Mimi siwezi kukaa hapa kuargue na mtu aliyefungia akili zake kwenye box. Ungesoma ukaelewa vizuri post yangu ungebadili namna yako ya kufikiri. NIT naifahamu kuliko unavyowaza wewe, ninajuwa ilikotoka kwa miaka 6 iliyopita na ninajuwa ilipo sasa. Kwanza ni halali yake kabisa kupewa pongezi Mkuu wa Chuo Prof. Mganilwa na timu yake kwa kazi kubwa waliyoifanya kuibadilisha NIT ya zamani kuifanya kuwa NIT nyingine ya sasa. Asiyeona mabadiliko hayo, huyo ni kipofu wa macho na akili na haijui NIT.
Wewe unayelalamika juu ya ada huna hata survey ya fee structure kwenye Public Institutes nyingine. Sasa kwa kuwa unapiga kelele tu bila kuwa na taarifa za kukusaidia, mimi nakusaidia fee structures za baadhi ya vyuo vya umma.
1. Centre for Foreign Relations = 1,5M
2. CBE kwa course ya ICT=1.6M
3. DMI kuna kozi zinalipiwa 1.54M & 1.59M
4. TIA Arusha 1.5M
5. IFM kwa course ya Computer Science=1.7M
6. Institute of Tax Administration (ITA)=1.95M
Sasa kwa akili muono wako wa haraka, wewe na mwanafunzi wa kozi ya ICT-CBE, DMI, IFM na ITA, nani alitakiwa kulalamika zaidi ya mwingine? Acha uvivu tafuta taarifa na ufanye analysis kabla kupiga piga kelele.
Mvivu mwingine humu asiyetambua wajibu wake nimeona akimshtumu mwalimu Daud, Daud. Ni kweli Daud hakumbatii ujinga, usiposoma anakula kichwa hatoi marks za bure yule kama mnavyopendelea. Mimi amenifundisha ICT, ujinga wa kupewa marks bila kufaulu mwenyewe, kwa Daud sahau. Na siyo Daud tu, bali waalimu wote wasioendekeza ujinga wana maadui kama nyinyi. Heko kwa Dr. Prosper Mgaya, Mkuu wa Taaluma, Tafiti na Ushauri- ameipa heshima taaluma ya NIT, vilaza wanaofikiri wanakuja kuchukua degree bila kusoma, degree siyo ya kuchukua ni ya kutafuta.
You NIT guys need to change your attitudes and position yourselves in a new versatile way of thinking.
Honestly Mimi nasoma NIT... Kwa miaka minne niliokaa pale Chuo kimebadilishwa Sana tena Sana Na mkuu wa Chuo.. Cjui kwa loan beneficiaries ILA kwa personal sponsored naona kina fundisha vizuri cjawahi bambikiwa carry or supplementary... Kiukweli ukileta urembo pale carry Na sup utazila Tu walimu wanajitahidi... People wana criticize hadi school of aviation wen hawasomi pale... For the past four years Chu kimebadilika Na binafsi nampongea Mganilwa.. Nimesoma shule za serikali hata huko poa maneno ya kusema vvibaya shule yalikuwepo... Vyuo tunachukua maarifa Na ustadi gamba bila kuwa creative in your profession is nothing... Cjui kwanini ila I am sure aliye post hii anasoma NIT... This is personal vendetta...
Nashkuru mkuu kwa kuja kutufahamisha ukweli kuhusu NIT, kwani uwongo ukisemwa sana huaminiwa na ili kuundoa uongo katika ubongo wa binadamu ni kuuzungumza ukweli wake, na hilo umelifanya shukrani sana sasa mimi nina haja ya kufahamu mambo mawili kutoka kwako, kwanza mlikuwa na mpango wa kuanza kufundisha mafunzo ya urubani naomba kufahamishwa mmefikia wapi katika hilo, na kama tayari ada yake ni kiasi gani? na la pili ni kuhusu shahada ya uhandisi ya matengenezo ya ndege kuhusu ada yake kwa mwaka ili niweze kufahamu kwa muda wa miaka minne itagharimu kiasi gani?, natumai majibu yako yatatusaidia wengi wenye haja ya kuja kujiunga na NIT, Shukrani Mr. Mwanga A.
