Umenijibu vyema sana.Hint tu,Mkaguzi wa mahesabu na Muhasibu watu hawa wataelewa tofauti na injinia na watu wengine wenye taaluma nyingine.
Wenye taaluma za Ukaguzi wa mahesabu na Muhasibu wanaelewa nini maana ya CAG na ripoti zake,hasa pale anapofanya Independent Investigation au auditing,watu hawa wanajua vigezo vitumikavyo mpaka kupata FACTS.Hawamuangalii mtu wala kusikiliza unasema nini.Wanatafuta FACTS za kubainisha kama kuna wizi au la.Na ndiyo maana imeelezwa wamepeleka information TAKUKURU ifanyiwe kazi,sababu siyo field yao kutafiti kama kuna RUSHWA au la.Wameona kuna FACTS za RUSHWA lakini mwenye taaluma hiyo yupo,wamempelekea FACTS azifanyie kazi.
Wametafuta FACTS kama kuna wizi wameziainisha vyema na kuzitoa kwa lugha nyepesi kwa wale waliowatuma wakiamini kuwa kuna wasiyo wahasibu au auditors na lugha yao ya kitaaluma ingekuwa ngumu kueleweka.
Wahasibu na auditors hakika watajua nini kichambuliwe vipi,na wataoanisha facts zilizotolewa ili wapate uhakika.Hivyo basi kwa uhakika kabisa ripoti ya CAG ndiyo yenye UKWELI USIOKUWA NA PINGAMIZI,wameweka FACTS zilizofanyiwa kazi kwa UTAALAMU wa hali ya juu bila kuweka visasi,uzushi,uwongo nk nk.
Nadhani utakuwa umenielewa japo kidogo.