Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
TAARIFA KWA UMMA
Hivi karibuni kumekuwa na taarifa iliyotolewa na baadhi ya vyombo vya habari na baadhi ya wabunge kuwa posho ya vikao vya bunge imeongezeka kutoka Sh 70,000/= hadi kufikia 200,000/=.
Suala la mabadiliko la bosho za vikao vya bunge lilijadiliwa katika mkutano wa wabunge November 08, 2011 walipoiomba serikali iangalie upya suala hili ili kuboresha. Hadi tunapotoa taarifa hii serikali haijatoa taarifa kama posho hizo zimeongezeka kutoka kiwango cha awali na kufikia laki mbili.
Tunasikitika na kushangaa sana kwa kauli hii kwani inajenga chuki baina ya wabunge na wananchi waliowapigia kura.
Posho inayotolewa kwa sasa ni ile iliyoainishwa kwenye waraka wa Rais wa October 25, 2010 ambayo iliridhia posho ya vikao kuwa 70,000/=
Kwa hiyo taarifa iliyotolewa siyo sahihi.
Imetolewa na
Dr. Thomas D. Kahililah
Katibu wa Bunge
Suala la mabadiliko la bosho za vikao vya bunge lilijadiliwa katika mkutano wa wabunge November 08, 2011 walipoiomba serikali iangalie upya suala hili ili kuboresha. Hadi tunapotoa taarifa hii serikali haijatoa taarifa kama posho hizo zimeongezeka kutoka kiwango cha awali na kufikia laki mbili.
Tunasikitika na kushangaa sana kwa kauli hii kwani inajenga chuki baina ya wabunge na wananchi waliowapigia kura.
Posho inayotolewa kwa sasa ni ile iliyoainishwa kwenye waraka wa Rais wa October 25, 2010 ambayo iliridhia posho ya vikao kuwa 70,000/=
Kwa hiyo taarifa iliyotolewa siyo sahihi.
Imetolewa na
Dr. Thomas D. Kahililah
Katibu wa Bunge
Bofya link ya kijani hapo chini habari hii ilivyoripotiwa na Gazeti la Mwananchi kupata mengi zaidi.
Bunge latoa tamko nyongeza ya posho