Nyamtalakyono
JF-Expert Member
- Dec 17, 2015
- 795
- 479
Mh Mama yetu kipenzi na Rais wetu nakusalimu Kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwanza kabisa napenda kukupongeza kwa kazi nzuri unazozifanya kwa ajili ya kuiletea nchi yetu ya Tanzania maendeleo. Lakini kwangu naomba nichukue moja ambalo ninalichukua kurudia kukupongeza kwalo ambalo ni ujenzi wa vyumba vya madarasa.
Kuna baadhi ya watu ambao wanabeza kuwa unakopa eti nchi itauzwa bila kukumbuka kuna bomu lilikuwa limeandaliwa la kundi kubwa la wanafunzi wanaitwa wa Elimu bure ili likulipukie ili maneno yawe mengi zaidi ya kwamba watoto wamemaliza Elimu ya Msingi wamekosa nafasi ya kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa vyumba vya madarasa.
Ulichokifanya ni kikubwa na sidhani kama mbeleni tutakuwa na uhaba wa vyumba vya madarasa sekondari maana wanafunzi wanaofuata baada ya hawa wa mwaka huu takwimu zao zinapongua.
Hili lilikuwa ni gumu na kama mama umejiongeza pakubwa sana kunusuru wanao wasife njaa. Hakika nani kama mama.
Baada ya kusema hayo nina ombi moja.
Mimi ni miongoni mwa Walimu niliondolewa kazini kutokana na changamoto ya vyeti. Kama unavyojua mama yetu watu wengi tena wengine walikuwa watendaji wazuri kazini walikumbwa na shida hiyo ambayo ilipelekea familia zetu kuyumba, watoto kushindwa kuendelea na masomo na baadhi yetu kupata magonjwa ya moyo hata vifo hasa ukizingatia tulivyoondolewa ghafla bila hata ya kujua wapi pa kuelekea.
Sasa wewe kama mama najua unajua uchungu wa mwana na unajua furaha ya mwana maana nilikusikia siku ya kuzaliwa kwako unasema ukipata msongo wa mawazo unawaita wajukuu Ikulu unacheza nao wanakupa furaha.
Naomba ufikirie kuturejesha kazi au kutulipa mafao yetu kwa pale tulipotumika ili walau uturejeshee furaha sisi na familia zetu.
Najua watu watakubeza kwa hili lakini najua utakuwa umegusa na kufuta machozi ya watu wengi.
NB: Jaribu kufuatilia kwa kutumia vyombo vyako vya usalama utabaini waliondolewa kazini wengi walikuwa wachapakazi na tegemeo kubwa.
Mungu akuongoze kwa hili na hakuna aliyemkamilifu hapa duniani.
Kwanza kabisa napenda kukupongeza kwa kazi nzuri unazozifanya kwa ajili ya kuiletea nchi yetu ya Tanzania maendeleo. Lakini kwangu naomba nichukue moja ambalo ninalichukua kurudia kukupongeza kwalo ambalo ni ujenzi wa vyumba vya madarasa.
Kuna baadhi ya watu ambao wanabeza kuwa unakopa eti nchi itauzwa bila kukumbuka kuna bomu lilikuwa limeandaliwa la kundi kubwa la wanafunzi wanaitwa wa Elimu bure ili likulipukie ili maneno yawe mengi zaidi ya kwamba watoto wamemaliza Elimu ya Msingi wamekosa nafasi ya kuendelea na masomo kutokana na ukosefu wa vyumba vya madarasa.
Ulichokifanya ni kikubwa na sidhani kama mbeleni tutakuwa na uhaba wa vyumba vya madarasa sekondari maana wanafunzi wanaofuata baada ya hawa wa mwaka huu takwimu zao zinapongua.
Hili lilikuwa ni gumu na kama mama umejiongeza pakubwa sana kunusuru wanao wasife njaa. Hakika nani kama mama.
Baada ya kusema hayo nina ombi moja.
Mimi ni miongoni mwa Walimu niliondolewa kazini kutokana na changamoto ya vyeti. Kama unavyojua mama yetu watu wengi tena wengine walikuwa watendaji wazuri kazini walikumbwa na shida hiyo ambayo ilipelekea familia zetu kuyumba, watoto kushindwa kuendelea na masomo na baadhi yetu kupata magonjwa ya moyo hata vifo hasa ukizingatia tulivyoondolewa ghafla bila hata ya kujua wapi pa kuelekea.
Sasa wewe kama mama najua unajua uchungu wa mwana na unajua furaha ya mwana maana nilikusikia siku ya kuzaliwa kwako unasema ukipata msongo wa mawazo unawaita wajukuu Ikulu unacheza nao wanakupa furaha.
Naomba ufikirie kuturejesha kazi au kutulipa mafao yetu kwa pale tulipotumika ili walau uturejeshee furaha sisi na familia zetu.
Najua watu watakubeza kwa hili lakini najua utakuwa umegusa na kufuta machozi ya watu wengi.
NB: Jaribu kufuatilia kwa kutumia vyombo vyako vya usalama utabaini waliondolewa kazini wengi walikuwa wachapakazi na tegemeo kubwa.
Mungu akuongoze kwa hili na hakuna aliyemkamilifu hapa duniani.