Operesheni Kimbunga yazoa mawaziri

Operesheni Kimbunga yazoa mawaziri

Hivi ni kweli bei ya mbege imeshuka kwa asilimia 75?

Inadhirisha ni jinsi gani unatumia kichwa kufugia nywele, badala ya kutumia kichwa kujadili mawazo yenye tija.. Gambaz mnamatatizo sana.
 
Tanzania bwana. Watu wameona wanaingiliwa kwenye ulaji wao tayari oporesheni tokomeza wameitokomeza !!!? Cheza na majangili wewe!!!.
 
Noted: ccm=serikali=sotoka.
obvious,
wanachama (gambaz) +wafuasi=sotoka
 
WASIFU WA LUKOSI 1.Huyu jamaa alikuwa polisi akafukuzwa sababu ya ajali katika msafara wa pm wakati ule John Malecela na kukimbilia Botwana ...

Mkuu hapo kwenye red; are you serious? Mbona anatemaga sana pumba tofauti na age yake? IQ yake lazima itakuwa extremely very low! Kubwa-jinga type.
 
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ni janga la Taifa. The guy is butterfingered and forbearing. Sometimes You can't differenciate him with klutzy.

God forbid, ninatumaini Waziri Mkuu wa aina ya Mizengo Pinda atakuwa wa kwanza na mwisho nchini. It's pathetic to say the least.

Maamuzi ya huyu jamaa yako kisiasa utadhani ni katibu mkuu wa CCM anaogopa kukosa wanachama wakati ni mtendaji Serikalini.

Huwa wakati mwingine nashindwa kuamini kama ni mwanasheria ambaye anafahamu kazi ya serikali ni utekelezaji ndani ya rule of the law ambapo kila mtu yuko accountable under the law.

Sheria hazina siasa, na serikali ikianza kuweka siasa kwenye sheria inafikia sehemu hata wananchi wanashindwa kutofautisha kati ya chama na serikali. Hili ndilo linalofanyika Tanzania kwa sasa ambapo watu wanavunja sheria wakitegemea hawawezi kushughulikiwa kisheria(kesi ya malori na barabara).

Mawaziri kama Magufuri na Mwakyembe wakichukua maamuzi ya kiserikali kisheria, anawapiga stop for apparent NO sensible reason. Kwa nchi kama Tanzania inayopitia mpito wa kisiasa, kiuchumi na kijamii, huwezi kuwa na viongozi wakuu wa nchi ambao character zao zinakaribia kufanana halafu mambo yakaenda vizuri na kwa kasi kuendana na mapitio ya nchi. Tanzania ya sasa inahitaji Rais au Waziri Mkuu ambaye ni mkali lakini pia awe firm and fair. Mh. Lowassa was one of them.

Nenda mbele, rudi nyuma. Mh. Lowassa alikuwa ni aina ya Mawaziri wakuu wanaohitajika kwa Tanzania ya sasa. Take it or leave it. Tangu aachie madaraka, utawala wa Rais Kikwete ndipo ulipoanza kuwa butu katika maamuzi magumu.

Kuna watu huwa wanadai Mh. Lowassa ni fisadi lakini wameshindwa kubainisha ufisadi wake uko wapi na hasa ikichukuliwa kuwa sheria za maadili ya wafanyakazi ( wabunge) zinawataka kuweka kila wanachomiliki na kama ikitokea wamedanganya na ikagundulika, basi kuanzia siku hiyo waliyogundulika ubunge wao unakoma na wanapelekwa mahakamani. Kwa nini hajapatikana mtu wa kudhibitisha kama kweli Mh. Lowassa ni fisadi pamoja na kuwa na maadui kwa makumi na mamia wa kisiasa?. Habari zinakuwa niza kiudaku na hearsay zaidi ya ukweli.

