Kichancheda
Senior Member
- Oct 29, 2012
- 142
- 46
Hapa kinchozungumzwa sio sales turnover. Utajiri wanazungumzia thamani ya hisa alizonazo mtu kwa kila kampuni ambayo amewekeza hisa zake. Zile hisa ndio hufanyiwa tathmini na kuamua mtu ni tajiri kwa kiasi gani. Tatizo letu Tanzania inakuwa vigumu kutathmini thamani ya hisa za matajiri kwa sababu hawatoi takwimu sahihi hasa kwenye ulipaji kodi na kampuni nyingi haziko kwenye soko la hisa.
hisa si ndio shares? thamani ya mtaji wako kwenye kampuni. Na hiyo thamani inapatikana kwenye asset.Na ukubwa wa thamani ya asset ndio una determine uwezo wa biashara yako kuingiza faida, faida na mauzo ndio mpango mzima.Sasa inashindikana nini kupima mitaji ya local investors wa kibongo? Hata kama hawako kwenye soko la hisa?