Elections 2010 On TBC1: Augustine Mrema vs John Mrema vs Meira (jimbo la Vunjo)

Lyatonga bwana . . .

Kalalamika kuwa watu wanadai kuwa yeye Mzee . . . kawatolea nje kuwa Bungeni hawaendi kubeba zege. Pia wanasema yeye mgonjwa . . mbona wengi tu wagonjwa . . . yeye yuko fit sana hata mke wake anajua . . . haaaa haaa

Inanikumbusha mambo ya Mzee Kenyattta . . . . Kwamba Muulizelini Mama Ngina . . . Ni nini ninamfanya usiku . . . .

Du! wagombea nao bwana . . .
 
Superman shukrani sana hata sisi tulio ng'ambo tunapata habari kama tuko nyumbani, asante sana kaka, vipi huko bado technologia ya live streaming online haitumiiki mzee, tungefanya utaratibu tukawa tunazipata events on live video streaming ingekuwa poa kweli, nifikishie ujumbe kwa moderator, hata kama kuna gharama kidogo tungeweza changia wakubwa
 
Kwa haya machache niliyosoma hapa inaonyesha wazi viongozi nchini sii wazoefu kabisa wa Mdahalo. Hawa wote wanazungumza kama vile wao ni wagombea wa kiti cha Urais. Hakuna kati yao anayezungumzia matatizo ya watu na mazingira ktk jimbo lake na ku direct uwezo wake kuwakilisha wanajimbo badala yake zinazungumzwa sera za vyama vyao Kitaifa kama vile kila jimbo litapokea huduma sawa na matatizo yetu yanafanana.

Hii haiwezi kuwasaidia kabisa wananchi wa jimbo husika ikiwa mbunge anashindwa kuzungumzia kero za wananchi wake kuwa ndio sababu yake yeye kugombea. Kinachofanyika ni siasa tupu yaani wanashindwa kuzungumzia matatizo yanayowakabiri wana jimbo na kuna mipango gani ya kuwawezesha wao..
 
Lyatonga bwana . . .

Kalalamika kuwa watu wanadai kuwa yeye Mzee . . . kawatolea nje kuwa Bungeni hawaendi kubeba zege. Pia wanasema yeye mgonjwa . . mbona wengi tu wagonjwa . . . yeye yuko fit sana hata mke wake anajua . . . haaaa haaa

Inanikumbusha mambo ya Mzee Kenyattta . . . . Kwamba Muulizelini Mama Ngina . . . Ni nini ninamfanya usiku . . . .

Du! wagombea nao bwana . . .

Superman shukrani sana hata sisi tulio ng'ambo tunapata habari kama tuko nyumbani, asante sana kaka, vipi huko bado technologia ya live streaming online haitumiiki mzee, tungefanya utaratibu tukawa tunazipata events on live video streaming ingekuwa poa kweli, nifikishie ujumbe kwa moderator, hata kama kuna gharama kidogo tungeweza changia wakubwa
 
Kwa haya machache niliyosoma hapa inaonyesha wazi viongozi nchini sii wazoefu kabisa wa Mdahalo. Hawa wote wanazungumza kama vile wao ni wagombea wa kiti cha Urais. Hakuna kati yao anayezungumzia matatizo ya watu na mazingira ktk jimbo lake na ku direct uwezo wake kuwakilisha wanajimbo badala yake zinazungumzwa sera za vyama vyao Kitaifa kama vile kila jimbo litapokea huduma sawa na matatizo yetu yanafanana.

Hii haiwezi kuwasaidia kabisa wananchi wa jimbo husika ikiwa mbunge anashindwa kuzungumzia kero za wananchi wake kuwa ndio sababu yake yeye kugombea. Kinachofanyika ni siasa tupu yaani wanashindwa kuzungumzia matatizo yanayowakabiri wana jimbo na kuna mipango gani ya kuwawezesha wao..

Thanks kwa kuliona hilo!!!! wako too general; kuna haja ya kupata msaada wa watu wa marekani tuweze ku-disect majimbo kiutendaji zaidi

Nakumbuka niliwahi kusikia mgombea mmoja wa ccm primaries, aliweka vizuri sana mpango wake kwa kuanzia kata, hadijimbo kamili, na pia aligusa sekta zote na akamalizia na land plan ya jimbo kwa kuangali namna geography ilivyokaa [nadhani ni kondoa kaskazini]; lakini hakupata wakampa yule wa shaa shaa
 
Mgombea wa ccm ni Meela au Meira? kuna posts nyingi hapa Jamvini wameandika Crispin Meela.
 
Nilifuatilia kwa umakini mkubwa mdahalo wa wagombea ubunge jimbo la Vunjo, uliorushwa na TBC juzi. Kwanza nilishtuka niliposikia Kijana John Mrema anasema kuwa ana umri wa miaka 30. Alionekana mchanga sana akilinganishwa na wapinzani wake pale; Lyatonga wa TLP na Meela wa CCM.

Hata hivyo baada tu ya kupewa kipaza kila mgombea aanze kwa dk 5 za kujieleza kwa ufupi, nilisisimka jinsi John Mrema alivyojieleza kwa umahiri mkubwa, akitoa takwimu mbalimbali na kuzihusisha na mipango yake. Kwa kweli kwa mtu yeyote aliwasikiliza na kama yuko fair, atakubali kuwa yule kijana aliwaacha kwa mbali sana wapinzani wake kwa uwezo wa kujieleza na mipango makini. Hali iliendelea kuwa hivyo hata pale walioanza kuulizwa maswali kwani John Mrema alijibu kwa ufupi, lakini kwa umahiri mkubwa. Sijui upepo uko vipi huko lakini kama yule kijana akienda bungeni..., Dah CHADEMA watatisha.
 
Back
Top Bottom