Hata Dr. Slaa alichagiza kuhusu sheria ya maadili kuhusiana na kadhia ya utajiri wa Mbowe lakini cha kushangaza pamoja na kudai Mh. Lowassa ni fisadi hajaweza kuitumia hii sheria kuchukua mkondo wake,
Boscontaganda na WanaJF,
Uchambuzi na mchango wowote wa maana ni ule uliofanyiwa utafiti, haunt ushabiki, na au katika dhamira safi una nia ya kutaka kufahamu jambo. Hapa Thread hii ni ya kutupotezea muda, kwa kuwa ushabiki unatawala kuliko dhamira na nia njema.
I) Kuna watu wanafanya biashara halali ndani na nje ya nchi, na hawa Kama ni Wabunge au kundi lililotajwa na Sheria, huhitaji kuwa mganga wa kienyeji kubuni na kuchafua majina ya watu. Hatua ya kwanza, Kama hamuifahamu niwasaidie bure, ambayo ni ya kisheria unaenda Tume ya Maadili ya Viongozi, unalipia fee ndogo, nadhani Tshs 1500, Kama haijapanda, unakagua Fomu za Maadili ya Kiongozi husika. Kama ni Mbunge, Kama hajajaza Mali hiyo, akaunti, nyumba au share kwenye Kampuni ya Nje, kisheria ushahidi ukitolewa wa uhakika kuwa Ana Mali nje na Haipo kwenye Fomu anapoteza ubunge wake automatically. Hivyo si masuala ya ushabiki, wala siyo la Wanachadema kuwewesekea. Ni dhahiri waleta thread hawakufanya home work yao, au wameweka ushabiki mbele, au tu wana agenda Yao ya siri.

https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...-ngeleja-wahojiwa-18.html#post7638759[/QUOTE]
 
...mbunge wa
Busega Dk.Titus Kamani
(CCM),aliifananisha
serikali ya CCM na
ugonjwa wa miguu
na midomo kwenye
mifugo,maarufu
kama "Sotoka",ambao miaka ya
nyuma ulikuwa
ukiua ng’ombe
wengi...

HERI MIMI SIJASEMA!

Huyo dr Kamani angekuwa CDM alafu ndo anaikosoa sijui kingemkuta nini?CCM baba lao katika Uvumilivu wa kukosoana
 
Nini lawama?Kama unao uwezo wa kisiasa ni bora ukajiunge au ujiingize ktk siasa kuliko kuwakosoa hao watu wenu au ni bora ungeenda bungeni ukawapigia kelele humo humo ukapata na posho.(mzee wa Gambosh macho makavu)
 
ila jamani km umemsikia mbunge (ccm)
kangi lugola akiongea basi sidhani km unaweza kuishabikia ccm.
inauma sn jamani.


eti askari wamepiga risasi na kuuwa ng'ombe 60za mzee m1 wa miaka zaidi ya 60.
hiv huyu mtu amekua maskini ghafla ataisjije?!!
cku zinakuja .....
 
Tanzania bwana. Watu wameona wanaingiliwa kwenye ulaji wao tayari oporesheni tokomeza wameitokomeza !!!? Cheza na majangili wewe!!!.

Mimi nimeshangaa sana mkuu manning. Yaani nimewangalia jana wakati wanajadili..hakuna hata mbunge mmoja aliyejaribu kuonyesha ubaya wa ujangili na hali ilivyokuwa mbaya sasa hivi....wala kuonyesha kwamba ni kwa nini hii operation ni muhimu.

Mi nadhani kwenye.operation kama hii haiwezi kukosa majeruhi na kuisitisha pamoja na kiwalaumu watekelezaji kwa maaana ya JWTZ Polisi na askari wa wanyamapori ni kuwaondolea morale kabisa

Wabunge.wameshindwa kuona ni kwa nini ujangili uliokithiri utaathiri sana utalii.ambao unachangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa.

Suala la ujangili limeshakuwa systemic...wamekamatwa watu hapa lakini unasikia wanaachiwa au watu wanalobby waachiwe..huo.ni.udhaifu wa utekelezaji wa sheria na ingepaswa wahusika wote waadhibiwe vikali....

Suala la mifugo kuingi hifadhini ni kinyume cha sheria ya wanyamapori ..so ikikamatwa ndani inabidi mwenye nayo alipe faini nk...kuwaachia namna hii inaset precedent kwamba unaweza tu ukaswaga mifugo yako hifadhini kisha ikaachiwa kiroho safey. Kila siku watu wanahubiriwa wapunguze idadi ya mifugo lakini wapi....matokeo yake ndo kama hivi.

