bidam90
JF-Expert Member
- Aug 28, 2013
- 273
- 193
Top 10 Wasanii wa Bongofleva matajiri mwaka 2015..
Kama kuna kitu ambacho unaweza kukitofautisha wakati mziki wa bongofleva unaanza hadi leo basi bila shaka ni thamani ya mziki ho kuongezeka mara dufu. Ni juzi tu hapa alikiba alihojiwa na kudai aliuza copy milioni 2 za album yake ya kwanza ya Cinderella na kuambulia shilingi 200 kwa kila copy .
Hivi sasa mziki umebadilika na Bongoweekly tumeamua kukaa mezani na kupiga hesabu ya wasanii matajiri kutokana na kazi zao wanazofanya katika mziki wa Bongo fleva na mikataba mbalimbali ya kibiashara. Twende kazi..
10. Joh Makini
Kama unadhani Joh Makini hana pesa basi ?Don?t bother? . Ni juzi tu hapa ametoka kushot video aliyomshirikisha AKA huko nchini Afrika Kusini ambayo iliyomgharimu milioni 32 za kitanzania . Kabla ya hapo Joh Makini aliingia gharam nyingine huko huko SA kushoot video ya ?Nusu nusu ? . Ni wazi kama kuna mwaka ambao umemtajirisha mwamba wa kaskazini basi ni mwaka 2015 kwani anatarajiwa kutoa audio na video na Davido ambayo ni wazi itamgharimu sana.
09. Linah
Nani atasahau mwanzoni mwa mwaka mwanadada Linah alipotoa Dola 47,000 , zaidi ya milioni 100 za bongo kwenda Afrika Kusini kutengeneza video ya Ole Themba . Pia Linah aliteuliwa kua balozi wa kinywaji cha Jebel kitu ambacho tkimemuongezea kipato. Mwaka 2015 linah ameweza kutengeneza pesa za kutosha kupitia mziki kiasi cha kustahili kuingia kwenye hii listi.
08. Jux
Baada ya kuachia ngoma ya ?Uzuri wako? , maisha ya kimziki ya jux hajarudi nyuma tena na mwaka huu jux ameweza kuingiza pesa za kutosha kupitia mziki wake. Ni juzi juzi hapa jux alipost picha la begi likiwa na noti za pesa za kimarekani huku akiandika kwamba aliona milioni 200 alipokua na miaka 22 . Ukiachana na hizo pesa za instagram , mpenzi huyu wa mwanadada Vanessa Mdee mwaka huu ameweza kuporomosha bonge moja la ikulu lenye hadhi ya kistaa lina studio ya kurekodi, Gym kwa ajili ya mazoezi na Bwawa la Kuogelea ndani.
07. Shettah
Unaweza kumuita shikorobo master . Shetta naye ni miongoni mwa wasanii waliofanya vizuri mwaka huu na kuingiza pesa za kutosha hasa kutokana na show zake za nje na Biashara. Juzijuzi Alizushiwa kwamba anauza Unga Afrika Kusini kutokana na kwenda mara kwa mara na kukanusha kwa kuwaambia mashabiki wake kwamba anaingiza pesa kupitia mziki na kutumia pesa hizo kufanya biashara nyingine.
06. Nay wa Mitego
Kati ya wanamuziki wafanyabiashara na wanaojua kuwekeza kwenye Mziki basi huwezi kumuacha Nay wa Mitego . Mwaka 2015 ameendelea kujitajirisha kupitia mziki wake na mikataba ya kibiashara hususani na kampuni ya simu za mikononi ya Airtel.
05. Professor Jay
Mmbunge mteule wa mikumi hakusikika sana kwenye mziki mwaka huu lakini bado ameweza kuendeleza utajiri wake kupitia uwekezaji kwenye vitu kadhaa kama Studio. Baada ya kupata ubunge , Professor Jay ameahidi kuendeleza kasi yake katika mziki huku akiwa anaingiza mkwanja wa kutosha kila siku akizama mjengoni.
04. AY
Kwasasa anatamba na ngoma yake ya ?Zigo? , AY anaingiza pesa nyingi kupitia mikataba mbalimbali ya kibiashara na kampeni mbalimbali za kimataifa kama Balozi. Mwaka Jana akiwa na wasanii wenzake 9 alitembelea Ikulu ya Marekani. Pia mwishoni mwa mwaka Jana aliachia ngoma ya "Touch Me" aliyomshirikisha Sean Kingston hivyo kujipanulia wigo la ukuaji wake kiuchumi.
