Old Skool - tukumbuke nyuma kidogo

Old Skool - tukumbuke nyuma kidogo

Goboshi

Member
Joined
Jul 15, 2013
Posts
63
Reaction score
27
Habari wana jamvi naomba tujikumbushe nyuma kidogo, maisha ya shule ya wakati uleee

Nakumbuka wakati namaliza shule ya msingi mwaka 1989 nilikuwa na miaka 16. Nilionekana mdogo sana darasani kwetu kwani wakati huo hasa vijijini watu walikuwa wanaanza darasa la kwanza wakiwa na pubic hair (mav...ziii). Nilipomaliza shule shule ya msingi nilifauli masomo na kuchaguliwa kujiunga shule ya sekondari Mazengo (Dodoma) na ikawa bahati kusoma kwenye mji wa posho ya kukalia viti vya kunesanesa. Hii si mada yangu ngoja niwaambie waskaji zangu, si mnajua tena stori za old-skool zinaanza na historia fupi!!!

Basi washkaji zangu pale Matesesco ambayo baadae ilikuja kuitwa Mazengo Complex na baadae ikabatizwa Dodoma University kwa majigambo ya walimu wake, nilijikuta naingia shule kusoma na mibaba mizima. Kuna watu walikuwa wanamaliz form four huku watoto wao wakifanya mtihani wa darasa la saba na wengine wakioza mabinti zao wa kwanza. Unashangaa nini, ndo ilivyokuwa wakati ule wa elimu ya kuhimizana. Kwenda shule lazima uwe umepata wa kuku-leave kwenye machungo ya ng'ombe (ukikosa no skool).

Shule yetu ilikuwa ya midume mitupu ikichukua wanafunzi wa O-Level na A-Level. Basi bwana kulikuwa na mgawanyo wa kazi ambapo kuna kazi zilikuwa zinafanywa na form one tu. Palikuwa na form one wa masika (Form One kweli) na form one wa kiangazi (Form Five). Hawa walikuwa na kazi ya kusafisha vyombo vya kitchen kwenye muhula wao wa kwanza wanapojiunga na shule. Basi wale wasiosafisha vyombo na meza wakimaliza kula wanachafua mazingira ili kuifanya kazi iwe ngumu kwa wenzao.

Kulikuwa na T.M.O bana wakati huo hakuna cha mobile phones na hata landlines zilikuwa kwenye maofisi na kwa watu wenye uwezo tu. Basi kila siku kabla ya kuingia kwenye bwalo la chakula unapitia kwenye ubao kusoma kama jina lako limo ili ukchukue hela zako za matumizi. Kama jina lako halija-display mpaka mnapokaribia kufunga inabidi ujiandikishe kubaki shule. Mawasiliano nayo yalikuwa kwa njia ya barua tu na kulikuwa na kitu kinaitwa pen-pal (rafiki wa kalamu). Hicho ndo kilikuwa kikikutanisha wanafunzi wa shule mbalimbali na hasa wavulana kwa wasichana.

Pesa ilikuwa shida lakini barua zilikuwa zinazunguuka tu, kulikuwa na mtindo wa kufuta mhuri kwenye stamp kwa mafuta na kuitumia tena. Ukitumiwa barua yenye stamp mpya, stamp huikuti. Kuna wengine walidiriki hata kurudisha barua kwa kutumia bahasha ya awali kwa kusingizia barua iliotumwa imepotea njia irudi kwa sender.

Basi wana jamvi kuna jamaa mmoja tulikuwa tunasoma darasa moja. Jamaa huyo alipenda sana kwenda kuchukua barua na kuja kuzisoma mbele ya wanafunzi. Jamaa alikuwa na vioja sana. Alikuwa na kofia moja (cap) ya blue ameandika kwa wino Zairwaz, huyu jamaa ilikuwa kila siku lazima apate barua. Na akikosa barua alikuwa anafunga bahasha ya barua zilizopita na kuzisoma upya. Huenda huko mtaani anakoishi (hasa km amepanga) atakuwa anakusanya maganda ya mayai na kuyatupa jalalani mbele za majirani zake.

Kuna mengi sana ya kukumbuka wakati huo .........
 
