Ombaomba wanaotumia watoto

Domo Kaya

JF-Expert Member
May 29, 2007
531
59
Ndugu zangu Watanzania wenzangu, katika vitu vinavyo niumiza akili yangu ni hili la Omba omba wa wanawake kutumia watoto wao wachanga kupata huruma kwa wapita njia barabarani.

Hii hali imekuwa ikindelea kuongezeka kila siku hapa jijini na Serikali yetu imelinyamazia kimya hili swala, Mtoto mchanga kabebwa mgongoni na mama yake anatembezwa barabarani mchana kutwa jua lake mvua yake, haki ya huyu motto ni nini hasa? Ustawi wa jamiii kazi yake nini katika Nchi yetu hii. Hawa watoto nani atawasaidia ili waweze kupata haki zao za msingi kama watoto?

Watunga sheria kwanini wasitunge sheria inayowahusu hawa watoto wanaotumiwa kama mradi na wazazi wao, Ukisimama barabarani anakuja mama na mototo wake mgongoni anaomba msaada, hana kilema cha aina yeyote, ukimuuliza baba wa mototo yupo wapi utasikia amekufa, au alinipa mimba akanitelekeza kumbe uongo mtupu baba zao wapo na wanaishi pamoja. Kuna Yule mama mwingine kule ocean road anayeshinda na kulala pale ufukweni alianza na mototo mmoja na sasa wamefika wane(4) hivi hii ni bahati mbaya kweli, kuna kituo cha redio kimoja waliwahi kumchangishia hela ya mtaji ili arudi kwao Kigoma akafanye biashara ndogondogo imfae na wanae hakwenda kokote mpk leo yupo, aliwahi kushauriwa awapeleke watoto ustawi wa jamii wapate kulelewa na wasome amegoma akijua wale ndio mtaji wake wa kujiingizia pesa.

Hii ni haki kweli, wale watoto wakikuwa watafanya nini au na wao ndio wawe ombaomba au ndio vibaka wajao?

Mimi nadhani Sheria ingechukua mkondo wake kwa kuwafikiria hawa watoto na future yao wakikuwa.

Njia rahisi ni kila mama anayeingia barabarani na mototo mgongoni kuombaomba Serikali/Ustawi wa jamiii wampokonye mototo na akalelewe kwenye vituo maalulu vya kulelea watoto.

Hii itasaidia kama mtu anataka kuwa omba omba aache motto nyumbani atangetange peke yake…….. hii haingii akilini mtu mungu kakuumba na viungo vyako kamili kwa nini ukae barabarani na motto kuomba. Kwa nini usitafute biashara ndogo ndogo ufanye uweze kulea motto.

Huu ni uzembe na serikali yetu kwa ujumla inachangia hili kwa kuwafumbia macho hawa wazazi.

Sijui wenzangu mnalionaje hili swala kwa upande wenu.

Nawakilisha.
 
Mi wale watoto huwa wananiumiza sana.

Ukiacha hao wa mgongoni kuna wengine wapo kwenye umri wa kusoma ila hata shule hawaendi. Tatizo tunaweza kuwalaumu serikali ila omba wengi wanayafurahia hayo maisha. Kuna mmoja mtoto alisema wazazi wake wamekufa hasomi anaishi barabarani tukataka kumchukua ila yule mtoto alikataa kata kata pamoja na kumuahidi tungemsaidia.

Huku nilipo ndio hadi kero, mtu anakuomba ukimwambia huna anakukaripia au anakufyonya.
Ukiwasaidia ndio wanaendelea kuomba, ukiacha kuwasaidia mara nyingine nafsi inakusuta. Hata sijui wafanywaje hawa wenzetu.
 
Mi wale watoto huwa wananiumiza sana.
Ukiacha hao wa mgongoni kuna wengine wapo kwenye umri wa kusoma ila hata shule hawaendi. Tatizo tunaweza kuwalaumu serikali ila omba wengi wanayafurahia hayo maisha. Kuna mmoja mtoto alisema wazazi wake wamekufa hasomi anaishi barabarani tukataka kumchukua ila yule mtoto alikataa kata kata pamoja na kumuahidi tungemsaidia.
Huku nilipo ndio hadi kero, mtu anakuomba ukimwambia huna anakukaripia au anakufyonya.
Ukiwasaidia ndio wanaendelea kuomba, ukiacha kuwasaidia mara nyingine nafsi inakusuta. Hata sijui wafanywaje hawa wenzetu.

Hunifikii kwa uchungu ninaopata.