Nashkuru sana Mr.Mwanga A, for that detailed explanation, may the God bless you!Ndg Norton 82, nakushukuru kwa kuelewa vema maelezo yangu na wale wote pia walioelewa kupitia ufafanuzi nilioutoa.
Kuhusu mafunzo ya urubani-tayari chuo kimeshapata ithibati. Lakini course hii ina masharti yake na taratibu za kufuata, kwa sasa wanakamilisha taratibu zilizobakia na Tanzania Civil Aviation Authority (TCAA), then wata-finalize na International Civil Aviation Organization (ICAO). Hopefully kama mambo yataenda kama yalivyopangwa mwaka huu mafunzo yataanza-Notice will be served to the public ili muombe hizo nafasi. Kuhusu ada yake, ni miongoni mwa mambo yanayoshughulikiwa kwa sasa, tusubiri kidogo.
Kuhusu Shahada ya Uhandisi wa ndege-Wanafunzi wako wanaendelea na masomo, wapo mwaka wa kwanza intake ya 2016/2017 na wa mwaka wa pili intake ya 2015/2016. Ada yao kwa sasa ni milion 10. Hata hivyo muda wowote inaweza ikafanyiwa review. Lakini kwa uelewa zaidi na ushauri zaidi ya hapa unaweza kufika NIT chuoni Mabibo Campus ukatembelea School of Aviation.
Nakukaribisheni, njoni mpate ujuzi muitumikie nchi yenu, actually nchi yetu.
Acha kutetea ujinga. SAUT, SJUT, SEKUCO, na takataka nyingine utalinganisha na vyuo nilivyo vitaja ?
St john's ya dodoma au tawi la buguruni????Waende chuo kizuri kama St.John's University,hawatajutia walicho jifunza baada ya kumaliza,na wanafunzi wake wanasoko kubwa.
Ndg yangu NJAMES 88, hatukusoma ili tuondoke na cheti tu, bali tulichukuwa maarifa ya darasani na uongozi pia. "Unaweza kuwahadaa watu wote kwa kitambo tu lakini huwezi kuwahadaa watu wote wakati wote". NIT mna Almanac inayoonyesha shughuli zote za kitaaluma na muda wake wa kufanyika. Na fedha za mikopo ya HESLB pia inalipwa kwa kufuata Almanac. Wewe na wenzako, mwezi huo wa sita hadi wa saba mlikuwa semister I na mmeshalipwa Quarters 2. Semister II yenu ilikuwa inaanza August halafu watu wachache bila shaka na wewe ukiwemo mnafanya rallies eti mlipwe Q3 na Q4 wakati mnajuwa kabisa na mmeeleweshwa na Uongozi na Board kuwa hayo malipo ya Q1 na Q3 kwa utaratibu wa Board unaotumika ktk vyuo vyote ni due kulipwa Semister II. Sasa wewe bado hujamaliza hata Semester I, nyinyi eti mnagoma kudai Q3 na Q4!. Yaani mlazimishe kuvunja sheria, halafu ukiadhibiwa useme umeonewa? Kama unadai ulishinikiza zikapatikana kama unavyotaka kuhadaa umma hapa, waambieni watu hapa je, hizo fedha za Q3 na Q4 ulizipata semister I au Semister II?. Jibu ni kwamba ulilipwa ulipoingia Semister II kwa sababu ndo muda zilikuwa due kulipwa.kutoka
Kwanini unapata Carry?
