On the Brink: What is troubling Tanzanian Economy?

Mwanakijiji, Rais kakujibu hoja, anawatuma mawaziri wakatembelee nchi wajionee kero za wananchi, another expense...
 
Tukisema sera zao zimeshindwa wengine wanafikiria tunatafuta ugomvi jamani; ndio tunavuna sasa?
 
Kukopa per se siyo dhambi. Miaka ya 50 wamarekani walikopa sana kujenga mtandao wao wa barabara. Lakini inapendeza sana pale serikali inapopata mapato yake (hasa ya kujikimu), kupitia kodi.


Akchuale, Merekani imekuwa inakopa toka nyuma zaidi ya hapo. Rejea kauli mbiu ya "New Deal" ya Roosevelt, sera na mikakati ya kipindi kile. Ile ndio for lack of a better term, "textbook Keynesianism".

Kifupi ni kwamba ili utengeneze fedha ni sharti utumie fedha ila ni namna gani na maeneo gani unawekeza mtaji wako ndipo panapogomba kwa Tanzania. Kama taifa tumekosa vipaumbele vya muda mrefu ambavyo sacrifices are made kuweza kuzirealize. Angalia sera ya mapinduzi ya kijani na utamaduni yalivyozikwamua China na India. It is simple, unapokuwa na malengo madhubuti ya muda mrefu, vikwazo vya hapa na pale hususani wakati wa awali ni lazima vitumike kama changamoto na uzoefu wa namna ya kufanya mambo yaende sawasawa. Badala yake sisi Tanzania huwa tunakimbilia mbinu ya mbuni ya kufukia kichwa mchangani pindi mambo yakienda mrama kidogo na kuanza kulaumiana na hata kureverse course badala ya kujifunza.


Simaanishi kuwa sasa serikali iende ikaongeze kodi, kwani hiyo ni mbaya kama kukopa mabenki. Serikali inaweza ikaongeza kodi kwa kufanya yafuatayo;

1. Weka mazingira ya ku-attract FDI. FDI huwezesha miradi mikubwa ambayo uwezo wetu haufiki. Mfano, mtaji wa kujenga mgodi mmoja unaweza kufikia Dollar billionij moja. Utazitowa benki gani pesa kama hiyo hapa TZ?

Kwa muda mrefu sana TZ tumekuwa tukitoa picha ambayo haiko consistent. Tunaalika FDI, wakija tunawachenjia


Mbona haya mazingira yamekuwepo kwa zaidi ya miaka kumi na ushee sasa? Sera ya Uwekezaji ya 1997, sera za mawasiliano, madini, kanda maalumu za uchumi/biashara? Kwa upande wa FDI, Tanzania mbona imeweza kuvutia wawekezaji zaidi toka nje toka kwa kiasi cha dola milion 150.9 mwaka 1995 mpaka 573.3 mwaka 2010? tena na haya yakiwa ni mapungufu ya kutoka $744mil mwaka 2008 (kutokana na misukosuko ya uchumi duniani na kukamilika kwa uanzishwaji wa Buzwagi). Matatizo makubwa katika upande wa sera ya kuvutia wawekezaji yamekuwa ni:
Mosi, Kushindwa kuweka tayari mifumo ya kuwezesha mtiririko wa keki ya mwekezaji kwa wazawa walio wengi kupitia, miundo mbinu mibovu, sheria mbovu za uhamiaji zinazotoa upendeleo kwa wageni hata kama hawakidhi sifa stahili, kushindwa kuwekeza ipasavyo kama maeneo jirani na sites za uwekezaji ili kuweza kubana keki isitoke nje. Tumeshindwa kuanzisha miji midogo yenye kujihimili yenyewe kuzunguka machimbo yetu yote ya madini hali inayopelekea mpaka tenda za kusambaza kuku kupelekwa Afrika Kusini au Kenya.

Pili, Ukosefu wa uzalendo na uaminifu miongoni mwa mwetu hususani kwa walioopewa dhamana ya kuliwakilisha taifa katika kuandaa rasimu za sera na mikataba mbalimbali. Haingii akilini leo hii mgeni kukodishiwa ardhi kwa miaka 99, 66 au kipindi chochote kile cha zaidi ya miaka mitano

Tatu, Making tooo any positive assumptions about the potential benefits of greenfield investments when evidence points to the contrary. Time and time again unasikia porojo za utengenezwaji wa ajira ilihali hakuna support chains za uhakika na pia investments zenyewe ni capital intensive.