Hivi wale watoto pale fire vipi? Hata magari ya mawaziri si huwa yanapita pale wakati wanaenda Kuangalia mashamba yao kule bagamoyo siku za wkend?
 
Mie niliwahi kumwambia mtoto mmoja maeneo ya fire aje nyumbani afanye kazi za ndani alinitukana mbona nilijuta hadi leo hii nimeacha kabisa kuwapa hela.
 
Hunifikii kwa uchungu ninaopata.

Hivi wale watoto pale fire vipi? Hata magari ya mawaziri si huwa yanapita pale wakati wanaenda Kuangalia mashamba yao kule bagamoyo siku za wkend?

We acha tu ndugu yangu, ukiacha hao wa fire, wapo wengine pale feri, ukipita asubuhi walivyopangana wamelala ndio utaumia zaidi, lakini chanzo cha haya yote ni wazazi......,

Mzazi anaanza kuomba na huyu mtoto tangu yupo mgongoni hapo unadhani akifikisha miaka mitatu-minne anafanya nini zaidi na yeye kuchukua tabia hiyo hiyo...... mimi ndio maana nikasema Ustawi wa jamiii ingewachukua watoto wote wanaotumiwa na wazazi wao (watoto wa mgongoni) wakalelewe kwenye vituo vya kulelea watoto, wangepungua hawa watoto huko mitaani wakabaki wale wanaotoroka majumbani mwao, hao nao Serikali ingeangalia jinsi ya kuwapunguza.
 
sheria inamruhusu mtu mzima yoyote amwonapo mtoto mdogo (kama hawa tunaowazungumzia) akirandaranda hovyo barabarani 'kumkamata' na kumfikisha kituo cha polisi au kituo cha ustawi jamii. polisi wanatakiwa kuwapeleka hawa watoto kwenye vituo vya ustawi wa jamii, kama hana kwao. kwa hiyo kwa watoto wanaombaomba ni wazi kila mmoja wetu anao wajibu wa kumfikisha kwenye vituo vya ustawi wa jamii, hiyo ni kwa mujibu wa sheria yetu. tatizo hapa ni kuwa ustawi wa jamii ilishajifia siku nyingi na hawana habari tena na watoto hawa. imebaki kushiriki kwenye kesi chache cha adoption ambazo mhusika atawezeshwa kidogo ili atoe taarifa kuwa adopter ni mtu sahihi kum-adopt mtoto mtarajiwa! ni mfumo wetu mbovu wa utawala unaolikuza hili tatizo la watoto wa mitaani na ukweli ni kuwa hili ni bomu linalosubiri kulipuka tena kwa kishindo hasa. watoto hawa huishia kuwa wahalifu tena wahalifu hatari kabisa wenye chuki (subconsciously) dhidi ya jamii inayowazunguka.
 
sheria inamruhusu mtu mzima yoyote amwonapo mtoto mdogo (kama hawa tunaowazungumzia) akirandaranda hovyo barabarani 'kumkamata' na kumfikisha kituo cha polisi au kituo cha ustawi jamii. polisi wanatakiwa kuwapeleka hawa watoto kwenye vituo vya ustawi wa jamii, kama hana kwao. kwa hiyo kwa watoto wanaombaomba ni wazi kila mmoja wetu anao wajibu wa kumfikisha kwenye vituo vya ustawi wa jamii, hiyo ni kwa mujibu wa sheria yetu. tatizo hapa ni kuwa ustawi wa jamii ilishajifia siku nyingi na hawana habari tena na watoto hawa. imebaki kushiriki kwenye kesi chache cha adoption ambazo mhusika atawezeshwa kidogo ili atoe taarifa kuwa adopter ni mtu sahihi kum-adopt mtoto mtarajiwa! ni mfumo wetu mbovu wa utawala unaolikuza hili tatizo la watoto wa mitaani na ukweli ni kuwa hili ni bomu linalosubiri kulipuka tena kwa kishindo hasa. watoto hawa huishia kuwa wahalifu tena wahalifu hatari kabisa wenye chuki (subconsciously) dhidi ya jamii inayowazunguka.

