Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,234
Mratibu Kitaifa wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa, amekosoa tamko la Chama cha Mawakili wa Serikali (PBA) lililopinga uamuzi wa Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) kuwataka wanachama wake kuandamana nchi nzima kulaani tukio la kukamatwa kwa Wakili Deogratius Mahinyila katika Mahakama Kuu jijini Dar es Salaam.
Olengurumwa amesema hatua ya TLS ilikuwa sahihi kwa kuwa inalenga kuwalinda na kuwatetea mawakili wote nchini dhidi ya vitendo vya udhalilishaji au kuzuia utekelezaji wa majukumu yao ya kitaaluma. Ameeleza kuwa uamuzi huo pia ni sehemu ya kulinda heshima ya taaluma ya sheria na kuonesha mshikamano wa kitaaluma pale ambapo mwanachama mmoja anakumbwa na changamoto zinazoweza kudhoofisha uwezo wake wa kutekeleza wajibu wa kisheria.
Olengurumwa amesema hatua ya TLS ilikuwa sahihi kwa kuwa inalenga kuwalinda na kuwatetea mawakili wote nchini dhidi ya vitendo vya udhalilishaji au kuzuia utekelezaji wa majukumu yao ya kitaaluma. Ameeleza kuwa uamuzi huo pia ni sehemu ya kulinda heshima ya taaluma ya sheria na kuonesha mshikamano wa kitaaluma pale ambapo mwanachama mmoja anakumbwa na changamoto zinazoweza kudhoofisha uwezo wake wa kutekeleza wajibu wa kisheria.