KUHUSU 3D
Picha kwenye screen ya kawaida inaonekana flat, kwa vipimo viwili "2 dimensions", "2d". Picha ya 3d, mbali ya kuonekana kuwa na upana na urefu, inaonekana pia kuwa na kina, na ndio "dimension" au kipimo cha tatu. Mwonekano huo wa kina unaifanya picha ya 3d kuonekana kama inaendelea kuelekea ndani ya screen, na hivyo kukufanya uhisi unaangalia vitu halisi kama kwa kupitia dirisha. Wakati mwingine vitu vingine vinaonekana kama vipo nje ya screen.
PICHA YA 3D INA NINI
Kwa maelezo mafupi kabisa, picha hizo zina taswira mbili zinazo tofautiana kidogo, moja kwa kila jicho. Wazungu wamesema "stereoscopic". Unapotazama picha ya 3d unaona kama vile unatazama taswira moja, lakini kimsingi unatazama taswira mbili tofauti. Taswira inayoonekana na jicho la kushoto haionekani na jicho la kulia, na taswira inayoonekana na jicho la kulia haionekani na jicho la kushoto. Taswira hizo mbili zinachambuliwa kwenye ubongo na kukufanya uone taswira moja yenye kina.
MBINU MBALIMBALI
Ni vigumu kutofautisha taswira kwenye screen moja kwa kila jicho. Leo unapozungumzia 3d unaskia habari za video ya pekee, tv channel ya pekee, screen ya pekee, miwani ya pekee nk. Hata hivyo mbinu mbalimbali zimetumika nyakati tofautitofauti kulingana na maendeleo ya teknolojia ya wakati husika.
Mbinu ya kwanza wazungu waliita "Anaglyph". Hapo walicheza na tofauti ya rangi. Mara nyingi picha pamoja na kuwa na rangi nyingine, ilikua na rangi nyekundu na buluu kama picha hii.http://data:image/jpeg;base64,
Na miwani iliyotumika ilikua na vioo vyenye rangi hizo mbili kama hii.
Jicho lenye kioo rangi nyekundu lilishindwa sehemu za bluu, na lenye kioo cha bluu likawa kinyume chake na hivo taswira mbili zikawa zimetenganishwa. Tatizo ni kwamba rangi hizo zisingeweza kuonekana tena kwenye picha na kuifanya picha hiyo kuwa na mapungufu kidogo, lakini lengo la 3d lilifikiwa.
Mbinu ya pili ilijulikana kama "Polarized". Hapa wazungu waligundua kuwa mionzi ya mwanga inaweza kuchujwa na kupewa mwelekeo mmoja. Wa wima, au wa mlalo, wa mzunguko wa saa au kinyume cha saa kwa kutumia vioo vya pekee vilivyo julikana kama "polarized glasses". Hapo projector mbili zenye vichujio tofauti vya mwanga zilirusha taswira mbili kwenye ubao mmoja. Mwanga huo ulichujwa baadae na miwani ya pekee aliyovaa mtazamaji yenye vichujio vya mwanga vilivyo wezesha kutofautisha taswira ya kila projector kwa kila jicho. Kwa mfano hapa jicho la kushoto liliona taswira ya projector ya kushoto na jicho la kulia liliona taswira ya projector ya kulia.
Video za namna hii zinatazamwa hadi leo kwenye kumbi za filamu za pekee, zilizo tengenezwa kwa njia hiyo. Hapa rangi zote zinaonekana na picha ni za kiwango kizuri sana.
Mbinu ya tatu inaitwa active shutter. Hii ni ya kisasa. Miwani yake inauzwa ghali, pengine inaanzia laki na kuendlea wakati miwani ya "polarizing" inaweza kuuzwa hadi elf tano. Miwani hiyo ya active shutter inakua na betri, na inafanya kazi kwa kufungua jicho moja na kufunga jingine kwa kupokezana kwa haraka sana kiasi kwamba aliyevaa hawezi kutambua. Hufanya hivyo kwa kupokea maelekezo kwa njia ya infrared kutoka kwenye screen ambayo nayo hubadilisha picha kwa kila jicho kwa haraka hiyo hiyo. Na hivyo hifikia lengo la taswira mbili, kila taswira kwa kila jicho.
Screen zinazotumika hapa ni za kisasa, zile zenye majina kama akina Samsung 3d na wazee wengine wenye majina. Hivo usinunue miwani ya plarized ukitaka unataka kuangali 3d kwenye madude hayo.
Rangi zinakua nzuri sana, ila ukiangalia muda mrefu utahisi kichwa kinauma kidogo.
Leo utaskia pia watu wanaangalia picha za 3d kwa kutumia maboksi ya Virtual Reality, "VR"
na Google cardboard vr.