Mkuu Manumbu na Domo kaya,

Hizi ndizo hasa issues ambazo sisi kama wanajamii tunapaswa kuzijadilli na kuzipatia majibu na muafaka ,lakini siku hizi kijiwe hichi kimeingiliwa watu sijui kwanini tuna zirusha akili zetu na tunaanza kujadiri mambo yasio ya masingi.
Maada hii ingalikua ni ya umbea au udaku kumjadiri mtu,washabiki wangekuwa wengi sana lakini tazama....ni watu wachache tu wamechangia na kuonyesha kuguswa kwako.
Kama ulivyo sema Mkulu Manumbu,hili ni BOMU linalosubiri kulipuka ni kweli vile maisha yanavyo endelea hawa watoto wana kuwa wakubwa na future zao ni kiza kinene wataishia kuwa wakabaji,wezi ,majamabazi na mengineyo mabaya zaidi.Nasisi kama watu tunao jiita "makini" GREAT THINKERS sasa tuna fumbua macho tu na baadae sisi tunakuja kushusha lawama
 
Mkuu Manumbu na Domo kaya,

Hizi ndizo hasa issues ambazo sisi kama wanajamii tunapaswa kuzijadilli na kuzipatia majibu na muafaka ,lakini siku hizi kijiwe hichi kimeingiliwa watu sijui kwanini tuna zirusha akili zetu na tunaanza kujadiri mambo yasio ya masingi.
Maada hii ingalikua ni ya umbea au udaku kumjadiri mtu,washabiki wangekuwa wengi sana lakini tazama....ni watu wachache tu wamechangia na kuonyesha kuguswa kwako.
Kama ulivyo sema Mkulu Manumbu,hili ni BOMU linalosubiri kulipuka ni kweli vile maisha yanavyo endelea hawa watoto wana kuwa wakubwa na future zao ni kiza kinene wataishia kuwa wakabaji,wezi ,majamabazi na mengineyo mabaya zaidi.Nasisi kama watu tunao jiita "makini" GREAT THINKERS sasa tuna fumbua macho tu na baadae sisi tunakuja kushusha lawama

Hujakosea ndugu yangu Sanda, Baadae wakija kuwa majambazi/vibaka wataishia kuchomwa moto huku wananchi wakishangilia, wewe unadhani wale vibaka wanaopokonya simu watu wakiwa kwenye foleni pale Salender ni kina nani, ni hao hao watoto ambao wameshakuwa wakubwa na hawana cha kufanya kupata ridhi yao ya kila siku.

Ili kukomesha hili lazima Serikali na sisi wananchi tuangalie nini cha kufanya.

Hao wanaojiita Sirikali pia huwa wanapitia humu kujua nini kinajadiliwa, hebu kila mtu ajalibu kutoa mawazo yake labda yatafanyiwa kazi.
 
mkulu Dm,
Sisi watanzania sio watu wakutafuta majibu kabla ya majanga kutufika always tunasubiri mpaka matatizo na majanga kutufika ndio TUUNDE tume!
hapa wapo wengi tu HAO unao waita WATENDAJI WA SERIKALINI ,watakaa kimya kwenye hili baadae watatumia HILI kama mtaji wa kisiasa kujiongezea umaarafu kwa "wapiga kura"
 
Mie niliwahi kumwambia mtoto mmoja maeneo ya fire aje nyumbani afanye kazi za ndani alinitukana mbona nilijuta hadi leo hii nimeacha kabisa kuwapa hela.

ni kweli wengi wana kauli chafu sana, ila kisasi unachowalipizia kinawaathiri wengine na sio yule aliyekutukana.
Kunjua moyo.
 
.

Hivi wale watoto pale fire vipi? Hata magari ya mawaziri si huwa yanapita pale wakati wanaenda Kuangalia mashamba yao kule bagamoyo siku za wkend?

kutoa ni moyo ndugu yangu haijalishi mtoto wa waziri au wa bar maid.
Kama upo barabarani uki observe watu wanaowapa mia mia wale omba utagundua wengi ni abiria waliopo kwenye daladala. Magari binafsi hata kugeuka hageuki.
 
Ndugu zangu Watanzania wenzangu, katika vitu vinavyo niumiza akili yangu ni hili la Omba omba wa wanawake kutumia watoto wao wachanga kupata huruma kwa wapita njia barabarani.

Hii hali imekuwa ikindelea kuongezeka kila siku hapa jijini na Serikali yetu imelinyamazia kimya hili swala, Mtoto mchanga kabebwa mgongoni na mama yake anatembezwa barabarani mchana kutwa jua lake mvua yake, haki ya huyu motto ni nini hasa? Ustawi wa jamiii kazi yake nini katika Nchi yetu hii. Hawa watoto nani atawasaidia ili waweze kupata haki zao za msingi kama watoto?

