Ongezeko la Magari yenye vimulimuli, Serikali imeamua kuacha ‘uhuni’ kuendelea?

Ex Spy

JF-Expert Member
Jan 15, 2007
213
1,726
Hivi, tuna serikali ambayo ni responsive kwa wananchi kweli? Mbona dharau kwa wananchi zimezidi kiasi hiki? Ni uvunjifu wa Sheria ya Usalama Barabarani (2002), kifungu cha 19 B (1) na (2) na kifungu cha 54 (1), (2), (3), (4) na (5).

1) Nani ameruhusu watu hawa kujiwekea ving’ora au vimulimuli kihololela? Ilifuatwa sheria?

2) Tunajenga Taifa la aina gani kiasi kwa sasa unakutana hadi na IST ina vimulimuli?

Nilishangaa kukutana na DC aliyetemwa akiwa na gari la vimulimuli; nikajiuliza - kwani huyu bwana mdogo ni nani sasa?

Hayati Magufuli pamoja na udhaifu wake alikemea hili (angalau); sasa ‘wahuni’ wamerejea tena kazini na wanafanya hivi bila kukemewa wala Sheria kuchukua mkondo kwao.

Tujikumbushe:

a) Agosti 2019 - Jeshi la Polisi Latoa katazo Kwa Madereva Nchini

b) Julai 2020 - Polisi waagizwa kuwakamata wanaofunga ving’ora na vimulimuli kwenye magari

c) Hatua zikachukuliwa Dodoma: Polisi wanayashikilia magari 25 kukiuka amri ya IGP kwa kuyafunga magari yao ving’ora na taa kali

Sasa kwanini sasa imekuwa rahisi? Wanamwona Rais Samia kuwa dhaifu? IGP ni dhaifu kiasi hicho?
 
sisi tunapambana na M23 kwa sasa! na tunapambana na wahuni magaidi msumbiji! ni.muhimu sana kulinda viongoz wetu! tatizo watu hamuoni kwa.jicho.la tatu! mavimulimuli yakiwa mengo ndio safi kupotezea maboya! mkilazmisha yale ya kwenye utaratibu ni rahisi sana kuspot viongoz na kuwaua
 
sisi tunapambana na M23 kwa sasa! na tunapambana na wahuni magaidi msumbiji! ni.muhimu sana kulinda viongoz wetu! tatizo watu hamuoni kwa.jicho.la tatu! mavimulimuli yakiwa mengo ndio safi kupotezea maboya! mkilazmisha yale ya kwenye utaratibu ni rahisi sana kuspot viongoz na kuwaua
Sasa hao ndio hawatauawa?
 
Hivi, tuna serikali ambayo ni responsive kwa wananchi kweli? Mbona dharau kwa wananchi zimezidi kiasi hiki? Ni uvunjifu wa Sheria ya Usalama Barabarani (2002), kifungu cha 19 B (1) na (2) na kifungu cha 54 (1), (2), (3), (4) na (5).
Mpaka passo siku hizi wanafunga huvi vidude, ukutane na hii gari usiku sasa
 
Hoja nzuri ila kwa wana JF makini, tusi dilute mada muhimu kama hizi ambazo ni muhimu, thanks mtoa hoja kwa kuliongelea hili, blue lights ni kwa President, Vice President, PM tu wengine kama wana haraka lazima wapange muda vizuri.

Na mbaya nyingine ni matumizi ya ovyo ya blue lights, rangi hii ni ya police tu, sio mafuso, bajaji, au bodaboda na orange colour ni kwa magari ya uokozi tu, ni craze now middle of nowhere usiku unaona blue lights unapunguza mwendo na kujua ni tukio la kipolisi pale,unapokaribia ni fuso lililobeba ulanzi maana nalo limefungwa blue lights!

Mwisho drivers hasa wa magari madogo ,ful lights wakati wa night driving zina sheria yake
 
Nchi yetu bila serikali imara za mikoa, wilaya na Halmashauri au majimbo kabisa itakuwa inapiga hatua moja kwenda mbele kwenye jambo moja kisha inapiga nyingine mbili kurudi nyuma.
 