Kikubwa ninachoona hapa ni uchaguzi unakaribia na kura za wafugaji.ni muhimu sana...
 
Last edited by a moderator:
Unajua bwana pasco wakati mwingine huyu lukosi anakera sana anataka kuhamisha mwelekeo wa kinachojadiliwa kwa kuleta utani kwenye suala nyeti, kilichofanywa na yegella ni kataka kulionyesha jukwaa mtu anayetaka kupindisha mjadala ni mtu wa aina gani. Kwa hiyo huyu lukosi sio kila hoja uchangie wakati mwingine ni vema kuwa msomaji kama huna cha kuchangia badala ya kuchangia ujjnga na kuamshi hasira kwa wengine
Umetoa hoja ya msingi,kama mtu huna la kuchangia ni bora ukakaa kimya
 
kumbe Lukosi ndio mtu wa namna hiyo!!!! daaa, aiseee kumbe ndio maanaa!.
 
Mkuu Yegella, hata kama ni kweli, au si kweli, comment hii ni kinyume cha utu wa mtu, huu ni unyanyapaa ambao ni kosa against morality!. VVU ni janga la kitaifa, kuna wengi ama tunaishi na vvu ama wanaishi na vvu, kitendo cha kuandika tumdharau fulani kwa sababu ni muathirika wa vvu, ni kuwadhalilisha waathirika wote wa vvu!, tena usikute unaandika haya huku hujapima!.

Pamoja na utani na mizaha yote tunayotoleana humu jukwaani, tusivuke mipaka ya utu na ubinaadamu!.
This comment is not fair!.
Pasco.
Ni kweli kabisa kuwa tuheshimu utu wa binadamu na tusifanye mizaha ambayo haina tija.
Lakini pia Lukosi ajaribu kuangalia the way anavyo comment humu ndani ya jamvi,he is opening a lot of warfronts bila sababu!!
 
operesheni kimbunga yazoa mawaziri
• wabunge wataka pinda, nchimbi, kagasheki, mathayo wang'oke

na salehe mohamed, dodoma
tanzania daima


hatima ya mawaziri watano kuendelea na nyadhifa zao iko shakani baada ya wabunge kuwatuhumu kushindwa kuwajibika ipasavyo na kusababisha migogoro ya wafugaji na wakulima.
Kufuatia kadhia hiyo iliyojitokeza wakati wa kutekelezwa kwa operesheni kimbunga na operesheni tokomeza ujangili, bunge limeamua kuunda kamati teule kuchunguza migogoro ya wakulima na wafugaji ambayo imesababisha vifo, ukiukaji wa haki za binadamu na upotevu wa mali.

Wabunge wengi waliochangia hoja hiyo waliwataja wazi mawazi kadhaa akiwemo waziri mkuu mizengo pinda, wakitaka wawajibishwe kwa kuondolewa kwenye nyadhifa zao kutokana na kushindwa kuchukua hatua wakati operesheni hizo zikipoteza maisha ya watu na mifugo.
Mbali na pinda, wamo pia dk. Emmanuel nchimbi (mambo ya ndani), khamis kagasheki (maliasili na utalii), david mathayo david (mifugo na uvuvi) na shamsi vuai nahodha (ulinzi na jeshi la kujenga taifa).

Dalili mbaya kwa viongozi hao zilianza kuonekana jana asubuhi baada ya spika wa bunge, anne makinda, kutangaza kuwa amekubali hoja za wabunge wawili waliotaka shughuli za bunge ziahirishwe ili kujadili jambo la dharura.

Alisema mbunge wa sikonge, said nkumba (ccm) alitaka bunge lijadili kuhusu migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi, huku mbunge wa mwibara, kangi lugola (ccm), alitaka bunge lijadili vitendo vinavyofanywa na watendaji katika operesheni tokomeza ujangili.
Lugola alidai watendaji wamekuwa wakiwaua kwa risasi ng'ombe waliowakamata kwenye operesheni hiyo pamoja na kuwatesa wamiliki wasiotoa fedha zinazohitajika.