Watunga sheria kwanini wasitunge sheria inayowahusu hawa watoto wanaotumiwa kama mradi na wazazi wao, Ukisimama barabarani anakuja mama na mototo wake mgongoni anaomba msaada, hana kilema cha aina yeyote, ukimuuliza baba wa mototo yupo wapi utasikia amekufa, au alinipa mimba akanitelekeza kumbe uongo mtupu baba zao wapo na wanaishi pamoja. Kuna Yule mama mwingine kule ocean road anayeshinda na kulala pale ufukweni alianza na mototo mmoja na sasa wamefika wane(4) hivi hii ni bahati mbaya kweli, kuna kituo cha redio kimoja waliwahi kumchangishia hela ya mtaji ili arudi kwao Kigoma akafanye biashara ndogondogo imfae na wanae hakwenda kokote mpk leo yupo, aliwahi kushauriwa awapeleke watoto ustawi wa jamii wapate kulelewa na wasome amegoma akijua wale ndio mtaji wake wa kujiingizia pesa.

Hii ni haki kweli, wale watoto wakikuwa watafanya nini au na wao ndio wawe ombaomba au ndio vibaka wajao?

Mimi nadhani Sheria ingechukua mkondo wake kwa kuwafikiria hawa watoto na future yao wakikuwa.

Njia rahisi ni kila mama anayeingia barabarani na mototo mgongoni kuombaomba Serikali/Ustawi wa jamiii wampokonye mototo na akalelewe kwenye vituo maalulu vya kulelea watoto.

Hii itasaidia kama mtu anataka kuwa omba omba aache motto nyumbani atangetange peke yake…….. hii haingii akilini mtu mungu kakuumba na viungo vyako kamili kwa nini ukae barabarani na motto kuomba. Kwa nini usitafute biashara ndogo ndogo ufanye uweze kulea motto.

Huu ni uzembe na serikali yetu kwa ujumla inachangia hili kwa kuwafumbia macho hawa wazazi.

Sijui wenzangu mnalionaje hili swala kwa upande wenu.

Nawakilisha.



Huu uzi umetoka mda kidogo but tokana na sababu zilizokua nje ya uwezo wangu sikua jamvini… Namshukuru alotoa Uzi huu kwani ni moja ya maeneo ambayo hunigusa saana (watoto hasa katika vulnerable positions..).. Namshukuru pia na mwana JF mwenzangu aloni PM uzi huu kwa kutambua kabisa kua nitakua interested na kutaka tubadilishane mawazo…

Domo kaya huwezi amini nilikua naanda kitu kinafanana na this thread ili nipost nione Watanzania kupitia JF members wanalichulia vipi hili suala but hamna kilichoharibika ila tu nimesikitika saana kwamba ukweli wa Jamii Forums kama jamvi la Great Thinkers ni kwamba tunakoelekea tutachakachuliwa/kujichakachua na kupoteza kabisa maana halisi ya GT… watoto ambao ndo future generation hawawi considered kabisa katika jamii yetu tokana na ukweli kua sie Watanzania ni wachongaji saana mdomo kwa mambo ambayo hatufaidi directly na hatuna kabisa uzalendo… Tungekua wazalendo ni mambo mengi ambayo tungezingatia na kutafakari hasa katika suala zima la Watoto.. Mfano mdogo hapo Zambia, Lusaka au Ndola wana mabango kubwa (whether you like it or not unaliona) ambalo serkali limeweka kuhamasisha kua hamna kuwapa watoto wa mtaanai msaada wowote… Vivyo hivyo na Malawi pia…

WAZAZI/WALEZI WANAOWATUMA WATOTO

Hawa kwa kweli ilitakiwa wawe wanachukuliwa hatua kabisa for hawafai wala kuwaonea huruma watoto hao ambao mara saa ingine hata wakuwazaa wenyewe… hata hivyo naomba nisiwaongelee saana hawa niwaongelee watoto wenyewe ambao wanahusika moja kwa moja na tabia ya kuomba omba aidha kwa kutumwa ama mwenyewe kuamua kufanya hivyo..

Na kabla sijaenda mbali... naomba ujue Domo Kaya kua akina mama tunafanya kazi kubwa saana kulea familia zetu hivyo naomba mtambue hilo na pia muappreciate nguvu zetu hizo… naamini unajua kua idadi kubwa ya single parents Tanzania kubwa ni akina mama tena hawana hata support – na kuwalea wanae kwa kile kidogo/kikubwa apatacho; as a result of ujane or sababu nyingine nyiiingi!

