kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,428
- 7,216
Eeeh bana hao jamaa ni ruthless ukisikia jinsi walivyokua wanawafanyia wenyeji baada ya kupata vibali fake kwa kuhonga usingeliwaonea huruma. Halafu wana hila nyingi nadhani ndio maana nguvu inatumika. Bila hivyo huwezi kuwatoa hao. Pamoja na hivyo sio kama naunga mkono wale wasiokua wakorofi wafanyiwe vitendo vya ubabe au kuhujumiwa haki zao.Nyumba za wahamiaji (nachelea kutumia haram, binadamu hawezi kuwa haram) zimechmwa, mifugo inaibiwa na familia zinatenganishwa kule Kagera.
Kigoma na Geita kimyaaa! Ukweli ni jk hakuagiza hivyo. Alisema: MIFUGO IONDOLEWE HIFADHINI, NG'OMBE WALIOINGIZWA WARUDISHWE WALIKOTOKA, WAHAMIAJI WALIOPEWA VIBARI NA WATENDAJI WA VIJIJI WARUDISHWE, NA WANAOINGIA KIHOLELA WAFUATE UTARATIBU.
Hajase waliozaliwa hapa na wana mifugo yao waondoshwe haraka, hajasema wenye vibari halali vichanwe na watimuliwe, hajasema wana vijiji wavamie nyumba na kuzichoma eti ni za wahamiaji haram, na kula mifugo yao.
JK, inabidi aingilie kati manake anaonekana analipiza kisasi kwa Kagame, kumbe hakuwa na nia mbaya kiongozi wa watu.