Heinrich Himmler
Member
- May 20, 2013
- 71
- 151
Wiki iliyopita nilisafiri kwenda Songea na gari yangu aina ya noah kutokea DSM, nilivyokuwa narudi nikaona nisanye abiria wanichangie mafuta. Sasa nimetoka Songea mpaka Iringa bila matatizo yoyote na sikuona kama gari ina tatizo lolote. Nilipofika kwenye milima ya kitonga nikaanza kuteremka ghafla mbele yangu kukawa na roli linateremka taratibu, si nikaamua kuliovateki, katika kuliovateki lile roli nikawa nimeliacha gari langu limechanganya speed ili niliovateki roli. Hamadi namaliza kiliovateki kuna kona kali upande wangu mimi dereva, narudisha mguu kati kwenye breki hamna kitu yaani naipata kwa mbali sana, nikajaribi kulala nayo ikanishinda nikaenda kubamiza kwenye lile gema la mbele yangu head-on. Kioo cha mbele kikatuchanachana mimi na abiria aliekuwa aliekuwa mbele. Gari kwa mbele ikaharibika nyakanyaka mchuzi tu ukawa unamwagika chini umechanganyika maji ya rejeta, hydraulic na oil vikawa vinamwagika, Nilichofanya ni kuwarudishia abiria nauli zao na mimi kutafuta gari ya kuivuta kuja dar. Hapa nilipo nipo mwaisela nyuma ya key board.
USHAURI: Wengi hatuna kawaida ya kuangalia break pads za magari yetu kama hazijaisha. Ukiendesha gari hapa mjini inaweza isiwe ishu ila ukiamua kutoka nalo kwenda mikoani hebu jaribu kutazamabreak pads kama ni nzima. Gari ikiwa na break pads zilizolika sana inaweza ikawa inashika break ikiwa haina mzigo, ila ukiwa na mzigo au abiria halafu unateremka kwenye kilima kikali kama kitonga, hiyo ni time bomb.
USHAURI: Wengi hatuna kawaida ya kuangalia break pads za magari yetu kama hazijaisha. Ukiendesha gari hapa mjini inaweza isiwe ishu ila ukiamua kutoka nalo kwenda mikoani hebu jaribu kutazamabreak pads kama ni nzima. Gari ikiwa na break pads zilizolika sana inaweza ikawa inashika break ikiwa haina mzigo, ila ukiwa na mzigo au abiria halafu unateremka kwenye kilima kikali kama kitonga, hiyo ni time bomb.