Katika huo mfano ulotoa wa huyo mama wa watoto wanne, Yule ni special case na anapenda position aliyopo kwani kajaribu kusaidiwa na kushawishiwa atoke pale ikiwemo na serkali yenyewe but hurudi pale pale na anapenda saana wanaume (in her own words…) nilibahatika kusikiliza siku moja interview radion akiwa anahojiwa na Dina Marios… it was so disappointing and cannot go into that right now….

JINSI GANI JAMII INACHANGIA HILI TATIZO..

Watoto wa mtaani kwa sasa wanaongezeka kwa kasi ya ajabu.. na inaniuma saana kua hao watoto na wakike wamekua wengi katika hilo kundi.. jamani mtu yoyote aki comprehend hiki kitu kwa umakini ataona the way ilivyo serious; hapa inatakiwa kuobserve si tu madhara ya papo hapo ambayo pia ni meeengi but kama haitoshi there future is really really bleak…
Watanzania ama niseme wanajamii kwa ujumla ni moja ya sababu kubwa saana kwa kuongezeka idadi ya hao watoto wa jinsi hio mtaani.. Hi ni sababu watu wanatoa msaada kadri awezavyo wakiamini as much as they can help at least wasadie na the little they have… hii ndio mbaya kabisa! Bahati nzuri sifanyi kwa assumptions, maana katika masomo ya elimu ya juu nilibahatika kufanya project inayohusisha watoto wa mtaani… katika kutaka kupata majibu ni kwa nini watoto ni wengi hapa Jijini (Dar) na hali panaongoza kwa vituo vingi vya kulelea watoto hizi ni baadhi ya majibu…

  • Pamoja na kusema watoaji wanatoa pesa ndogo ndogo kama Ths 100/=, Ths 200/=, Tsh 500/= wengine hata zaidi ya hapo; mwisho wa siku hao watoto hufikisha pesa nzuri kama alfu 2/3/4 mpaka hata alfu saba and in rare cases hata zaidi… (na hio information kwa hao watoto unapata kwa kuwahonga… you buy them food talk to them patiently and promise them money to tell the truth… huku ukichukulia aweza kukudanganya but once umewasiliana na wengi unaunganisha moja na moja unapata jibu..)
  • Wazaza/walezi wa watoto hao huwatuma hao watoto kufanya shuguli ya kuomba.. hao watoto wakikusanywa kula baada ya muda na vituo vya watoto yatima au wa mtaani… baada ya siku mbili tatu wanarudi tokana na ukweli yuko huru zaidi kufanya atakalo… baada ya time kujiingiza katika mitihani mbali mbali ambayo imetawala katika miji yetu ya sasa katika ulimwengu ulochafuka!
  • To mention but a few reasons…
SERKALI

Kama kawaida Serkali yetu on paper inamalengo mazuri na Watanzania in most cases.. the problem lies with implementation of those rules, guidelines or policies whatever they call them… Serkali yoote na wizara zake kwa mtazamo wangu naona wame concertrate katika siasa and all the propaganda happening mpaka wanasahau utendaji na bahati mbaya saana hawana hawa watoto hawana watetezi… Hata hivyo napenda ni acknowledge Non Governmental Organisations ambazo naona kama zaongezeka kwa kaasi kuhusiana na welfare za watoto kama Save the Children, Tanzania children Trust Fund, SOS Children’s Village (kama sikosei…), Railway Children Africa, Save the Children, Feed your Children.. to mention but a few… Wimbi kubwa la children related Organisations ni evident kua serkali yetu ililega saana na kushindwa control hio issue mpaka imetoka out of hand na sasa kama kawaida forces from outside imekuja kututatulia hii issue….
 
Mkuu Manumbu na Domo kaya,

Hizi ndizo hasa issues ambazo sisi kama wanajamii tunapaswa kuzijadilli na kuzipatia majibu na muafaka ,lakini siku hizi kijiwe hichi kimeingiliwa watu sijui kwanini tuna zirusha akili zetu na tunaanza kujadiri mambo yasio ya masingi.
Maada hii ingalikua ni ya umbea au udaku kumjadiri mtu,washabiki wangekuwa wengi sana lakini tazama....ni watu wachache tu wamechangia na kuonyesha kuguswa kwako.
Kama ulivyo sema Mkulu Manumbu,hili ni BOMU linalosubiri kulipuka ni kweli vile maisha yanavyo endelea hawa watoto wana kuwa wakubwa na future zao ni kiza kinene wataishia kuwa wakabaji,wezi ,majamabazi na mengineyo mabaya zaidi.Nasisi kama watu tunao jiita "makini" GREAT THINKERS sasa tuna fumbua macho tu na baadae sisi tunakuja kushusha lawama