Haki nimesoma hii threat nmecheka sana. Inaonesha namna gani mtoa mada ana chuki na nna wasiwasi na yeye kafukuzwa chuo. Nenda vyuo vingi sasahv kitambulisho lazima. Hiyo michango umetozwa peke yako? Maana mwaka wa nne nasoma engineering mbona sijawah kutozwa chochote? Acha kuwadanganya watoto. Watakaopangwa hapo wawaulize waliomaliza hapo kama wamepata usumbufu kazini.
Huo ndoukweli mkuuSio Kweli Kama ingekuwa Kweli mleta mada asingefeli, kifupi anapersonal issue, ushauri wangu mleta mada apambane na hali yake tu, asigeneralize mambo.
Waende chuo kizuri kama St.John's University,hawatajutia walicho jifunza baada ya kumaliza,na wanafunzi wake wanasoko kubwa.
Usisahau na Institute kama IAA ni kuzuri sana.vyuo hivyo tajwahapo juu vina digree za kuiba na kununua exams. Na hasa degree za sketi. SAUT na St.JoHNS are the best universities in Tanzania.
St. John bannedWaende chuo kizuri kama St.John's University,hawatajutia walicho jifunza baada ya kumaliza,na wanafunzi wake wanasoko kubwa.
Nawashauri vijana wote mliomaliza kidato cha sita au Diploma , msikiombe chuo cha taifa cha usafilishaji yaani NIT cha hapa mabibo Dar es salaam kwani kwa atakayejichanganya kufanya hivyo atajuta maishani mwake mwote.
Matazizo ya NIT ni kama ifuatavyo:
1) Elimu hafifu kuliko kawaida inayosababishwa uongozi mbovu wa chuo,
Chuo kimejikita katika kukusanya mapato ya fedha kuliko kutoa Elimu sitahiki kwa wanafunzi.
2)kuwapa waalimu Uhuru uliopitiliza kuamua lolote juu ya wanafunzi eidha kutokuwafundisha syllabus yote katika course husika jambo linalosababisha elimu kuwa hafifu sana kwani wanafunzi hujikuta wanasoma miezi takribani mitatu na kumaliza semester bila ya kumaliza syllabus kwa baadhi ya course.
3) Baadhi ya walimu walio wengi kuwa Lugha isiyo na staha kwa wanafunzi. Jambo linalosababisha chuo kuongozwa kama shule ya msingi!
4) Kufukuza fukuza chuo wanafunzi wanaojitokeza kuomba mataizo hayo yasitishwe.
5) Kuwaibia wanafunzi fedha zao (50,000 Tsh) kwa kisingizio kuwa wanachangia Vyeti vya kumaliza Level 7 wakati hata hawajaanza kusoma course husika na wala hawajafikia Level 8 yaani Barchelar degree kwa kuwaambia kuwa kama huna hiyo fedha huwezi kusajiliwa kama mwanafunzi.
6) Kuwakata pesa za mikopo wanafunzi bila wao kujua kupitia benk mala baada ya pesa ya mkopo kuingizwa kwenye account za wanafunzi, mfano NIT COMMISSION FEE zaidi ya Tsh 3,580 hukatwa Kwa kila mwanafunzi anayepokea 510000 kama pesa ya kujikimu kwa kipindi cha siku 60 kupitia bank ya NMB ( kwa CRDB sijapata ushahidi) mchango ambao hukatwa kwa siri siri kwenye account za wanafunzi kila wanapopokea pesa zao bila wao kufahamu kuwa wanachangia Nini.
7) TATIZO SUGU, pesa ya kujikimu ( boom) kucheleweshwa mmno yaani hadi zaidi ya siku 45 baada ya wanafunzi kufika chuoni au pindi akiendelea na masomo, Jambo ambalo huleta adha kubwa kwa wanafunzi kwani hukosa pesa ya kulipia vyumba au hostel za kuishi na pesa ya kula hali ambayo huwafanya washindwe kufanya vizuri darasani.
