Kecha Boksi
Member
- Nov 5, 2010
- 55
- 107
Habarini wana bodi!
Tafadhalini rejea kichwa cha habari hapo juu.
Hivi karibuni nimekutana na tathmini ya biashara moja ya kukoboa na kusaga mahindi iliyopo mkoa wa jirani na Dar inaonyesha kuwa wana profit margin ya 98% katika mwaka wa kibiashara uliopita. Nikajaribu kudadisi zaidi kwa biashara nyingine zinazofanana na hizo nikakuta wenyewe wanarange 10% hadi 65%.
Nikabaki na maswali mengi najiuliza ina maana biashara ya kusaga na kukoboa nafaka inaweza ikawa na profit margin kubwa kiasi hicho kwa mwaka uliopita ukiachilia mbali changamoto mbali mbali zinazoikabili sekta hii ikiwemo ya umeme usioaminika na bei yake kuwa juu au kuna ka uchakachuaji katika zoezi la kuandaa hizo taarifa?!
Naombwa kujuzwa wakuu, kwa wenye ujuzi na uzoefu wa hii kitu je inaweza kuwa kweli kwa mazingira yetu haya ya kibiashara humu nchini kuwa na profit margin hiyo kwa biashara ya kusaga na kukoboa nafaka (mahindi)? Na je kwa mliobahatika kuona / kupitia / kuandaa taarifa kama hizo range ya profit margin ilikua ngapi kwa maeneo hayo?
Naomba kuwakilisha na karibuni kwa michango yenu!
Tafadhalini rejea kichwa cha habari hapo juu.
Hivi karibuni nimekutana na tathmini ya biashara moja ya kukoboa na kusaga mahindi iliyopo mkoa wa jirani na Dar inaonyesha kuwa wana profit margin ya 98% katika mwaka wa kibiashara uliopita. Nikajaribu kudadisi zaidi kwa biashara nyingine zinazofanana na hizo nikakuta wenyewe wanarange 10% hadi 65%.
Nikabaki na maswali mengi najiuliza ina maana biashara ya kusaga na kukoboa nafaka inaweza ikawa na profit margin kubwa kiasi hicho kwa mwaka uliopita ukiachilia mbali changamoto mbali mbali zinazoikabili sekta hii ikiwemo ya umeme usioaminika na bei yake kuwa juu au kuna ka uchakachuaji katika zoezi la kuandaa hizo taarifa?!
Naombwa kujuzwa wakuu, kwa wenye ujuzi na uzoefu wa hii kitu je inaweza kuwa kweli kwa mazingira yetu haya ya kibiashara humu nchini kuwa na profit margin hiyo kwa biashara ya kusaga na kukoboa nafaka (mahindi)? Na je kwa mliobahatika kuona / kupitia / kuandaa taarifa kama hizo range ya profit margin ilikua ngapi kwa maeneo hayo?
Naomba kuwakilisha na karibuni kwa michango yenu!