Nne, kudharau na kunyanyasa wawekezaji wazawa. Requirements za TIC, SEZ/EPZ ni lazima zitoe kipaumbele kwa ili kuwawezesha wazawa kunufaika na nchi yao. Hapa ni lazima kuwe na affirmative action kuwahamasisha wazawa wawekeze nchini

2. Makali ya sheria ya TRA yapunguzwe. Uwezo wa TRA ku-block account ya kampuni hufanya wengi kuweka hela zao nje. Hizi hela zingekuwa hapa nchini, zingetumika katika uwekezaji


Sheria ya TRA haina tatizo katika hilo, tatizo lipo katika ukizani baina ya sheria hiyo na mkakati mzima wa MKURABITA, jambo linalofanya MKURABITA kuwa ni kisingizio cha wataalam kulamba posho bure. Pato la taifa la Tanzania linashindwa kujumuisha shughuli za uzalishaji katika sekta isiyo rasmi ambayo inakadiriwa kuwa na thamani angalau ya asilimia 50 na pato la taifa linalohesabiwa.
Ajira nyingi zipo katika sekta isiyo rasmi, sekta ambayo inanyanyaswa kutokana na uvivu wa kufikiri wa serikali unaotaka kumkamua yule anayelipa mpaka ashindwe kulipa tena siku inayofuata.

3. Serikali ipunguze matumizi. Iachane na magari ya kifahari na ipunguze ukubwa wake.

Hawa waheshimiwa wetu hawana chembe ya aibu wala huruma. Wao wanataka kuishi kama miungu watu. Ukitazama vizuri takwimu za matumizi ya serikali utagundua ya kwamba toka tulivyoanza kunufaika na mpango wa unafuu wa madeni toka kwa wakopeshaji wakubwa (Multilateral Debt Relief Initiative) mwaka 2004, ile ziada ya fedha ambayo tulitakiwa tuiwekeze katika maendeleo tumekuwa tunaitumia katika kureverse mantiki nzima ya Civil service reform ya miaka ya 90 kwa kisingizio cha kuajiri watumishi katika sekta za huduma ya jamii.


4. In the long term: serikali ifumue kabisa mfumo wa elimu. Ni bora turudi Cambridge system - hii ya sasa inazalisha nguvu kazi isiyo tayari kukabiliana na mfumo wa uchumi tandawazi (hawaajiriki, hawana uwezo wa kutunga sera zinazofaa, hawawezi ku-negotiate mikataba migumu, hawana uwezo wa kuendesha mashirika nk)

Ufumuaji wa mfumo wa elimu unahitajika ila sio kurudi katika mfumo wa Cambridge. Tunahitaji kutoa kipaumbele sawa kwa elimu ya kazi stadi na ufundi. Tuna watoto wengi sana wanaoshindwa kuendelea na elimu ya sekondari, sekondari ya juu pamoja na elimu wa juu, ambao wanakuwa hawana stadi za maisha za kuwawezesha aidha kujiajiri wenyewe au kuchangia katika uzalishaji wa taifa. Wengi wao hawa wanaishia kuishi maisha yasiyokuwa na mwelekeo. It is high time tukajifunza kutoka kwa wenzetu wa Scandinavia na Ujerumani jinsi gani elimu ya mafunzo inavyoweza kutoa mchango mkubwa kwa jamii na uchumi kwa ujumla.

Mafundi mchundo hawapatikani darasani, wako kwenye makarakana
 
Tatizo kubwa linaloisumbua Tanzania ni assumptions. Assumptions kwamba jobs will be created without knowing how, assumptions kwamba the government should be the primary provider of all things essential, assumptions kwamba tija katika uzalishaji itaongezeka bila ya kuewekeza katika namna ya kuongeza tija, assumptions kwamba soko la bidhaa zetu lipo nje ya Afrika tu na lastly assumptions kwamba mungu atatusaidia tu tutafika.

We need to go back to the drawing board, set one or two core priorities then pursue them vigorously. Katika hili ni lazima niwe kweli, kuna vitu ambavyo payoff period yake inachukua muda kuliko vingine wakati pia vina umuhimu, elimu ni mojawapo.
 
Tz is being troubled by Blah Blah even in serious matters that need professionalism!
 
Back
Top Bottom