Tukubaliane jambo moja, kuna makosa ya kuonya na kuna yale ya kupiga faini.Kwa muda mrefu ni kama mindset za wenzetu wanaosimamia usalama barabarani imehamia kwenye kupiga faini makosa mbalimbali, hii imefanya kutokuona umuhimu wa kukumbusha na kuelekeza na kukataza mambo mbalimbali ambayo ni kinyume na sheria zetu barabarani.


Unapowakuta njiani akili ime focus kupiga faini na wamejisahau kwenye role yao.

Kwa upande wetu watumiaji wa vyombo vya moto, kuna kundi kubwa la madreva ambao tunajifanyia tu mambo yetu, kama isipotokea kuonywa wala hatujali si ajabu kuona bulb ya capacity ya kuwekwa kwenye Lorry inafungwa kwenye gari dogo la route za mjini bila kuzingatia athari zake.
 
Jana niliona video ya RTO wa Manyara akiwa anazungumzia haya mambo, yule dada yuko vizuri sana, anazijua sheria za usalama barabarani na anazifuata.

Alisema wazi kabisa, dereva hata akiwa wa kiongozi wa serikali, kama asipofuata sheria za usalama barabarani anangoa taa ya kin'gora anaondoka nayo, hawezi kuhangaika na bosi anayeendeshwa, yeye anahangaika na dereva aliyesomea hiyo kazi.
 
kama wewe ni dereva DSM, hasa ukiwa unaendesha usiki na sanasana katika foleni. jiandae kuwa kipofu. Morogoro highway DSM
 

Attachments

  • IMG_20230311_213524_734.jpg
    IMG_20230311_213524_734.jpg
    317 KB · Views: 10
Jana niliona video ya RTO wa Manyara akiwa anazungumzia haya mambo, yule dada yuko vizuri sana, anazijua sheria za usalama barabarani na anazifuata.

Alisema wazi kabisa, dereva hata akiwa wa kiongozi wa serikali, kama asipofuata sheria za usalama barabarani anangoa taa ya kin'gora anaondoka nayo, hawezi kuhangaika na bosi anayeendeshwa, yeye anahangaika na dereva aliyesomea hiyo kazi.
Yule RTO anaongea tu kufurahisha GENGE...

Aende Mikoa hii miwili DODOMA na DSM akang'oe hovyo hizo Taa kama hawajamdeal
 
Hivi, tuna serikali ambayo ni responsive kwa wananchi kweli? Mbona dharau kwa wananchi zimezidi kiasi hiki? Ni uvunjifu wa Sheria ya Usalama Barabarani (2002), kifungu cha 19 B (1) na (2) na kifungu cha 54 (1), (2), (3), (4) na (5).

1) Nani ameruhusu watu hawa kujiwekea ving’ora au vimulimuli kihololela? Ilifuatwa sheria?

2) Tunajenga Taifa la aina gani kiasi kwa sasa unakutana hadi na IST ina vimulimuli?

Nilishangaa kukutana na DC aliyetemwa akiwa na gari la vimulimuli; nikajiuliza - kwani huyu bwana mdogo ni nani sasa?

Hayati Magufuli pamoja na udhaifu wake alikemea hili (angalau); sasa ‘wahuni’ wamerejea tena kazini na wanafanya hivi bila kukemewa wala Sheria kuchukua mkondo kwao.

Tujikumbushe:

a) Agosti 2019 - Jeshi la Polisi Latoa katazo Kwa Madereva Nchini

b) Julai 2020 - Polisi waagizwa kuwakamata wanaofunga ving’ora na vimulimuli kwenye magari

c) Hatua zikachukuliwa Dodoma: Polisi wanayashikilia magari 25 kukiuka amri ya IGP kwa kuyafunga magari yao ving’ora na taa kali

Sasa kwanini sasa imekuwa rahisi? Wanamwona Rais Samia kuwa dhaifu? IGP ni dhaifu kiasi hicho?
Sasa hivi kila mtu anataka ukubwa, na ktambulika barabarani kuwa ana madaraka.
 
Back
Top Bottom