Nakubaliana nawe na maneno hayo ulooandika katika post yako… Bahati mbaya saana ni kua pamoja na kusema Jamii Forums ina Great Thinkers walokua registered sio chini ya 39,000 people; the sad thing is wale ambao wako interested ni almost HAKUNA! Kisa heading ni Ombaomba wanaotumia watoto - UKITAKA waingie hii thread andika CHADEME VS CCM OR WAKRISTO VS WAISLAM.. ndo utajua kua kweli wachangiaji wapo na basi bora wawe wachangiaji wa kutafakari; unfortunately wengi (hafadhali wangekua wachache, ni waropokaji tu wala haelewi ni nini anaongea ili mradi tu anaona ana uhuru wa kujielezea…) Ukitoka hapo nje unakuta walo pitia hii thread ni kama 190.. katika members wooote hao ambao hata kama nusu tu ya members ndo active haiwezekani watu wawe 190 and of all the 190 walochangia ni 7! JAMANI 7 people on (hata kama wengine wameobserve as guests…) matters concerning our future generation, our children and our Tanzania… INASIKITISHA MNO…
 
sheria inamruhusu mtu mzima yoyote amwonapo mtoto mdogo (kama hawa tunaowazungumzia) akirandaranda hovyo barabarani 'kumkamata' na kumfikisha kituo cha polisi au kituo cha ustawi jamii. polisi wanatakiwa kuwapeleka hawa watoto kwenye vituo vya ustawi wa jamii, kama hana kwao. kwa hiyo kwa watoto wanaombaomba ni wazi kila mmoja wetu anao wajibu wa kumfikisha kwenye vituo vya ustawi wa jamii, hiyo ni kwa mujibu wa sheria yetu. tatizo hapa ni kuwa ustawi wa jamii ilishajifia siku nyingi na hawana habari tena na watoto hawa. imebaki kushiriki kwenye kesi chache cha adoption ambazo mhusika atawezeshwa kidogo ili atoe taarifa kuwa adopter ni mtu sahihi kum-adopt mtoto mtarajiwa! ni mfumo wetu mbovu wa utawala unaolikuza hili tatizo la watoto wa mitaani na ukweli ni kuwa hili ni bomu linalosubiri kulipuka tena kwa kishindo hasa. watoto hawa huishia kuwa wahalifu tena wahalifu hatari kabisa wenye chuki (subconsciously) dhidi ya jamii inayowazunguka.



Manumbu habari yako bana! Asante kwa kunirushia thread really apprecitate…

Nakubaliana na post yako… in fact I have to admit I did not know that.. Iko very logical the way umeelezea but ukweli unabaki kua Watanzania majority shida za maisha na familia ni nyingi mno mpaka kuamua kuchukua hatua ya kushika mtoto mtaani na kumpleka kituo cha polisi ni issue, kwanza kuna tatizo dogo tu moja la foleni – imagine ukamate watoto pale mnazi au manzese uwapeleke kituoni… dah! Ratiba the whole day mparanganyuko na afadhali kama ingekua na guarantee kua it will work.. pili jamii itakayo kuona unadaka huyo motto yaweza ona una nia mbaya na huyo mtoto, tatu polisi watakupokea but kukushangaa.. na wakimpokea once you turn your back the child is definitely OUT!

Kwa mtazamo wangu nafikiri hio sheria inayo ruhusu hivyo ni kama vile hawakutafakari vizuri… in other words mtu yeyote ana uwezo wa kukusanya watoto hata kumi a day akawafanyia biashara na akikamatwa akajifanya anawapeleka kituon… naona kama itakua na mapungufu… sijui wewe unaonaje hilo suala…
 
wadau niwaambieni ukweli wa wale watoto,hao wa mgongoni huwa wanakodishawaga!kwa masaa machache shs 2,000!wanaowabeba sio mama zao!kuhusu hao wakubwa huwa wanakusanywa huko vijijini kwa wazazi wao ndio wanaletwa huku mijini kuomba!serikali ispokuwa makini after 10 jiji litakua balaa tupu!
 
Wale watoto hata uwapeleke home utakaa nao siku ya tatu watakuibia na utawakuta pale pale wakiwa wanaomba. Waache hata wakuu wa kaya wanawaona vizuri tu kwa kuwa wapo kwenye lango la jiji.
 
Back
Top Bottom