Ondoa utata, weka 10,001 katika maandishi

Ondoa utata, weka 10,001 katika maandishi

Kalamu Nzito

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2015
Posts
376
Reaction score
850
10,001
Naomba mnisaidie kuweka hii namba katika maandishi(kwa kiswahili)
 
Nakumbuka darasa la pili: Makumi elfu na moja
 
Elfu kumi,na moja.Unapotamka unatakiwa uweke shaddah au pumziko dogo unapotamka KUMI. Ila kwenye uandishi baada ya neno KUMI weka alama ya kituo kidogo(comma)
 
Ni kumi elfu na moja,kwa sababu tunahesabu tarakimu tatu kutoka kulia kuja kushoto na kuweka alama ya kimkato yaani(,)kinacho tamkwa elfu baada ya kusoma namba ya mwanzo kabla ya kimkato hicho cha elfu,kwahiyo 10,001 itasomwa,kumi elfu na moja.
 
Kumi elfu na elfu kumi zote mbili zinatumika. Naona Kumi Elfu ni Kiswahili sanifu, maana tunaweka namba baada ya jina linalohesabiwa (nyumba kumi, watoto wanne). Hapa "elfu" itazamiwe kama jina linalohesabiwa.

Ila tu kwa sababu watu wote wanajifunza kiasi cha Kiingereza, basi "kumi elfu" inaonekana ni athira ya Kiingereza inayoweka namba kabla ya jina (ten houses, four children, ten thousand)
 
Back
Top Bottom