Wakati huo bwana ....
Kulikuwa na mwalimu mmoja wa Kihindi aliyekuwa na tv, basi unaambiwa kila ikifika weekend wajanja wote ni kwa mama Siraju kuangalia movie za akina Anorld, Rambo, No retreat no surrender n.k. Hayo ndo mapicha ya kipindi hicho bana pamoja na the hard way ...
 
m nilikuwa zangu kjjn nilikuwa nabeba ugal kwenye mfuko na shule ilikuwa mbali sawa na kutoka gongolamboto mpaka tazara unaenda kwa mguu na hiyo ndo shule ya karibu, nakumbuka unaamka alfajir ni ful umande yaaaan we acha tu....!
 
nakumbuka sana enzi hizo nilikuwa seminari moja huko sengerema(Mary Queen of the Apostles Sengerema Seminary), barua zikija lazima Rector hazifungue basi tukabuni kwamba zile barua zote ambazo ni hatarishi zitokazo Bukumbi na Nganza tuwe tunazipitishia sengerema secondari. Tukaweka agenti kule barua zote zikawa zinaaandikwa kwa kupitia kwake, alafu siku tukipata free and out jumamosi ya kwanza ya mwezi tunazifuata.....tulifanikiwa kwa kiasi fulani. Room master siku zote kilikuwa cheo cha form one ili awajibike kusafisha chumba mwenyewe kwani wakuojiwa ni yeye kama chumba kitakuwa kichafu. Tukiwa form one tulikataa kuosha madishi tukapigwa mchinjo(kunyimwa chakula) hadi tukaunda kamati ya kusaidiana tukawa tunachanga pesa na kufata matinda mjini tunajificha polini tunakula kwani sheria ilikuwa hairuhusu kwenda na chakula chochote maeneo ya seminarini, nakumbuka ilikuwa mwezi wa tisa ndo yalitukumba hayo hivyo na sisi tukanuwia kuwatesa kwa mateso makali waseminari watakaokuja kuanza form one sisi tukiwa form two. Kweli tulipofungua shule tu na kuitwa form two watu walipania sana kutesa form one hivyo mimi nilifika jioni siku na kukuta tayari form two watatu wameishafukuzwa kwa kuwalazimisha form one kusukuma choo eti gari ya rector imekwama, walikuwa wakisukumwa huku wakipewa kipigo. Pamoja na hayo yote hatukukata tamaa, utesaji uliendelea na ilipofika mwezi wa tisa tulikaa kikao cha kuhimiza kuongeza kiwango cha utesaji ikiwa ni kukumbuka mateso tuloteswa sisi, kikao kilipendekeza kwamba siku ya mwisho ya kufunga mateso yaani tarh 30/9/....lazima usiku kama Rector na Spritual Director hawatakuwepo kichapo kitolewe. Basi siku ya kuhitimisha mateso kweli Rector hakuwepo, form one walikuwa wanasomea katika ukumbi wa kulia chakula, mimi niliwekwa katika kitengo cha kuzima taa, kilikuwepo kitengo cha fimbo kitakachobaki nje ya ukumbi na kuwacharaza form one wote watakaofanikiwa kutoka nje vilevile kilikuwepo kitengo cha wavamizi ambao taa zikizimwa tu, watavamia na kuanza kutembeza kisago. Kweli nilifanikiwa kuingia mle ukumbini na kujifanya nimekwenda kunywa maji ya kunywa, palepale nilizima taa na fujo zikaanza, tulipanga zoezi hili lifanyike kwa muda wa dakika tatu tu. Baada ya dakika tatu wote tulikuwa tuko darasani, viongozi wengi walikuwa form three hivyo walisikia purukushani walipofika hawakukuta watu kwani form one wote walikuwa wamekimblia vichakani usiku huo na sisi tayari tulikuwa darasani kimya tukijisomea. Baadaye walifanikiwa kumwona form one mmoja raia wa musoma, akawapa full stori alikuwa amepasuka kichwani kwani aliingia chini ya meza akafumuliwa buti moja na li-form two moja pia la musoma. Hofu ilitawala kwa wote viongozi na sisi form two kwani tulijua rector angefika na kukuta hali ile ya kutoonekana baadhi ya form one na kuumia kwa huyo jamaa basi form two wote tungeondoshwa vilevile viongozi nao wangefukuzwa. Hivyo hapakuwa na wakumlaumu mwenzake kwani hata hao viongozi enzi zao walitutendea hayo ingawa ni kwa style nyingine. Ilibidi tukubaliane kuanza kuwatafuta form one kule porini, kazi ilikuwa ngumu kwani kila walipotuona walizidi kujificha wakidhani tunaendeleza kichapo, hadi muda wa kulala saa 4 kamili usiku ilifika baadhi yao wakiwa hawajaonekana, vilevile tulishirikiana na viongozi kumshawishi yule aliyeumia kuwa kesho yake achukue daftari la wagonjwa bila rector kumuona aende hospitali alafu akirudi asitoke nje sisi tutamuhudumia kwa kila kitu ikawa ni pamoja na kumpelekea chakula chumbani. Alikaa ndani kwa muda wa siku tatu ndo akaanza kutoka nje tukamwambia rector akimuuliza aseme aliumia mpirani, kweli alishawishika kwani tulimwambia kuwa hata yeye akifika form two atayafanya hayohayo na mtu akifukuzwa kwa ajiri yake basi hata yeye atafukuzwa kwani akifanya kosa dogo tu huwa inaangaliwa alishawahi kumfukuzisha nani, tulimtisha kwamba ukifukuzisha mtu ikitokea ukakamatwa hata unaongea kiswahili lazima uondoke na huu ndo ulikuwa ukweli......yapo mengi ya kukumbuka, lakini all in all nimefanikiwa kuwa Baba Paroko.
 
