misamiati ya kiswali bila ya kuangalia kwanza na kufanya tafiti kujua watu wengi huwa wanatumiaje neno husika wakati wanajua kabisa hiyo TV yao inatazamwa Tanzania?