Ofisi ya CAG Tanzania yashinda tuzo kubwa ya Kimataifa kwa ripoti bora ya 2019

Removers

Member
Nov 1, 2018
71
39
Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Tanzania imeshinda tuzo ya Kimataifa ya Ripoti Bora zaidi ya Hesabu za Serikali kwa mwaka 2019 kwa ukanda wa nchi za Afrika zenye Taasisi za Udhibiti na Ukaguzi zinazotumia Lugha ya Kiingereza (AFROSAI-E region).

Taarifa iliyotolewa na taasisi hiyo inayofadhiliwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Sweden, inasema kuwa ‘’tuna furaha ya kutangaza kuwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Tanzania ndiyo mshindi Tuzo ya Ripoti Bora zaidi ya Ukaguzi wa Hesabu kwa mwaka 2019 katika ukanda wa AFROSAI-E.

Hii ni mara ya nne kwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Tanzania kushinda tuzo hii tangu ilipoanzishwa mwaka 2008 na Ofisi ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali ya Sweden.

Ripoti hiyo yenye jina ‘’Management of Water Projects in Rural Areas’’ imejikita kuangalia sekta ambayo ina uhusiano wa karibu na afya ya jamii, hivyo imeangazia zaidi mtazamo wa wananchi, inasema taarifa hiyo.

Timu huru ya Kimataifa ya Mapitio iliamua kwa kauli moja kuhusu ripoti iliyoshinda, na nchi ambazo ripoti zake zilikuwa nzuri, zenye ubora na zimebuniwa na kutengenezwa vizuri. Inahusisha mnyororo mzima wa uwajibikaji kuanzia katika ngazi ya wilaya hadi ngazi za chini za utawala. Ripoti ya Tanzania iliwasilisha mahitimisho na mapendekezo ambayo ni ya kichambuzi na yanaongeza thamani na yametokana na msingi wa masuala yaliyoibuliwa.

Naye Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali nchini Tanzania, Bw. Charles Kachere amesema kuwa amefurahishwa sana kupokea tuzo hiyo kwa niaba ya Ofisi yake. ‘’Nina furaha sana kupokea tuzo hii kwa niaba ya ofisi yangu, na ninajivunia na timu nzima iliyoandaa ripoti iliyoshinda tuzo. Vilevile, ningependa kushukuru Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali wa Sweden kwa kuendelea kutuunga mkono kwa kipindi kirefu, ambayo imechangia kwenye kujengea uwezo wa ukaguzi kwa Ofisi ya Taifa ya Udhibiti na Ukaguzi wa Hesabu za Serikali Tanzania’’.

Jumla ya ripoti 10 ziliwasilishwa kutoka of Ethiopia, Ghana, Seychelles, Sierra Leone, South Africa, Sudan, na Tanzania kwa mwaka huu.

Katika hatua nyingine, Mkurugenzi Mtendaji wa AFROSAI-E, Meisie Nkau amepongeza Ofisi ya CAG Tanzania kwa ubora wa ripoti yake. Akizungumza wakati wakati wa kutangazwa kwa mshindi amesema kuwa ‘’Nina furaha kubwa kuwapongeza Ofisi ya Tanzania kwa mafanikio haya. Mmefanikiwa kwa mara nyingine! Pia ningependa kushukuru kwa mataifa yote kwa kuendelea kushiriki kwa kuwasilisha ripoti bora’’.
 
Ni sawa, mbona mimi nashinda chato na wengine wanashinda njaa?

Huku ndio kugawana majukumu sasa🤣🤣
 
Hongera Profesa Musa Assad kwa kujenga taasisi na sio mtuu mmoja mmojaaaa. Natumaini ripoti zingine zijazo tutapata tunzo zaidiiii kwa kuwa ulomkabidhi ofisi aliahidi kufanya vizuri zaidi.

Mungu ibariki Tanzania
 
Tanzania wins Prize for the best Performance Audit report of 2019

By Annerie Pretorius | 11th May 2020

We are delighted to announce that the National Audit Office of Tanzania is the winner of the Best Performance Audit Report Prize of 2019 for the AFROSAI-E region. This is the fourth win for SAI Tanzania since we jointly launched the prize in 2008, with the Swedish National Audit Office. The aim of the Prize is to benchmark good practices in performance audit and to highlight efforts made by performance auditors around the region.

The winning report “Management of Water Projects in Rural Areas” deals with a sector that is closely connected to public health, and therefore has a clear citizen perspective.

The international independent Review Team was unanimous in its decision on the winning report, and states that the audit report is well-motivated, of good quality and well designed. It covers the whole chain of responsibility, from the ministry to the local level of administration. The report presents conclusions and recommendations that are clearly analytical, add value and are based on an overarching integration of the findings.

“I am very happy to receive this prize on behalf of my office, and I am very proud of the team that has conducted the winning performance audit report. I would also like to thank the Swedish NAO for its longstanding support, that has contributed to developing the audit capacity in NAO Tanzania” Mr. Charles Edward Kichere, Controller and Auditor General of the National Audit Office of Tanzania

The SAIs of Ethiopia, Ghana, Seychelles, Sierra Leone, South Africa, Sudan, and Tanzania nominated a total of ten reports to this year’s competition.

It is encouraging to see the spread of topics and geographic coverage in the nominated reports, as it demonstrates that qualified performance audit work is conducted throughout the region, says Auditor General of Sweden, Helena Lindberg.

The audit team behind the winning report are Mr Victor Mapigano, Mr Andalason Hamba and Ms Esnath Henry Nicodem. As part of the prize, the team will visit the Swedish National Audit Office in Stockholm at a later date, to exchange knowledge and experiences with their Swedish colleagues.

“It is with immense pleasure, that I congratulate SAI Tanzania for this achievement. You have done it again! I would also like to thank all those SAIs that continue to participate in this initiative by consistently nominating reports for the prize. By sharing your reports with the region, others can learn from your good example and experiences. I applaud you all for your efforts to strengthen performance audit in your countries and in the region.” – Meisie Nkau, AFROSAI-E CEO

Capture.PNG
 
Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Tanzania imeshinda tuzo ya Kimataifa ya Ripoti Bora zaidi ya Hesabu za Serikali kwa mwaka 2019 kwa ukanda wa nchi za Afrika zenye Taasisi za Udhibiti na Ukaguzi zinazotumia Lugha ya Kiingereza (AFROSAI-E region).

Taarifa iliyotolewa na taasisi hiyo inayofadhiliwa na Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali wa Sweden, inasema kuwa ‘’tuna furaha ya kutangaza kuwa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali Tanzania ndiyo mshindi Tuzo ya Ripoti Bora zaidi ya Ukaguzi wa Hesabu kwa mwaka 2019 katika ukanda wa AFROSAI-E.
cc:Bia yetu,Troll JF, kabombe, stroke, Wakudadavuwa
 
Back
Top Bottom