Nakumbuka nilikua muongeaji sana darasani kwetu, ikatokea mwalimu akanichagua mimi kuwa monitress na kijana mwingine kuwa moniter. Hatukuwa tunapendana kwani me nilikuwa nawapa support waongeaji yeye alikua anawachomea kwa mwalimu. Nikaanza mtindo wa kwenda na pipi ili kumuhonga monitor asiwaandike majina wenzagu likiwemo la kwangu. Baba akiniletea kopo la pipi, mimi nabebba kadhaa nikagawe kwa monitor niendeleze storiessssssss. Ikatokea siku pipi ziliniishia, jamaa hakuandika jina akitegemea after class ntampa chake. Nami nikaendelea kupiga stori kama kawaida. After class anadai chake sina, ilitokea ugomvi mkubwa sana btn us. Nilikabwa shingo l wont forget that day. Ugomvi ukaishia kwa madam na siri zote zilivuja. I will never forget this.
 
Dah..naweza kumwaga chozi..miaka saba ya umande bila kiatu mguuuni...miaka saba bila kuwa hata na ndala...asilimia 99.9 ya mwanafunzi tulikuwa peku...mpo hapoooooo?
 
nameless...ndo mimi niliyekulamba kabari ya mwaka...teh teh teh
 
Poa wazee wa old skool.
mmesomeka.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
nakumbuka nilikua muongeaji sana darasani kwetu, ikatokea mwalimu akanichagua mimi kuwa monitress na kijana mwingine kuwa moniter. Hatukuwa tunapendana kwani me nilikuwa nawapa support waongeaji yeye alikua anawachomea kwa mwalimu. Nikaanza mtindo wa kwenda na pipi ili kumuhonga monitor asiwaandike majina wenzagu likiwemo la kwangu. Baba akiniletea kopo la pipi, mimi nabebba kadhaa nikagawe kwa monitor niendeleze storiessssssss. Ikatokea siku pipi ziliniishia, jamaa hakuandika jina akitegemea after class ntampa chake. Nami nikaendelea kupiga stori kama kawaida. After class anadai chake sina, ilitokea ugomvi mkubwa sana btn us. Nilikabwa shingo l wont forget that day. Ugomvi ukaishia kwa madam na siri zote zilivuja. I will never forget this.

huyo jamaa lazima ndio hawa mafisadi au sio?
 
MAZEE MIMI NILIKUWA NA SIVAI CHUPI, si unajua enzi zile hakuna chupi za maana zaidi ya 77 na ile ambayo ikikatika kwenye maungi unaweza ukashangaa inefika tumboni.

Basi bwana nikaamua nikachagua kijinzi kimoja maalumu cha kuvalia ndani, hakijawahi kufuliwa, si unajua vuzi linabadilika rangi linakuwa kama rangi ya silva, hivi basi kaptula ikawa kama ngozi ya ng;ombe, siku moja tukaenda zao haooo kuogelea, si mbwa akaibamba jinzi yangu akasepa nayo.:smile-big:
 
MAZEE MIMI NILIKUWA NA SIVAI CHUPI, si unajua enzi zile hakuna chupi za maana zaidi ya 77 na ile ambayo ikikatika kwenye maungi unaweza ukashangaa inefika tumboni.

Basi bwana nikaamua nikachagua kijinzi kimoja maalumu cha kuvalia ndani, hakijawahi kufuliwa, si unajua vuzi linabadilika rangi linakuwa kama rangi ya silva, hivi basi kaptula ikawa kama ngozi ya ng;ombe, siku moja tukaenda zao haooo kuogelea, si mbwa akaibamba jinzi yangu akasepa nayo.:smile-big:

duh kweli ulikuwa mchafu
 
Mwalimu Dungu umemsahau????mama Raju sio Siraju mkuu
Wakati huo bwana ....
Kulikuwa na mwalimu mmoja wa Kihindi aliyekuwa na tv, basi unaambiwa kila ikifika weekend wajanja wote ni kwa mama Siraju kuangalia movie za akina Anorld, Rambo, No retreat no surrender n.k. Hayo ndo mapicha ya kipindi hicho bana pamoja na the hard way ...
 
Shule ya msingi ilikuwa balaa, mtu akiwa na ndala anachaguliwa kuwa kaka mkuu ama dada mkuu.
 
Back
Top Bottom