ONYO: Ubungo Darajani kuna wezi balaa

ONYO: Ubungo Darajani kuna wezi balaa

Kuna mmoja alitaka kumwibia polisi mstaafu mmoja ile anataka kuiba tu simu akamdaka mkono alipewa kichwa kimoja tu kimya kimya nikaona anatema meno matatu.
 
Habari za siku Mingi ?

Leo nilikua pale ubungo darajani stand,maeneo haya ni maeneo yangu ya kujidai kabisa toka 2006 napajua ubungo vizuri na washenzi wote wa pale tena enzi za Hamidu mzawa.

Leo naomba nikujulishe wewe mtanzania unaetumia kituo kile ni kwamba kimejaa wasafiri wengi feki,kuna vijana kama thelathini wao hushinda pale kama wasafiri kumbe ni wezi tu,na huwa wana vibegi mgongoni kazi yao kubwa ni kuiba tu.

Kama wewe ni mtumiaji wa eneo hilo kuwa makini sana.Leo nilikaa pale Masaa matatu nikaona walivyo na network yao kubwa.

Kuweni makini.ukifika pale angalia vijana waliovaa mabegi mgongoni wanapokimbikia gari huwa hawapandi.

Yang hayo.

Zubedayo_mchuzi MZEE kutembea mpk chalinze.[/Quote
Kwa nini ukae masaa matatu?
 
Unakuta jamaa anakimbilia gari alaf akifika mlangoni anajifanya anahangaika kuingia ndani so wewe akili yako yote itakuwa kutafuta namna ya kupita uingie ndani uku unawaachia wengine wakupekue watakavyo
 
"ulikaa pale masaa 3"?

Uliwaona wezi wanavibegi mgongoni wanapokimbilia gari huwa hawapandi!!!

Hapa mimi napata mshangao, watu waliopita leo darajani wakienda nakurudi wakikuona umekaa kwa muda wa Masaa 3 watakufirikiaje?

Sasa wewe na wale waobeba vibegi mgongoni japo wanakimbilia gari na hawapandi ninani kati yenu atakuwa mshukiwa?
Acha hizo sasa unatetea wezi, mwenzio kakaa kituoni kwa ajili ya uchunguzi we unaleta ungese, au hujui lolote kichwani mwako
 
Ukishuka kweny gar toka mikoani usiku ni vyema kupakia boda kuliko kusogelea maeneo yale
 
Hakuna kitu huwa kinanishangaza kama swala la vibaka police wapo na mda wote Wanazunguka tu kwenye gar kaxi Yao kuvizia maroli tu nimekulia ubungo riveside naijuwa mipango yote ya pale ubungo
 
Mnajuwa kazi ya vile vibegi? Kazi yake ukiwa umekaa kwenye siti ukawa makini utaona wanaume wengi huweka pesa mfuko wa nyuma hivyo basi lile begi hujifanya kukuwekea pale matakoni na kujifanya kabanwa huku likiwakinga abiria wasione mkono wake unavyo kuchomolea pesa makonda wengi wanawafahamu waungwana huwafukuza wengine ni sehemu ya michongo hiyo kuweni makini mnapopanda DALADALA lilojaa kupita kiasi
Duu watu ma Expert





Mods naomba hii thread iwe sticky
 
Acha hizo sasa unatetea wezi, mwenzio kakaa kituoni kwa ajili ya uchunguzi we unaleta ungese, au hujui lolote kichwani mwako
Ahaaa matusi mipasho fahari yako "uchafu wa kinywa ndio tafsiri mtu alivyo"
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom