Otomyiasis: Funza kuishi ndani ya sikio lako

Otomyiasis: Funza kuishi ndani ya sikio lako

Traxtion

JF-Expert Member
Joined
Dec 10, 2021
Posts
6,086
Reaction score
12,225
Unaweza ku imagine kuishi huku unajua kuna funza wapo hai ndani kabisa ya sikio lako, na wanapata chakula, hewa na mahitaji yote wanayohitaji ili kuishi.

Ufahamu ugonjwa wa OTOMYIASIS

Otomyiasis ni hali ambapo funza huishi na kukua ndani ya sikio la binadamu au mnyama. Hii hutokea pale nzi anapotaga mayai yake ndani au karibu na sikio, na mayai hayo huanguliwa na kuwa funza.

Mwishoni nimeweka video ya jinsi funza hao wanavyoondolewa kwenye sikio la binadamu

1. Unasababishwa na Nini?
Otomyiasis husababishwa na larva (funza) za nzi mbalimbali, hasa wale wanaojulikana kama "blowflies" au "botflies." Nzi hawa hutaga mayai yao kwenye majeraha, ngozi iliyovunjika, au maeneo yenye harufu mbaya, ikiwemo sikio.

2. Unapatikana Sana Nchi Gani?
Ugonjwa huu hupatikana sana katika nchi za kitropiki na zile zenye hali ya hewa ya joto na unyevunyevu, ambapo inzi huzaliana kwa wingi. Mara nyingi huonekana katika maeneo yenye usafi duni na yenye kuishi karibu na wanyama.

3. Unajilinda Vipi Ili Usikupate?
Ili kujikinga na otomyiasis, fanya yafuatayo:
* Zingatia usafi binafsi: Safisha masikio na miili yako mara kwa mara.
* Kinga majeraha: Funika majeraha yoyote kwenye ngozi, hasa karibu na masikio, ili kuzuia nzi kutaga mayai.
* Epuka kulala nje: Hususan katika maeneo yenye nzi wengi au usafi duni.
* Tumia vyandarua: Unapolala, hasa katika maeneo hatarishi.
4. Tiba Yake ni Ipi?
Tiba ya otomyiasis huhusisha kuondoa funza hao kutoka masikioni. Hii hufanywa na wataalamu wa afya, mara nyingi kwa kutumia zana maalum au dawa zinazoweza kuwaua au kuwafanya watoke. Baada ya kuondolewa, jeraha au eneo lililoathirika husafishwa na kutibiwa ili kuzuia maambukizi zaidi.

Tazama video hii uone jinsi funza hao wanavyoondolewa masikioni
 
dalili zake ni zipi?
Dalili za Otomyiasis ni
1. Maumivu makali ya sikio
Sikio linakiwa linauma sana kwa ndani huku unahisi kuna vitu vinatembea ndani ya sikio lako.

2. Kutokwa na usaha au majimaji meusi sikioni
Usaha na majimaji machafu yenye harufu mbaya yanakuwa yanatoka sikioni

3. Kupungua kwa uwezo wa kusikia
Unakuwa na uwezo mdogo wa kusikia kupitia sikio lililoathirika maana funza wanakuwa wameziba njia. Muda mwingine unapoteza uwezo wa kusikia kabisa kwenye sikio lililoathirika

4. Kuwashwa sana sikioni.
Mara kwa mara kunakuwa na muwasho mkali sana ndani ya sikio, na unatokana na funza kutekenya sikio wakati wanatembea ndani ya sikio. Muda mwingine muwasho huu unaambatana na maumivu makali.

5. Kuwepo kwa funza wenyewe: Mara chache, funza wanaweza kuonekana wakitambaa au kutambaa hadi nje ya sikio. Unawaona wanatoka nje ya sikio na kurudi ndani. Otomyiasis inaweza kufanya uwe na funza hata watano au hadi funza mia moja. Haijalishi idadi, wakiwa wengi wataanza kutoka nje na wengine kurudi ndani
Wengine huwa wanatafuta nafasi na kuzama ndani zaidi ya sikio, kufikia maeneo ambayo sio rahisi kufikika
 
Dalili za Otomyiasis ni
1. Maumivu makali ya sikio
Sikio linakiwa linauma sana kwa ndani huku unahisi kuna vitu vinatembea ndani ya sikio lako.

2. Kutokwa na usaha au majimaji meusi sikioni
Usaha na majimaji machafu yenye harufu mbaya yanakuwa yanatoka sikioni

3. Kupungua kwa uwezo wa kusikia
Unakuwa na uwezo mdogo wa kusikia kupitia sikio lililoathirika maana funza wanakuwa wameziba njia. Muda mwingine unapoteza uwezo wa kusikia kabisa kwenye sikio lililoathirika

4. Kuwashwa sana sikioni.
Mara kwa mara kunakuwa na muwasho mkali sana ndani ya sikio, na unatokana na funza kutekenya sikio wakati wanatembea ndani ya sikio. Muda mwingine muwasho huu unaambatana na maumivu makali.

5. Kuwepo kwa funza wenyewe: Mara chache, funza wanaweza kuonekana wakitambaa au kutambaa hadi nje ya sikio. Unawaona wanatoka nje ya sikio na kurudi ndani. Otomyiasis inaweza kufanya uwe na funza hata watano au hadi funza mia moja. Haijalishi idadi, wakiwa wengi wataanza kutoka nje na wengine kurudi ndani
Wengine huwa wanatafuta nafasi na kuzama ndani zaidi ya sikio, kufikia maeneo ambayo sio rahisi kufikika
je nkiwa naskia filimbi masikioni na vitu kama mashine inaunguruma pamoja na kizungu zungu ni dalili za huo ugonjwa?
 
Back
Top Bottom