Padri amekaa katika chumba cha kuungamisha, kanisani hakuna mtu. Mara muumini mmoja<br />
akaingia, akapiga magoti upande wa pili wa meza na kufanya ishara ya msalaba<br />
akaanza kuungama.<br />
<br />
Akisema "Padri naungama dhambi zangu, leo nimefanya dhambi kubwa sana"<br />
<br />
Padri "endelea"<br />
<br />
"Bosi wangu aliniita nyumbani kwake akaniambia amegundua nimeiba shilingi milioni<br />
50, akasema nisipotoa maelezo ya kutosha atanipeleka polisi , ukweli mimi naogopa<br />
kufungwa, nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke yetu, nikachomoa<br />
bastola nikamuua. <br />
Je ! Yesu atanisamehe?"<br />
<br />
Padri "utasamehewa"<br />
<br />
"Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango unafunguliwa, kutazama loh, mke wa<br />
bosi. Akaniuliza nimemfanya nini mume wake. Kutazama huku na huku nikagundua tuko<br />
wawili peke yetu, nikamuua na yeye. <br />
Je ! Yesu atanisamehe na hiyo?"<br />
<br />
Padri "utasamehewa" <br />
<br />
"nikatoka nje, nikawasha gari niondoke lakini mlinzi akakataa kufungua geti akasema<br />
amesikia kama kishindo hivi! Nikaona ananiwekea kiwingu. Kutazama huku na huku<br />
nikagundua tuko wawili peke yetu nikamuua. <br />
Je ! Yesu atanisamehe?"<br />
<br />
Padri "utasamehewa"<br />
<br />
"nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda nyumbani, wakati napanga kuja kanisani<br />
kuungama dhambi mtoto wa bosi akabisha hodi nikawaza mambo gani tena ! Akasema<br />
amefika nyumbani na kukuta yaloyotokea, lakini akanionyesha diary ya baba yake<br />
inayoonesha kuwa nilikuwa na appointment naye kabla hajafa. Nikamuuliza nani<br />
mwingine anajua? akasema ameanzia kwangu kisha atakwenda polisi. Nikatazama huku na<br />
huku nikagundua tuko wawili peke yetu nikamuua. Diary nikaichoma moto. <br />
Je ! Yesu atanisamehe na hilo?"<br />
<br />
Padri - kimya.......................................<br />
<br />
"Padriiii, Je Yesu atanisamehe kwa hilo?"<br />
<br />
- kimya..................................<br />
<br />
Jamaa kutazama kwenye box la maungamo padri hayupo. <br />
Lakini kwenye kona moja akaona kabati la nguo za mapadri kama linatikisika! <br />
Kufungua akamuona padri kajificha katikati ya majoho anatetemeka sana.<br />
<br />
"Sasa baba Paroko mbona umenikimbia?"<br />
<br />
Padri kwa taabu akajibu ;<br />
<br />
"nilitazama huku na huku nikagundua kuwa tuko wawili peke yetu........"