Optimal Profit Margin for Grain Milling Business in Tz

Kecha Boksi

Member
Nov 5, 2010
55
107
Habarini wana bodi!

Tafadhalini rejea kichwa cha habari hapo juu.

Hivi karibuni nimekutana na tathmini ya biashara moja ya kukoboa na kusaga mahindi iliyopo mkoa wa jirani na Dar inaonyesha kuwa wana profit margin ya 98% katika mwaka wa kibiashara uliopita. Nikajaribu kudadisi zaidi kwa biashara nyingine zinazofanana na hizo nikakuta wenyewe wanarange 10% hadi 65%.

Nikabaki na maswali mengi najiuliza ina maana biashara ya kusaga na kukoboa nafaka inaweza ikawa na profit margin kubwa kiasi hicho kwa mwaka uliopita ukiachilia mbali changamoto mbali mbali zinazoikabili sekta hii ikiwemo ya umeme usioaminika na bei yake kuwa juu au kuna ka uchakachuaji katika zoezi la kuandaa hizo taarifa?!

Naombwa kujuzwa wakuu, kwa wenye ujuzi na uzoefu wa hii kitu je inaweza kuwa kweli kwa mazingira yetu haya ya kibiashara humu nchini kuwa na profit margin hiyo kwa biashara ya kusaga na kukoboa nafaka (mahindi)? Na je kwa mliobahatika kuona / kupitia / kuandaa taarifa kama hizo range ya profit margin ilikua ngapi kwa maeneo hayo?

Naomba kuwakilisha na karibuni kwa michango yenu!
 
Habarini wana bodi!

Tafadhalini rejea kichwa cha habari hapo juu.

Hivi karibuni nimekutana na tathmini ya biashara moja ya kukoboa na kusaga mahindi iliyopo mkoa wa jirani na Dar inaonyesha kuwa wana profit margin ya 98% katika mwaka wa kibiashara uliopita. Nikajaribu kudadisi zaidi kwa biashara nyingine zinazofanana na hizo nikakuta wenyewe wanarange 10% hadi 65%.

Nikabaki na maswali mengi najiuliza ina maana biashara ya kusaga na kukoboa nafaka inaweza ikawa na profit margin kubwa kiasi hicho kwa mwaka uliopita ukiachilia mbali changamoto mbali mbali zinazoikabili sekta hii ikiwemo ya umeme usioaminika na bei yake kuwa juu au kuna ka uchakachuaji katika zoezi la kuandaa hizo taarifa?!

Naombwa kujuzwa wakuu, kwa wenye ujuzi na uzoefu wa hii kitu je inaweza kuwa kweli kwa mazingira yetu haya ya kibiashara humu nchini kuwa na profit margin hiyo kwa biashara ya kusaga na kukoboa nafaka (mahindi)? Na je kwa mliobahatika kuona / kupitia / kuandaa taarifa kama hizo range ya profit margin ilikua ngapi kwa maeneo hayo?

Naomba kuwakilisha na karibuni kwa michango yenu!
Profit margin ya 98% sounds very unrealistic kwa mazingira yetu! Gharama ya umeme,mafuta, wafanyakazi etc
 
Ndicho nilichokiwaza mkuu SMU, vp we kwa uzoefu wako PM kwa biashara hizo huwa inarange ngapi kwa maeneo uliyopo?
 
Mkuu naona unafanya kautafiti kidogo, na pengine wanajamvi tunajibu questioner zako bila kujua. Anyway hebu jaribu kupitia hiyo report vizuri maana nafaka hapa kwetu haina kodi na hii inaweza kua moja ya incentive kusukuma profit margin lakini sio kwa asilimia hizo tajwa,
Kuna makampuni kama Azania wanaagiza ngano kutoka Russia wanaikoboa na kupaki unga wanauuza hapa nchini na nje ila hakuna kodi, hata mkopo waliowezeshwa na mkulu hawana mpango wakurudisha. Sasa sijui profit margin zao zikoje hawa.
 
Mwanahisa, sipo kwenye kautafiti mkuu. Ingekua ni kautafiti ningemwomba Invisible aniwekee link ya questionnaire yangu hapo juu ili kila mdau atakaeguswa achangie mawazo!! Najaribu tu kupata uzoefu na mawazo ya wadau ili niondoe huu wasiwasi niliokua nao.

Enewei, nimeipata point yako mkuu. Ila kwa hawa wenye biashara za kiwango cha chini na cha kati huwa wanalipa ushuru wa mazao wanapofata malighafi sokoni + kodi ya mapato. Kwa hao wakubwa nafikiri ni muendelezo wa udahifu wa sirikali yetu ndo maana nchi haimbulii chochote kwenye biashara zao.

Vipi kwa eneo ulilopo PM za wale wenye biashara hizi katika small scale na medium zinarange ngapi?
 
Ndicho nilichokiwaza mkuu SMU, vp we kwa uzoefu wako PM kwa biashara hizo huwa inarange ngapi kwa maeneo uliyopo?
Labda kuna kitu tukiweke sawa kwanza kabla hatujaendelea. Hii biashara ya 'kukoboa na kusaga' tunayoizungumzia, ile ya wewe kununua mazao, kuyakoboa/kusaga, na kisha kuuza (products only) au ni biashara ambayo wewe unamiliki mashine tu za kukoboa na kusaga na kutoa huduma hiyo kibiashara kwa watu wengine (services only) au ni both?
 
Labda kuna kitu tukiweke sawa kwanza kabla hatujaendelea. Hii biashara ya 'kukoboa na kusaga' tunayoizungumzia, ile ya wewe kununua mazao, kuyakoboa/kusaga, na kisha kuuza (products only) au ni biashara ambayo wewe unamiliki mashine tu za kukoboa na kusaga na kutoa huduma hiyo kibiashara kwa watu wengine (services only) au ni both?

Hii biashara tunayoizungumzia ni ile ya mtu kumiliki mashine ya kukoboa na kusaga, either akiwa anafanya toll milling (kutoa huduma) au anafanya resale (ananunua mzigo - mahindi na kuuza unga) au anafanya zote.
 
Back
Top Bottom