8) Pesa ya field kupewa Siku chache kabla ya kumaliza field na hata baada ya kumaliza field kabisa ndipo upewe pesa ya field au kusubiri tena siku zaid ya 27 baada ya kumaliza field ndipo upewe pesa yako bila kupewa sababu za msingi ni kwa nini inakuwa hivyo.( ushahidi upo) WIZI MTUPU.
9)Walinzi wa chuo kuwasumbua wanafunzi getini pindi wakiingia chuoni kwa kuwa lazimisha wavae vitambulisho shingoni licha ya sehemu kubwa ya chuo kuwa wazi, na wahalifu wengi hutoka mtaani na kuingia chuoni kupitia sehemu za chuo zilizo wazi bila walinzi kuwakamata, na kukaa kwenye vichaka vidogo vidogo vya chuo na wengine wengi huvuta banki wakiwa maeneo hayo ndani ya Chuo na kusababisha adha kwa wanafunzi wanaosomea vimbwetani karibu na vichaka hivyo dhidi ya moshi unaovuka, jambo ambalo hutufanya wanafunzi tujihisi kuwa sisi ndiyo tunatiliwa shaka kama wahalifu kwa kushinikizwa kuvaa vitambulisho pindi tunapofika getini wakati wahalifu huingia chuoni hapa kupitia maeneo yalio wazi bila bugza yoyote kutoka kwa walinzi wa chuo.
10) kutozwa pesa Tsh. 40,000 kila mwanafunzi wa bachelar ya kulipia maabara za computer kwa ajili ya " practice " bila kuingia maabara hata Mara moja mwaka mzima wa masomo sanjali na kutozwa Tsh.20,000 ya vitambulisho vya chuo ambacho huisha mda wake Mara moja kila baada ya mwanafunzi kumaliza mtihani wa semester na kupelekea kutotambuliwa tena kama mwanafunzi awapo ndani au nje ya chuo. ( WIZI MTUPU)
11) Chuo kutoza fedha kubwa mno Tsh. 1500000 kama jumla na michango na karo kwa kila mwanafunzi wa course yoyote na kuacha mazingira ya chuo kuwa machafu licha ya kutoza kiasi hicho cha fedha hali ambayo hushusha hadhi ya mwanafunzi wa chuo kikuu.
12) kuwatoza wanafunzi Tsh.100,000 kama pesa ya kuwalipa ma_supervisor kipindi cha mafunzo wakati vyuo vingine vya serikari hawatozi fedha hiyo. ( WIZI MTUPU)
13) kulipia mitihani ya Cary kuanzia 118,500 hadi 206,000 Tsh hata kwa mwanafunzi mwenye Cary moja wakati vyuo vingine vya serikari havitozi kabisa kama DIT na UDSM na vingine vingine, na vingine vichache hutoza pesa hiyo kulingana na namna ya uzito wa somo husika kama vile MUST. ( WIZI MTUPU)
14) Matatizo mengine mengi kama kuwafanya wanafunzi wa chuo kama watoto wa shule ya msingi na mengine mazito zaidi ambayo sitaweza kuyasema kwa sababu za kiusalama.
Mwisho nawasihi vijana wanao tarajia kuomba vyuo vikuu wasithubutu kuomba chuo hiki hata kama course wanazotaka kusoma zinapatikana hapa tu, kwani kama kwenu uwezo wa kifedha siyo mzuri na unasoma kwa mkopo wa serikali, uwezo wa kuimaliza hata course uliochagua unaweza kuwa mgumu kutokana na matatizo ya mikopo yaliyopo hapa., na hata ukifanikiwa kuimaliza utakuwa shallow mno kutokana na mfumo wa chuo kujikita katika ukusanyaji wa mapato ( fedha kutoka kwa wanafunzi) na kujipa posho zisizokuwa za lazima kwa ka_ Kazi kadogo ambako hakahitaji posho, (mfano kazi ya kusainisha wanafunzi mikopo ambayo ni kazi ya loan officer akisaidiwa na wizara ya fedha katika serikari ya wanafunzi kitu ambacho baadhi ya watumishi hupewa hiyo kama kazi na kuandikiwa posho) bila kujali Ubora wa elimu wanayotoa kwa wanafunzi wao.