03. Ali Kiba
Ndio, Kama kuna mtu ambae ameshawahi kukutana na Ali kiba laivu basi atakubaliana na mimi kua sio mtu anayeonyesha kua ana pesa lakini hali hio haimfanyi kutokua namba 3 kwani ukiacha namba 1 kwenye list hii , Ali Kiba ndio msanii aliyejitajirisha mwaka huu kupitia mziki. Amefanya show nyingi sana nje na ndani ya nchi , amesaini mikataba ya kibalozi ya kutosha na gharama zake kwa show moja ni balaa mfano mzuri ni ile karatasi ya CCM iliyovuja ikionyesha pesa watazopata wasanii kwenye kampeni ambapo ali kiba alikua wa pili akipata milioni 60 kwa show 4 .
02. Lady Jaydee
Unaweza kumuita malkia wa mziki wa Bongo Fleva . Mwaka huu aliweza kuachia ngoma na video kadhaa japokua sio sababu yupo namba 2 kwani tayari alikua anaendeleza utajiri aliyokwisha jikusanyia miaka na miaka.
01. Diamond Platnumz
Kuna mtu anabisha ?? nadhani huyu amepitwa bila kupingwa . Muite Mfalme wa Bongo Fleva kwasasa na sio tu ni namba moja kwenye list hii bali hata ukitengeneza ya Afrika unaweza usimkose mzee mwenyewe Platnumz . Mwaka 2015 umezidi kumtajirisha Platnumz huku akimalizia Ikulu / Nyumba yake ya 10 kuijenga ikiwa na choo chenye Dhahabu , thamani yake ikiwa milioni 70 . Ebwanae , hicho choo wasiingize kila mtu maana usawa wenyewe huu?.Diamond ameweza kujiongezea mikataba kibao na makampuni ya ndani na nje ya nchi na mwisho wa siku pesa yake kubwa inaingia kupitia mauzo ya muziki wake na show huku akiwa ndio msanii ghali Tanzania.
Chanzo: Bongo Weekly
Kama kuna kitu ambacho unaweza kukitofautisha wakati mziki wa bongofleva unaanza hadi leo basi bila shaka ni thamani ya mziki ho kuongezeka mara dufu. Ni juzi tu hapa alikiba alihojiwa na kudai aliuza copy milioni 2 za album yake ya kwanza ya Cinderella na kuambulia shilingi 200 kwa kila copy .
Hivi sasa mziki umebadilika na Bongoweekly tumeamua kukaa mezani na kupiga hesabu ya wasanii matajiri kutokana na kazi zao wanazofanya katika mziki wa Bongo fleva na mikataba mbalimbali ya kibiashara. Twende kazi..
10. Joh Makini
Kama unadhani Joh Makini hana pesa basi ?Don?t bother? . Ni juzi tu hapa ametoka kushot video aliyomshirikisha AKA huko nchini Afrika Kusini ambayo iliyomgharimu milioni 32 za kitanzania . Kabla ya hapo Joh Makini aliingia gharam nyingine huko huko SA kushoot video ya ?Nusu nusu ? . Ni wazi kama kuna mwaka ambao umemtajirisha mwamba wa kaskazini basi ni mwaka 2015 kwani anatarajiwa kutoa audio na video na Davido ambayo ni wazi itamgharimu sana.
09. Linah
Nani atasahau mwanzoni mwa mwaka mwanadada Linah alipotoa Dola 47,000 , zaidi ya milioni 100 za bongo kwenda Afrika Kusini kutengeneza video ya Ole Themba . Pia Linah aliteuliwa kua balozi wa kinywaji cha Jebel kitu ambacho tkimemuongezea kipato. Mwaka 2015 linah ameweza kutengeneza pesa za kutosha kupitia mziki kiasi cha kustahili kuingia kwenye hii listi.
