Jembe Jembe
JF-Expert Member
- Jun 9, 2016
- 749
- 1,797
Wakati Serikali na vyombo vya dola vikiendelea kuchunguza uhalali wa uwepo wa kampuni ya biashara za mtandao ya Q-NET inayodaiwa kuwatapeli wananchi mamilioni ya fedha,ofisi za kampuni hiyo ziliopo mikoa ya Arusha na Kilimanjaro zimefungwa na Wafanyakazi wake hawajulikani walipo.
Awali mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya aliibua utapeli wa kutisha unaofanywa na kampuni hiyo kwa kuwatapeli walimu ,wastaafu na wafanyabiashara wilayani himo ambapo Sabaya aliamuru kukamatwa na kuhojiwa na Wafanyakazi wa kampuni hiyo na vyombo vya dola.
Baada ya kukithiri kwa madai ya wananchi na kuongezeka kwa mijadala kwenye mitandao ya kijamii, kufuatia DC Sabaya kuweka wazi kilio cha wananchi wakidai kutapeliwa na kampuni hiyo mkoani Kilimanjaro, Jeshi la Polisi limeamua kuingilia kati.
Baadhi ya WANANCHI waliotapeliwa bado wanahaha kujua hatima ya fedha zao walizopanda ikiwemo kushinda wamekaa katika ofisi hizo ambazo zimefungwa wakiwasaka Wafanyakazi wa kampuni hiyo ya Q-NET ili warejeshewe fedha zao.
Baadhi ya wahanga wa kampuni hiyo wamempongeza DC Sabaya kwa ujasiri alioufanya kwa kuibua madudu yanayofanywa na kampuni ya Q-NET inayoogofya hapa nchini na kusaidia kunusuru WANANCHI wengine wasiendelee kutapeliwa.
Awali mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya aliibua utapeli wa kutisha unaofanywa na kampuni hiyo kwa kuwatapeli walimu ,wastaafu na wafanyabiashara wilayani himo ambapo Sabaya aliamuru kukamatwa na kuhojiwa na Wafanyakazi wa kampuni hiyo na vyombo vya dola.
Baada ya kukithiri kwa madai ya wananchi na kuongezeka kwa mijadala kwenye mitandao ya kijamii, kufuatia DC Sabaya kuweka wazi kilio cha wananchi wakidai kutapeliwa na kampuni hiyo mkoani Kilimanjaro, Jeshi la Polisi limeamua kuingilia kati.
Baadhi ya WANANCHI waliotapeliwa bado wanahaha kujua hatima ya fedha zao walizopanda ikiwemo kushinda wamekaa katika ofisi hizo ambazo zimefungwa wakiwasaka Wafanyakazi wa kampuni hiyo ya Q-NET ili warejeshewe fedha zao.
Baadhi ya wahanga wa kampuni hiyo wamempongeza DC Sabaya kwa ujasiri alioufanya kwa kuibua madudu yanayofanywa na kampuni ya Q-NET inayoogofya hapa nchini na kusaidia kunusuru WANANCHI wengine wasiendelee kutapeliwa.