USIIPUUZE HII TAARIFA UTAJUTA KWANI WAHENGA WALISEMA, " ASIYESIKIA LA MKUU HUJUNJIKA GUU"Duh kumbe huu uzi unaendeleaa
Post sent using JamiiForums mobile app[/QUOTENawashauri vijana wote mliomaliza kidato cha sita au Diploma , msikiombe chuo cha taifa cha usafilishaji yaani NIT cha hapa mabibo Dar es salaam kwani kwa atakayejichanganya kufanya hivyo atajuta maishani mwake mwote.
Matazizo ya NIT ni kama ifuatavyo:
1) Elimu hafifu kuliko kawaida inayosababishwa uongozi mbovu wa chuo,
Chuo kimejikita katika kukusanya mapato ya fedha kuliko kutoa Elimu sitahiki kwa wanafunzi.
2)kuwapa waalimu Uhuru uliopitiliza kuamua lolote juu ya wanafunzi eidha kutokuwafundisha syllabus yote katika course husika jambo linalosababisha elimu kuwa hafifu sana kwani wanafunzi hujikuta wanasoma miezi takribani mitatu na kumaliza semester bila ya kumaliza syllabus kwa baadhi ya course.
3) Baadhi ya walimu walio wengi kuwa Lugha isiyo na staha kwa wanafunzi. Jambo linalosababisha chuo kuongozwa kama shule ya msingi!
4) Kufukuza fukuza chuo wanafunzi wanaojitokeza kuomba mataizo hayo yasitishwe.
5) Kuwaibia wanafunzi fedha zao (50,000 Tsh) kwa kisingizio kuwa wanachangia Vyeti vya kumaliza Level 7 wakati hata hawajaanza kusoma course husika na wala hawajafikia Level 8 yaani Barchelar degree kwa kuwaambia kuwa kama huna hiyo fedha huwezi kusajiliwa kama mwanafunzi.
6) Kuwakata pesa za mikopo wanafunzi bila wao kujua kupitia benk mala baada ya pesa ya mkopo kuingizwa kwenye account za wanafunzi, mfano NIT COMMISSION FEE zaidi ya Tsh 3,580 hukatwa Kwa kila mwanafunzi anayepokea 510000 kama pesa ya kujikimu kwa kipindi cha siku 60 kupitia bank ya NMB ( kwa CRDB sijapata ushahidi) mchango ambao hukatwa kwa siri siri kwenye account za wanafunzi kila wanapopokea pesa zao bila wao kufahamu kuwa wanachangia Nini.
7) TATIZO SUGU, pesa ya kujikimu ( boom) kucheleweshwa mmno yaani hadi zaidi ya siku 45 baada ya wanafunzi kufika chuoni au pindi akiendelea na masomo, Jambo ambalo huleta adha kubwa kwa wanafunzi kwani hukosa pesa ya kulipia vyumba au hostel za kuishi na pesa ya kula hali ambayo huwafanya washindwe kufanya vizuri darasani.
8) Pesa ya field kupewa Siku chache kabla ya kumaliza field na hata baada ya kumaliza field kabisa ndipo upewe pesa ya field au kusubiri tena siku zaid ya 27 baada ya kumaliza field ndipo upewe pesa yako bila kupewa sababu za msingi ni kwa nini inakuwa hivyo.( ushahidi upo) WIZI MTUPU.
