Asante. Umenikumbusha nitiki maneno ya Paulo katika 1 Tim 2:1-4 "Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote; kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu. Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu."✅
Kauli yako imenikumbusha kutiki maneno ya Paulo katika 2 Kor 5:13 Maana ikiwa tumerukwa na akili zetu, ni kwa ajili ya Mungu; au ikiwa tunazo akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.✅
Kauli yako imenikumbusha kutiki maneno ya Paulo katika 2 Kor 5:13 Maana ikiwa tumerukwa na akili zetu, ni kwa ajili ya Mungu; au ikiwa tunazo akili zetu timamu, ni kwa ajili yenu.✅
Kuna haja gani ya kutuambia unatiki? Kila mtu anajua utatiki basi kaa kimya na hizo tiki zako 3 kwani si kila mtu huvutiwa na kiasi cha ujinga ulionao.
Sijawahi kutumiwa na Ibilisi kuzuia Injili. Kichwa cha habari ulichotumia kina ukakasi ndugu. Hadi hapo bado hujagundua kasoro hiyo? Pamoja na kuhubiri Injili, tumia busara na hekima juu ya maneno unayotumia.
Ukakasi unatoka wapi ndugu yangu? Kutiki ni msemo wa siku nyingi tu. Wewe mwaka huu ndio mara yako ya kwanza unasikia kutiki? Hizi ni nyakati za mwisho, Yesu alisema maasi yataongezeka. Hivyo usitarajie dunia itakuwa mbingu. Badala ya kuhuzunishwa na mambo ya ulimwengu huu, jiandae kwa unyakuo. “Kwa kuwa bado kitambo kidogo tu yeye anayekuja atakuja , wala hatakawia;"(Ebr 10:37)✅
Kumbe wenye kupenda fedha bado mpo. Sasa ninatiki rasmi maneno ya Paulo 1 Tim 6:10 Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi.✅