Lakini kimsingi ndani pale picha inakua imegawanywa kwa kila jicho, na kuleta hisia ya kina, pamoja na upana na urefu na hivyo 3d.
Nimalizie hapa kwanza. Elewa kwanza hii nitakuletea maelezo jinsi ya kuchakachua 3d kwenye screen ya computer yako.
Picha kwenye screen ya kawaida inaonekana flat, kwa vipimo viwili "2 dimensions", "2d". Picha ya 3d, mbali ya kuonekana kuwa na upana na urefu, inaonekana pia kuwa na kina, na ndio "dimension" au kipimo cha tatu. Mwonekano huo wa kina unaifanya picha ya 3d kuonekana kama inaendelea kuelekea ndani ya screen, na hivyo kukufanya uhisi unaangalia vitu halisi kama kwa kupitia dirisha. Wakati mwingine vitu vingine vinaonekana kama vipo nje ya screen.
PICHA YA 3D INA NINI
Kwa maelezo mafupi kabisa, picha hizo zina taswira mbili zinazo tofautiana kidogo, moja kwa kila jicho. Wazungu wamesema "stereoscopic". Unapotazama picha ya 3d unaona kama vile unatazama taswira moja, lakini kimsingi unatazama taswira mbili tofauti. Taswira inayoonekana na jicho la kushoto haionekani na jicho la kulia, na taswira inayoonekana na jicho la kulia haionekani na jicho la kushoto. Taswira hizo mbili zinachambuliwa kwenye ubongo na kukufanya uone taswira moja yenye kina.
MBINU MBALIMBALI
Ni vigumu kutofautisha taswira kwenye screen moja kwa kila jicho. Leo unapozungumzia 3d unaskia habari za video ya pekee, tv channel ya pekee, screen ya pekee, miwani ya pekee nk. Hata hivyo mbinu mbalimbali zimetumika nyakati tofautitofauti kulingana na maendeleo ya teknolojia ya wakati husika.
Mbinu ya kwanza wazungu waliita "Anaglyph". Hapo walicheza na tofauti ya rangi. Mara nyingi picha pamoja na kuwa na rangi nyingine, ilikua na rangi nyekundu na buluu kama picha hii.http://data:image/jpeg;base64,
Na miwani iliyotumika ilikua na vioo vyenye rangi hizo mbili kama hii.
Mbinu ya pili ilijulikana kama "Polarized". Hapa wazungu waligundua kuwa mionzi ya mwanga inaweza kuchujwa na kupewa mwelekeo mmoja. Wa wima, au wa mlalo, wa mzunguko wa saa au kinyume cha saa kwa kutumia vioo vya pekee vilivyo julikana kama "polarized glasses". Hapo projector mbili zenye vichujio tofauti vya mwanga zilirusha taswira mbili kwenye ubao mmoja. Mwanga huo ulichujwa baadae na miwani ya pekee aliyovaa mtazamaji yenye vichujio vya mwanga vilivyo wezesha kutofautisha taswira ya kila projector kwa kila jicho. Kwa mfano hapa jicho la kushoto liliona taswira ya projector ya kushoto na jicho la kulia liliona taswira ya projector ya kulia.
Video za namna hii zinatazamwa hadi leo kwenye kumbi za filamu za pekee, zilizo tengenezwa kwa njia hiyo. Hapa rangi zote zinaonekana na picha ni za kiwango kizuri sana.
Mbinu ya tatu inaitwa active shutter. Hii ni ya kisasa. Miwani yake inauzwa ghali, pengine inaanzia laki na kuendlea wakati miwani ya "polarizing" inaweza kuuzwa hadi elf tano. Miwani hiyo ya active shutter inakua na betri, na inafanya kazi kwa kufungua jicho moja na kufunga jingine kwa kupokezana kwa haraka sana kiasi kwamba aliyevaa hawezi kutambua. Hufanya hivyo kwa kupokea maelekezo kwa njia ya infrared kutoka kwenye screen ambayo nayo hubadilisha picha kwa kila jicho kwa haraka hiyo hiyo. Na hivyo hifikia lengo la taswira mbili, kila taswira kwa kila jicho.
Rangi zinakua nzuri sana, ila ukiangalia muda mrefu utahisi kichwa kinauma kidogo.
Leo utaskia pia watu wanaangalia picha za 3d kwa kutumia maboksi ya Virtual Reality, "VR"
na Google cardboard vr.
Lakini kimsingi ndani pale picha inakua imegawanywa kwa kila jicho, na kuleta hisia ya kina, pamoja na upana na urefu na hivyo 3d.
Nimalizie hapa kwanza. Elewa kwanza hii nitakuletea maelezo jinsi ya kuchakachua 3d kwenye screen ya computer yako.