08. Jux
Baada ya kuachia ngoma ya ?Uzuri wako? , maisha ya kimziki ya jux hajarudi nyuma tena na mwaka huu jux ameweza kuingiza pesa za kutosha kupitia mziki wake. Ni juzi juzi hapa jux alipost picha la begi likiwa na noti za pesa za kimarekani huku akiandika kwamba aliona milioni 200 alipokua na miaka 22 . Ukiachana na hizo pesa za instagram , mpenzi huyu wa mwanadada Vanessa Mdee mwaka huu ameweza kuporomosha bonge moja la ikulu lenye hadhi ya kistaa lina studio ya kurekodi, Gym kwa ajili ya mazoezi na Bwawa la Kuogelea ndani.
07. Shettah
Unaweza kumuita shikorobo master . Shetta naye ni miongoni mwa wasanii waliofanya vizuri mwaka huu na kuingiza pesa za kutosha hasa kutokana na show zake za nje na Biashara. Juzijuzi Alizushiwa kwamba anauza Unga Afrika Kusini kutokana na kwenda mara kwa mara na kukanusha kwa kuwaambia mashabiki wake kwamba anaingiza pesa kupitia mziki na kutumia pesa hizo kufanya biashara nyingine.
06. Nay wa Mitego
Kati ya wanamuziki wafanyabiashara na wanaojua kuwekeza kwenye Mziki basi huwezi kumuacha Nay wa Mitego . Mwaka 2015 ameendelea kujitajirisha kupitia mziki wake na mikataba ya kibiashara hususani na kampuni ya simu za mikononi ya Airtel.
05. Professor Jay
Mmbunge mteule wa mikumi hakusikika sana kwenye mziki mwaka huu lakini bado ameweza kuendeleza utajiri wake kupitia uwekezaji kwenye vitu kadhaa kama Studio. Baada ya kupata ubunge , Professor Jay ameahidi kuendeleza kasi yake katika mziki huku akiwa anaingiza mkwanja wa kutosha kila siku akizama mjengoni.
04. AY
Kwasasa anatamba na ngoma yake ya ?Zigo? , AY anaingiza pesa nyingi kupitia mikataba mbalimbali ya kibiashara na kampeni mbalimbali za kimataifa kama Balozi. Mwaka Jana akiwa na wasanii wenzake 9 alitembelea Ikulu ya Marekani. Pia mwishoni mwa mwaka Jana aliachia ngoma ya "Touch Me" aliyomshirikisha Sean Kingston hivyo kujipanulia wigo la ukuaji wake kiuchumi.
03. Ali Kiba
Ndio, Kama kuna mtu ambae ameshawahi kukutana na Ali kiba laivu basi atakubaliana na mimi kua sio mtu anayeonyesha kua ana pesa lakini hali hio haimfanyi kutokua namba 3 kwani ukiacha namba 1 kwenye list hii , Ali Kiba ndio msanii aliyejitajirisha mwaka huu kupitia mziki. Amefanya show nyingi sana nje na ndani ya nchi , amesaini mikataba ya kibalozi ya kutosha na gharama zake kwa show moja ni balaa mfano mzuri ni ile karatasi ya CCM iliyovuja ikionyesha pesa watazopata wasanii kwenye kampeni ambapo ali kiba alikua wa pili akipata milioni 60 kwa show 4 .
02. Lady Jaydee
Unaweza kumuita malkia wa mziki wa Bongo Fleva . Mwaka huu aliweza kuachia ngoma na video kadhaa japokua sio sababu yupo namba 2 kwani tayari alikua anaendeleza utajiri aliyokwisha jikusanyia miaka na miaka.
01. Diamond Platnumz
Kuna mtu anabisha ?? nadhani huyu amepitwa bila kupingwa . Muite Mfalme wa Bongo Fleva kwasasa na sio tu ni namba moja kwenye list hii bali hata ukitengeneza ya Afrika unaweza usimkose mzee mwenyewe Platnumz . Mwaka 2015 umezidi kumtajirisha Platnumz huku akimalizia Ikulu / Nyumba yake ya 10 kuijenga ikiwa na choo chenye Dhahabu , thamani yake ikiwa milioni 70 . Ebwanae , hicho choo wasiingize kila mtu maana usawa wenyewe huu?.Diamond ameweza kujiongezea mikataba kibao na makampuni ya ndani na nje ya nchi na mwisho wa siku pesa yake kubwa inaingia kupitia mauzo ya muziki wake na show huku akiwa ndio msanii ghali Tanzania.
Chanzo: Bongo Weekly