Tutakujibu baada kujibu maswali haya, 1. Wewe ni nani? Mwanachadema, mwanaccm, mwanaPM7 au raia asiye na upande? 2. Lengo lako ni nini? Kuisaidia Chadema, kuiundia tuhuma za uongo na kuihujumu? 3. Ukishaelewa nani atanufaika? Wewe binafsi, Chadema, ccm au Watanzania na kivipi? bila kuturidhisha hapa hatuna sababu ya kukupa majibu ya maana.
mafunzo yote ya kukumwezesha mwanachama anayekaribia kwenda mstari wa mbele,kiongozi mpya wa chama au mgombea kuwa kamananda mpiganaji! una swali jingine?
CHADEMA wana oganaizesheni ya mafunzo ambayo mkurugenzi wake ni Benson Kigaila. nachotaka kujua je haya ni mafunzo ya darasani ama mafunzo ya namna gani hasa?. ni hilo tu linaloniumiza kichwa. wanachadema naomba mnifahamishe.
Asanteni .
Unaishi dunia ya ngapi wewe?!!. siku hizi sio lazima kila kitu uende ofisini. kama haujui kuhusu hayo mafunzo nyamaza. unasema hapa sio kwa Chadema, ina maana haujui kwamba humu ndani kuna wanachama na viongozi wa ngazi ya juu wa CHADEMA? halafu unajiita Senior Expert member!! Bure kabisa.
Hao wanachadema unaowajua hawajaingia hapa na vyeo vyao vya CHADEMA ni kwamba wametumia Verified ID na hawajifichi kama wa magamba, hivyo haimaanishi hapa ndo maulizo ya CDM. Pia wana mitandao yao nenda ukalalamike kule
asante kamanda kwa ufafanuzi kwa majibu ya kidiplomasia nadhani shomari amekupata kwa mjaarab kabisa! sie wengine tuko kikazi zaidi na majibu yetu yako hivo hivo sowakati mwingine watu hawatuelewi!Mkuu Shomari
Kwanza kabisa, inaitwa Kurugenzi anayoongoza Kamanda Singo Masalamakali Kigaila Benson, inaitwa Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo.
Juu ya hoja yako;
1. Suala la mafunzo kwa CHADEMA si suala la kufuata tukio au matukio, limefafanuliwa wazi na vyema kabisa kwenye kanuni
za chama.
2. Kurugenzi inafuata programu maalum ya mafunzo iliyopitishwa na Kamati Kuu ya CHADEMA.
3. Tunaweza kukupatia mifano michache hapa, hasa ya hivi karibuni kabisa ili ujue namna ambavyo majukumu ya Kurugenzi
ya Kigaila inafanya kazi, ikizingatiwa umuhimu wake katika suala zima la kufua rasilimali watu.
-Hivi karibuni, Kurugenzi imemaliza mafunzo ya madiwani wote nchi nzima, takriban watu 450, pamoja na viongozi wa chama,
jumla wote karibu watu 1000.
-Hata ukiamua kufanya utafiti kidogo tu hapo ulipo kwa kutumia tu vidole vyako na ku-google, unaweza kuona namna ambavyo kupitia Kurugenzi hiyo ya Benson, Chama kilitoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wenyeviti na makatibu wa mikoa yote ya kichama nchi nzima.
Mafunzo hayo yalifanyika Kayanga, Karagwe. Ni mafunzo ambayo kwa kweli yataifanya M4C kuendeshwa kwa ufanisi ziadi kuanzia ngazi za chini kabisa mpaka mkoa, badala ya kutegemea ngazi ya taifa pekee.
Kurugenzi hiyo pia imekuwa ikitoa mafunzo kila viongozi wapya wanapochaguliwa. Mfano mzuri ni mafunzo ya viongozi wa ngazi ya kata na majimbo kwa mikoa ya Mtwar na Lindi.
Kwa hakika hii ni mifano michache tu inayoonesha namna ambavyo Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo, inavyotekeleza majukumu yake.
Makene
0688 595831/ 0752 691569
afhadhali umeelewa mkuu.karibu chadema,karibu tumaini jipya la nguvu ya umma!Kamanda Tumaini Makene, asante sana kwa ufafanuzi wako, hii imenifanya kuijua zaidi CHADEMA. Ninawatakia mafanikio katika harakati za kulikomboa taifa.
una uhakika na ulichokiandika?
Kuna mafunzo ya Kilimo, mafunzo ya ufundi, mafunzo ya mapishi...etc,. Wewe je neno mafunzo unalielewaje?
CHADEMA wana oganaizesheni ya mafunzo ambayo mkurugenzi wake ni Benson Kigaila. nachotaka kujua je haya ni mafunzo ya darasani ama mafunzo ya namna gani hasa?. ni hilo tu linaloniumiza kichwa. wanachadema naomba mnifahamishe.
Asanteni .
Mkuu Tumaini Makene kuna mwananchi anaomba ufafanuzi huku; tafadhali msaidieni. Najua yote yanapatikana ndani ya katiba ya chama ila kwa faida ya wengi humu tunaomba kaufafanuzi.
Mkuu Shomari
Kwanza kabisa, inaitwa Kurugenzi anayoongoza Kamanda Singo Masalamakali Kigaila Benson, inaitwa Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo.
Juu ya hoja yako;
1. Suala la mafunzo kwa CHADEMA si suala la kufuata tukio au matukio, limefafanuliwa wazi na vyema kabisa kwenye kanuni
za chama.
2. Kurugenzi inafuata programu maalum ya mafunzo iliyopitishwa na Kamati Kuu ya CHADEMA.
3. Tunaweza kukupatia mifano michache hapa, hasa ya hivi karibuni kabisa ili ujue namna ambavyo majukumu ya Kurugenzi
ya Kigaila inafanya kazi, ikizingatiwa umuhimu wake katika suala zima la kufua rasilimali watu.
-Hivi karibuni, Kurugenzi imemaliza mafunzo ya madiwani wote nchi nzima, takriban watu 450, pamoja na viongozi wa chama,
jumla wote karibu watu 1000.
-Hata ukiamua kufanya utafiti kidogo tu hapo ulipo kwa kutumia tu vidole vyako na ku-google, unaweza kuona namna ambavyo kupitia Kurugenzi hiyo ya Benson, Chama kilitoa mafunzo ya nadharia na vitendo kwa wenyeviti na makatibu wa mikoa yote ya kichama nchi nzima.
Mafunzo hayo yalifanyika Kayanga, Karagwe. Ni mafunzo ambayo kwa kweli yataifanya M4C kuendeshwa kwa ufanisi ziadi kuanzia ngazi za chini kabisa mpaka mkoa, badala ya kutegemea ngazi ya taifa pekee.
Kurugenzi hiyo pia imekuwa ikitoa mafunzo kila viongozi wapya wanapochaguliwa. Mfano mzuri ni mafunzo ya viongozi wa ngazi ya kata na majimbo kwa mikoa ya Mtwar na Lindi.
Kwa hakika hii ni mifano michache tu inayoonesha namna ambavyo Kurugenzi ya Oganaizesheni na Mafunzo, inavyotekeleza majukumu yake.
Makene
0688 595831/ 0752 691569