Omba isikutokee

Murano

JF-Expert Member
Mar 11, 2012
2,058
1,099
Kijana mmoja aliota amekufa na yupo mbinguni. Akiwa huko, aliambiwa na Malaika kuwa ametolewa roho kwa bahati mbaya hivyo atarudishwa duniani kama mnyama au ndege.
Kijana akachagua awe kuku. Mara akakuta yupo ndani ya kibanda huku akipata hisia asiyoifahamu.
Akamuuliza jogoo pembeni yake, ni hisia gani hii?
Jogoo akamuuliza, ushawahi kutaga ww?
Akajibu bado.
Jogoo akamwambia, hilo ni yai linataka kutoka hivyo kamua kwa nguvu.
Akakamua mara ya kwanza, likatoka yai.
Akaendelea kukamua tena, likatoka jingine.
Ghfla akackia mtu anamuamsha, we ---- mbona UNAKUNYA kitandani? Chezea ndoto wewe!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom