Onyo: Dr. Magufuli asizomewe tena

Onyo: Dr. Magufuli asizomewe tena

Kura asipewe na azomewe tu,nami nasema mzomeeni tu kwa sababu hakuna namna nyingine"(Pinda voice)
 
Onyo wape ccm waache kusumbua wananch kipindi cha uchaguzi
 
Tatizo lakee anapenda sana mikutano isiyo rasmi, haya mambo yake ya kusimama barabaran na kusema watu ndo wamemsimamisha aache... .. .
 
CCM siasa zetu za kistaarabu. UKAWA wanaendeshwa kwa viroba! Katika hali kama hiyo ni lazima watafanya hizo tabia za kuzomea.

Aidha, UKAWA waelewe kuwa, CCM ina wanachama na wapenzi wengi pia, hivi na sisi tukiamua kuanza hiyo tabia ya zomea zomea, mgombea wao Lowassa atapona kweli?

Rai yangu ni kwamba vijana waache kukubali kutumiwa na wanasiasa kwa kupewa viroba ili kukidhi matakwa yao ya kudhalilisha wagombea. Hii tabia sio nzuri na haikubaliki.
2157554521065238871
 
napenda sana kuwashukuru wazazi wangu
kipindi kile wananikazania kuhusu elimu sikuwa ninaaelewa umuhimu wake
leo ndio ninaelewa kuwa shule ni kila kitu

wanaozomea ni mafala na malofa ... huwezi kuwa ukawa na akili nzuri na mwenye elimu yako ukakaa barabarani ukazomea unless hujaelimika ila tu umekaa tu muda mrefu darasani.....
Kwa hiyo darasani ulusomea matusi
 
Ile ndo mitaa ya kuanza nayo ukiingia, viroba vya asubuhi vile, mitaa ya wanadarisalama huwa hawazomei wao wanangoja kukukata tu, hiyo itakuwa moshi ndogo ubungo
 
CCM siasa zetu za kistaarabu. UKAWA wanaendeshwa kwa viroba! Katika hali kama hiyo ni lazima watafanya hizo tabia za kuzomea.

Aidha, UKAWA waelewe kuwa, CCM ina wanachama na wapenzi wengi pia, hivi na sisi tukiamua kuanza hiyo tabia ya zomea zomea, mgombea wao Lowassa atapona kweli?

Rai yangu ni kwamba vijana waache kukubali kutumiwa na wanasiasa kwa kupewa viroba ili kukidhi matakwa yao ya kudhalilisha wagombea. Hii tabia sio nzuri na haikubaliki.
Kistaarabu na matusi yote hayo tunayoyasikia kila siku? Labda utueleze kama ustaarabu unaosema sio tunaoufahamu wengine.
 
Na mwanza Nyegezi stand kwenye mkutano wa wenje alizomewa.alikuwa anatoka sengerema
afadhali mkuu ulikuwepo, maana nilichangia hili la Magufuli kuzomewa Mwanza kuna jamaa linajiita jingalao likawa linanibishia! Tena mkuu alizomewa kuanzia Buhongwa, Mkolani, Nyegezi stand na Mkuyuni!
 
Azomewe tu maana hamna namna!! Ccm imechokwa si yeye...
 
Kama una busara ungewashauri kwanza kina nape, lusinde na mwigulu na wengine waache kumtukana lowassa kwenye majukwaa ya kisiasa ningekuona wamaana. Magufuli kuzomewa ni sawa kabisa maana hao niliowataja wanamtukana lowassa na magufuli akiwemo yy anakenua tu kwahiyo hayo ndo malipo yake.
 
Mzee naona umejaa upepo.

Lowassa ni kama maji: usipoyakoga utayanywa, usipoyapikia ugali utapikia mihogo.
 
Zomeeni tuu, tena sana maana baada ya tarehe 25 October,mtakuwa msibani kuomboleza kushindwa,WAKIWA NYIE!
 
Tumechoshwa na vitendo vya kuzomewa kwa mgombea wetu. Kuanzia kule Mbeya na hata hapa Dar es Salaam,Dr. Magufuli amekuwa akizomewa na kuoneshwa wazi kuwa hatakiwi. Yeye hujikaza kisabuni tu. Hutetemeka lakini huimarika.
Amewakosea nini hadi mumzomee? Wana-Dar es Salaam hamna tabia hiyo. Mmekuwa watiifu kwa CCM kwa muda wote. Mmekuwa hata wavumilivu kuitwa wala-miguu ya kuku. Kiwewapata nini? Nani kawaondoa utii kwa CCM?

Mkimzomea tena Dr. Magufuli,nasi tutamzomea wenu hata kwa kuigiza kwenye giza. Mnapaswa kumshangilia Dr. Magufuli na kumpa kura zenu. Msimzomee na kumnyima kura tafadhari!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Mkuu umeuliza maswali muhimu sana na japo ndipo pa kuanzia. Nini kimeondoa utiifu kwa CCM? Hilo ndilo tatizo halisi wala si kuzomea. Kuzomea ni dalili tu ya tatizo ulilouliza

Pili, kuzomea kuna ukakasi gani zaidi ya matusi? Mbona alikuwepo wakati utenzi wa matusi ukisomwa?

Tatu, kuzomea sioni tatizo, tatizo ni kama kuna mtu analeta vurugu. Hata jana Rais wa China alizomewa kule UK lakini hakuna aliyerusha mawe au ngumi, inakubalika

Nne, Magufuli pia ana sehemu yake. Ukiji behave kama mtu wa kijiweni, watu wa kijiweni wata ku treat kama mwenzao. Sasa anapopiga push ups majukwaani badala ya kueleza sera tayari anakaribisha watu wa vijiweni. Hapo ndipo wanakuja na mizigo yao ikiwemo hiyo ya kukosa uvumilivu. Si mwenzao? Wanamshangilia akipiga push ups, kumzomea ni opposite ya hilo, akubali kuwa naye ni sehemu ya tatizo
 
Sasa mgombea anapopiga push-up,badala ya kutangaza sera, wananchi tufanyeje? Mnadhani sisi ni mbumbumbu kiasi hicho? Rais wa Kuwait ni Sadam, reli zitajengwa kwa kiwango cha lami, sisi ni malofa, wanaume wabebe mimba,kweli? Tunyamaze? Tumelogwa? Mgombea akiongea kistaarabu nasi tutakuwa wastaarabu...angalia hadhira kabla ya hotuba,,,, jiongeze...
 
Kuzomewa si kosa bali ni hisia kuwa hukubaliki n hatukutaki
 
Back
Top Bottom