Habari wana JF, naomba mchango wa mawazo yenu. Kuna kaka ameoa na familia ya watoto 2, mke wake ni mfanyakaz pia anasoma evening classes. Tatizo huyo bibie hapatikani home kuanzia monday to sunday. Weekdays anawahi misa za alfajir hata watoto wanaandaliwa na house girl na baba yao.kurudi ni saa 4 na mafoleni. Dada amejikita kanisani jumamosi anaenda misa ya alfajiri kumi na moja, akitoka anaunganisha shule, jioni anaunganisha kanisani pia ni katibu wa kinamama, mzee wa kanisa kwa maandalizi ya jpili, then anaunga mazoez ya kwaya na kusalimia wagonjwa. Kurudi ni saa 2 au 3. Jumapili anaenda misa ya kwanza, akitoka ni kutembelea wagonjwa, kurud ni jioni kabisa. Watoto mama yao kawa house girl. Ameshaonywa sana, sasa ni miezi mingi.