Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,788
- 218,420
Olengurumwa amesikika akiwaambia vyama vya upinzani wasigombee Urais wa Tanzania, na kwamba ushauri wake huo unataka kinyang'anyiro hicho aachiwe Samia Suluhu Hassan, ambaye kwa akili ya Olengurumwa ndiye mgombea wa CCM wa 2025.
Hatuna shida yoyote na Mwanaccm Olengurumwa kumpigia kampeni Mwenyekiti wa chama chake cha ccm Samia Suluhu Hassan, maana ni wajibu wa kila mwanachama kuhakikisha anampigia kampeni Mwanachama mwenzake, ili ashinde na kutwaa madaraka.
Bali anachopaswa kukumbuka ndugu Olengurumwa ni hiki, Samia Suluhu hakuwahi kuchaguliwa na yeyote ili awe Rais wa Tanzania, ni Rais wa kikatiba tu, kingine ni kwamba Mgombea yeyote wa Urais wa Tanzania ni lazima aombe Urais huo kupitia kwenye chama chake, na baadaye apitie mchujo wa Kamati Kuu na Mkutano Mkuu umpitishe kuwa Mgombea.
Ni kweli kwamba Samia Suluhu ameachana na siasa za kikatili za mtanguliI wake, na ni kweli kwamba nchi ina amani, na ni kweli kwamba kuna maridhiano mezani , lakini vitu hivi havimfanyi yeye kuwa mgombea pekee wa Urais 2025, lakini kingine ni hiki, je, Samia Suluhu ana nia ya kugombea Urais 2025? Mtu ambaye hatogombea awezaje kuwa mgombea pekee?
Kimsingi Olengurumwa amekurupuka ili kupata chochote, bali sisi watu wa Demokrasia tunamuonya aache uchawa, vinginevyo tutaingia vitani naye na hatoweza.
Kama unampenda mtu kwa sababu ya sura yake basi nenda kanywe naye chai - JK Nyerere
Hatuna shida yoyote na Mwanaccm Olengurumwa kumpigia kampeni Mwenyekiti wa chama chake cha ccm Samia Suluhu Hassan, maana ni wajibu wa kila mwanachama kuhakikisha anampigia kampeni Mwanachama mwenzake, ili ashinde na kutwaa madaraka.
Bali anachopaswa kukumbuka ndugu Olengurumwa ni hiki, Samia Suluhu hakuwahi kuchaguliwa na yeyote ili awe Rais wa Tanzania, ni Rais wa kikatiba tu, kingine ni kwamba Mgombea yeyote wa Urais wa Tanzania ni lazima aombe Urais huo kupitia kwenye chama chake, na baadaye apitie mchujo wa Kamati Kuu na Mkutano Mkuu umpitishe kuwa Mgombea.
Ni kweli kwamba Samia Suluhu ameachana na siasa za kikatili za mtanguliI wake, na ni kweli kwamba nchi ina amani, na ni kweli kwamba kuna maridhiano mezani , lakini vitu hivi havimfanyi yeye kuwa mgombea pekee wa Urais 2025, lakini kingine ni hiki, je, Samia Suluhu ana nia ya kugombea Urais 2025? Mtu ambaye hatogombea awezaje kuwa mgombea pekee?
Kimsingi Olengurumwa amekurupuka ili kupata chochote, bali sisi watu wa Demokrasia tunamuonya aache uchawa, vinginevyo tutaingia vitani naye na hatoweza.
Kama unampenda mtu kwa sababu ya sura yake basi nenda kanywe naye chai - JK Nyerere