kaka, ukiwatenganisha kama jamaa anavyosema, AG Hatabaki na kitu kabisa, kwasababu mtendaji mkuu wa ofisi ya mwanasheria mkuu ni DPP kwasababu shughuli zilizo nyingi hapo ni kuendesha mashitaka. ukimwondoa DPP, attorney general atabaki na division ya katiba na sheria, division ya mikataba, division ya mashauri ya madai...hapo division ya mashauri ya jinai anayoshikilia DPP itakuwa imenyofoka. hizo division zingine ukiondoa ya kuendesha mashitaka(dpp) ni watu wachache sana hata 500 sidhani kama wanafika ukijumuisha na makatibu muhtasi na wafagiaji. ofisi zote mikoani zinazoendesha mashauri ya madai ni kesi chache sana hivyo wanajikuta wote wanafanya kazi za DPP tu,...
hata hivyo, haitakuwa shida kwasababu kama kuna kesi ya madai, attorney general anacho kitengo cha madai na mikataba pale chenye mawakili wa serikali wanaozunguka nchi nzima kuendesha kesi za madai....nashauri watenganisha haraka ili kuwe na ufanisi, na wakitenganisha, arudishwe Feleshi ndiye alikuwa anaiweza hiyo ofisi na ndiye alikuwa amekubalika dunia nzima. alipoondoka nasikia aliondoka na kila kitu...wafadhili wakakimbia, misaada kwenye iyo ofisi ikakauka kwasababu watu waliona jembe limeondoka....hata kikwete alikuja kujilaumu baadaye kwa kuona amepotoshwa akatamani kumrudisha lakini ikawa ngumu.