Kutokana na hoja hizo, makinda alitoa fursa kwa waziri wa maliasili na utalii, khamis kagasheki na waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi, david mathayo kuelezea operesheni tokomeza ujangili na migogoro kati ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.
Kagasheki ndiye aliyekuwa wa kwanza kueleza operesheni hiyo inaendelea. Alisema inalenga kutokomeza ujangili ulioshamiri hapa nchini kiasi cha kutishia sekta ya utalii na tembo.
Hata hivyo, kagasheki alisema kutokana na malalamiko ya watu mbalimbali juu ya mwenendo wa operesheni hiyo, serikali imeamua kuisitisha ili kufanya tathmini.

Waziri huyo pia alisema mifugo yote iliyokamatwa ndani ya hifadhi kabla na baada ya operesheni hiyo iachiliwe bila gharama yoyote na watu wenye ushahidi wa ng'ombe wao waliouawa kwa risasi wawasilishe vielelezo ili achukue hatua zaidi.
Mara baada ya kagasheki kutoa taarifa hiyo, waziri mathayo alitoa taarifa kuhusu migogoro kati ya wafugaji na wakulima. Aliwaomba radhi waliopata hasara ya kujeruhiwa, kupoteza mifugo au vifo katika operesheni hiyo.

wabunge wacharuka
mara baada ya mawaziri hao kumaliza kutoa taarifa zao, spika makinda alitoa fursa kwa wabunge kuchangia. Mbunge wa kilolo, peter msolla (ccm), alitoa hoja ya bunge liunde kamati teule kuchunguza migogoro ya wafugaji na watumiaji wengine wa ardhi.
Alifuata lugola, ambaye alisema anashangazwa na mawaziri nchimbi, nahodha, kagasheki na mathayo kuendelea kuongoza wizara wakati damu za wananchi waliofariki katika operesheni zinazohusisha wizara wanazoziongoza zinawakabili.

Mbunge wa busega, dk. Titus kamani (ccm), aliifananisha serikali na ugonjwa wa miguu na midomo kwenye mifugo, maarufu kama sotoka, ambao miaka ya nyuma ulikuwa ukiua ng'ombe wengi.
"hii serikali ya ajabu sana, yaani ukiwa na mifugo mingi ni kero kwao. Badala ya kuweka mazingira mazuri ya kukuza uchumi, wanaiua. Mimi naifananisha na sotoka," alisema.

mbunge wa maswa, magharibi, john shibuda (chadema), aliwataka wabunge wa ccm waache unafiki na wamuondoe waziri mkuu, pinda kwa kuwa hachukui hatua kila anapopelekewa matatizo.
"wewe waziri mkuu, taarifa za kiintelijensia hazikufikii? Je, husomi magazeti kujua kinachotokea kwenye maeneo mbalimbali na mbona huchukui hatua? Nyinyi watu wa ccm msileane," alisema.
Naye mbunge wa viti maalumu, pauline gekul (chadema), alimtaka rais jakaya kikwete awafukuze kazi mawaziri wake waliosababisha operesheni za kinyama zilizosababisha vifo vya binadamu, mifugo na unyanyasaji.

Mbunge wa muleba kaskazini, charles mwijage (ccm), alisema serikali inatia aibu kwa kukamata meno ya tembo, lakini inashindwa kuwakamata majangili waliohusika.
Mbunge wa viti maalumu, esther bulaya (ccm), aliwataka mawaziri waache porojo za kisiasa wanapoambiwa matatizo ya wananchi na wabunge.
"wabunge humu ndani tunaeleza matatizo ya wananchi, eti waziri anasema si mambo ya msingi…acheni porojo, fanyeni kazi, maana tuna ushahidi wa kile tunachokisema," alisema.


kamati teule
akihitimisha mjadala huo, makinda aliafiki wazo la kuundwa kwa kamati teule.
Hata hivyo kamati teule hizo kila zinapoundwa na ripoti yake kusomwa zimekuwa zikisababisha kuondoka madarakani kwa watendaji mbalimbali.
Februari 8, 2008, waziri mkuu, edward lowassa, alilazimika kujiuzulu baada ya kamati teule iliyoundwa na bunge kuchunguza zabuni iliyoipa ushindi wa kuzalisha umeme wa dharura kampuni ya richmond kumgusa.