9)Walinzi wa chuo kuwasumbua wanafunzi getini pindi wakiingia chuoni kwa kuwa lazimisha wavae vitambulisho shingoni licha ya sehemu kubwa ya chuo kuwa wazi, na wahalifu wengi hutoka mtaani na kuingia chuoni kupitia sehemu za chuo zilizo wazi bila walinzi kuwakamata, na kukaa kwenye vichaka vidogo vidogo vya chuo na wengine wengi huvuta banki wakiwa maeneo hayo ndani ya Chuo na kusababisha adha kwa wanafunzi wanaosomea vimbwetani karibu na vichaka hivyo dhidi ya moshi unaovuka, jambo ambalo hutufanya wanafunzi tujihisi kuwa sisi ndiyo tunatiliwa shaka kama wahalifu kwa kushinikizwa kuvaa vitambulisho pindi tunapofika getini wakati wahalifu huingia chuoni hapa kupitia maeneo yalio wazi bila bugza yoyote kutoka kwa walinzi wa chuo.
10) kutozwa pesa Tsh. 40,000 kila mwanafunzi wa bachelar ya kulipia maabara za computer kwa ajili ya " practice " bila kuingia maabara hata Mara moja mwaka mzima wa masomo sanjali na kutozwa Tsh.20,000 ya vitambulisho vya chuo ambacho huisha mda wake Mara moja kila baada ya mwanafunzi kumaliza mtihani wa semester na kupelekea kutotambuliwa tena kama mwanafunzi awapo ndani au nje ya chuo. ( WIZI MTUPU)
11) Chuo kutoza fedha kubwa mno Tsh. 1500000 kama jumla na michango na karo kwa kila mwanafunzi wa course yoyote na kuacha mazingira ya chuo kuwa machafu licha ya kutoza kiasi hicho cha fedha hali ambayo hushusha hadhi ya mwanafunzi wa chuo kikuu.
12) kuwatoza wanafunzi Tsh.100,000 kama pesa ya kuwalipa ma_supervisor kipindi cha mafunzo wakati vyuo vingine vya serikari hawatozi fedha hiyo. ( WIZI MTUPU)
13) kulipia mitihani ya Cary kuanzia 118,500 hadi 206,000 Tsh hata kwa mwanafunzi mwenye Cary moja wakati vyuo vingine vya serikari havitozi kabisa kama DIT na UDSM na vingine vingine, na vingine vichache hutoza pesa hiyo kulingana na namna ya uzito wa somo husika kama vile MUST. ( WIZI MTUPU)
14) Matatizo mengine mengi kama kuwafanya wanafunzi wa chuo kama watoto wa shule ya msingi na mengine mazito zaidi ambayo sitaweza kuyasema kwa sababu za kiusalama.
Mwisho nawasihi vijana wanao tarajia kuomba vyuo vikuu wasithubutu kuomba chuo hiki hata kama course wanazotaka kusoma zinapatikana hapa tu, kwani kama kwenu uwezo wa kifedha siyo mzuri na unasoma kwa mkopo wa serikali, uwezo wa kuimaliza hata course uliochagua unaweza kuwa mgumu kutokana na matatizo ya mikopo yaliyopo hapa., na hata ukifanikiwa kuimaliza utakuwa shallow mno kutokana na mfumo wa chuo kujikita katika ukusanyaji wa mapato ( fedha kutoka kwa wanafunzi) na kujipa posho zisizokuwa za lazima kwa ka_ Kazi kadogo ambako hakahitaji posho, (mfano kazi ya kusainisha wanafunzi mikopo ambayo ni kazi ya loan officer akisaidiwa na wizara ya fedha katika serikari ya wanafunzi kitu ambacho baadhi ya watumishi hupewa hiyo kama kazi na kuandikiwa posho) bila kujali Ubora wa elimu wanayotoa kwa wanafunzi wao.
USIIPUUZE HII TAARIFA UTAJUTA KWANI WAHENGA WALISEMA, " ASIYESIKIA LA MKUU HUJUNJIKA GUU"
Post sent using JamiiForums mobile app