Jospina
JF-Expert Member
- Apr 19, 2013
- 2,421
- 1,395
Tuko watu tuna tabia ya kuchukua waume za watu na wake za watu! Na tunafikia mahali tunajivuna na kujipigapiga vifua kwamba! Hakuna mwanaume au mwanamke unayeshindwa kumpata ukimtaka!
Sababu zozote za kuchukua mke wa mtu au mume wa mtu hazikubaliki mbele za MUNGU! Kwanini unatumia uzuri wako, pesa zako, umaarufu wako kuchukua wake za watu na waume za watu? Na unajigamba kwamba hakuna mwanamke mwenye uwezo wa kukukataa!
Kama wewe unachukua wake za watu na waume wa watu juwa wewe ni mfu, huwezi kupona! Litakupata janga lolote la kukufutilia mbali katika uso wa dunia, ni laana! Usiseme ananijipendekeza mwenyewe, hiyo sababu haiwezi kuiponya nafsi yako.
Kama wewe unatembea na mke wa mtu au mume wa mtu, unatakiwa kuacha mara moja na kumrudia Mungu kwa toba nzito! Muache huyo mke wa mtu au mume wa mtu! Hata kama anakupenda sana! Muache!
Tulia! Mungu atakupa wa kwako! Kwani wanawake wameisha au wanaume wameisha? Wasiwasi wako tu! Na hata kama unaye mumeo au mkeo acha tamaa wewe; kaa na wa kwako, jivunie wa kwako! Jiamini.
#msgDelivered
Sababu zozote za kuchukua mke wa mtu au mume wa mtu hazikubaliki mbele za MUNGU! Kwanini unatumia uzuri wako, pesa zako, umaarufu wako kuchukua wake za watu na waume za watu? Na unajigamba kwamba hakuna mwanamke mwenye uwezo wa kukukataa!
Kama wewe unachukua wake za watu na waume wa watu juwa wewe ni mfu, huwezi kupona! Litakupata janga lolote la kukufutilia mbali katika uso wa dunia, ni laana! Usiseme ananijipendekeza mwenyewe, hiyo sababu haiwezi kuiponya nafsi yako.
Kama wewe unatembea na mke wa mtu au mume wa mtu, unatakiwa kuacha mara moja na kumrudia Mungu kwa toba nzito! Muache huyo mke wa mtu au mume wa mtu! Hata kama anakupenda sana! Muache!
Tulia! Mungu atakupa wa kwako! Kwani wanawake wameisha au wanaume wameisha? Wasiwasi wako tu! Na hata kama unaye mumeo au mkeo acha tamaa wewe; kaa na wa kwako, jivunie wa kwako! Jiamini.
#msgDelivered