Mwaka juzi, bunge liliunda kamati teule kuchunguza matumizi ya wizara ya nishati na madini, ambayo ilidaiwa kuchangisha sh milioni 50 kwa idara na taasisi zilizo chini ya wizara, ili kufanikisha upitishwaji wa bajeti, na ripoti yake ilimng'oa katibu wake, david jairo.

kosa kubwa ni kuingiza majeshi mengine katika mambo ambayo hawakusomea.
Polisi pamoja na udhaifu wao lakini angalau wana uelewa kiasi wa sheria lakini jwtz wapi na wapi.
Hili ndilo kosa ambalo hata mtwara limefanyika na madhara yake karibuni yatakuwa wazi.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
WASIFU WA LUKOSI 1.Huyu jamaa alikuwa polisi akafukuzwa sababu ya ajali katika msafara wa pm wakati ule John Malecela na kukimbilia Botwana kwa dada yake ambaye ni Nurse.2 2.Lukosi alifuatana na dadake nchini uk baada ya kupata kazi uk nayeye alipata nafasi ya kuambatana naye uk. 3.Lukosi alipata nafasi ya kujifanya mkimbizi na kuukana utanzania pamoja na porojo zake yeye uk anafahamika kama mkimbizi wa kisiasa na njaa. 4. Lukosi alipata kazi ya kuwa traffic warden kwa bahati mbaya alipata ajali ambayo ilimfanya adhurike kichwani alilazwa kwa muda mrefu na aliathirika na ajali ile kichwani.Kampuni aliyokuwa akiifanyia kazi ilimlipa malipo kutokana na ajali hiyo,na baada ya muda aliacha kazi na kuanza biashara. 5 Lukosi alianza biashara za kupeleka magari mabovu Tanzania na baiskeri za wizi kutokea maeneo ya barking&dagenham na baada ya muda alianza biashara nyingine ambazo wengi wanazijua. 6 Lukosi alijaribu kujiingiza kwenye siasa baada ya kukutana na mbunge Lema jijini London,na nia kubwa akifikiri atapata tender za kusafirisha mizigo na magari ya chadema.Alipewa nafasi kukaa hotelini kwa mzee ndesambulo jijini Dar kwa week moja free of charge. 7 Baada ya kukosa tender hiyo Lukosi alirudi ccm ambapo hajawahi kuwa mwanachama uk,na alianza kashfa nyingi kuhusu chadema na hii ni kutokana na waajiri wake wa biashara (sizisemi) kutoka Tanzania ambao ni wafadhiliwa na ccm kutokana biashara hizo.Ametumia muda mwingi mtandaoni ili wamkubali kuwa katoka chadema na anaichafua. 8. Tumdharau Lukosi kwa sababu ana ugonjwa wa pressure na inasemekana ni muathirika wa vvu si mwana siasa ila ni stress zinamsumbua..
Unataka kusema Lukosi alijilipua kama Mkongo, Msudan, au Mnyarwnda? Kuna haja ya kufuatilia taarifa zake hapa London ili Home affairs waweze kujua kuwa jamaa huyu ni mtanzania na si mkimbizi aliyetoka katika nchi ya vita ili asiendelee kupewa status ya ukimbizi wa uongo na kula pesa za walipa kodi wa Kiingreza.
 
Ukweli ni kuwa hizi operesheni zimegusa maslahi ya wakubwa; namely Katibu mkuu Kinana, Lukuvi, nk.
Tulisikia taarifa wabunge hapo kusini wanahusika na ujangili. Then tunajua Kinana ndiye kinara wa ujangili Tz, alafu tukasikia msaidizi wa Lukuvi kahusika. Tungetarajia nini katika hili.
Najua hili la operesheni kimbunga limeingizwa tu kutupoteza maboya but ukweli ni kwamba kinacholengwa hapa ni kuondoa hii operesheni ya kupinga ujangili.
Makinda amekubali hili suala lijadiliwe na kamati iundwe kwa sababu mbunge mwenzake wa Iringa, Lukuvi ameguswa. Najua hata kamati itakayoundwa itakuwa imeshaandaliwa tayari na taarifa yao wataandikiwa...
 
Pinda kawa waziri mkuu mwenye mikosi na misukosuko kulipo wote waliomtangulia
inaonekana ni kweli hicho kiatu hakimtoshi...
 
Back
Top Bottom