Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,820
- 4,573
KIONGOZI wa Chama cha Upinzani nchini Kenya, Raila Odinga amefichua kuwa bado hajajiandaa kujiondoa katika ulingo wa kisiasa na kwamba hatostaafu.
Raila mwenye umri wa miaka 78 alidokeza kujaribu bahati yake katika kiti cha urais kwa mara ya sita katika Uchaguzi Mkuu wa 2027.
"Siko tayari kuacha, na kwa hivyo mnapaswa kuwa tayari kuniunga mkono. Nilimsikia Ruto akisema kwamba ninaacha, na hivyo Kalonzo atachukua usukani, Kalonzo ni kitafunwa tu kwake," amesema Raila.
Akizungumza katika kisiwa cha Mfangano huko Homa Bay, Raila aliomba kuungwa mkono ili kuhakikisha muungano wa Azimio unaokabiliwa na kuzinduliwa upya, unasalia imara na kupata kiti cha juu.
Raila mwenye umri wa miaka 78 alidokeza kujaribu bahati yake katika kiti cha urais kwa mara ya sita katika Uchaguzi Mkuu wa 2027.
"Siko tayari kuacha, na kwa hivyo mnapaswa kuwa tayari kuniunga mkono. Nilimsikia Ruto akisema kwamba ninaacha, na hivyo Kalonzo atachukua usukani, Kalonzo ni kitafunwa tu kwake," amesema Raila.
Akizungumza katika kisiwa cha Mfangano huko Homa Bay, Raila aliomba kuungwa mkono ili kuhakikisha muungano wa Azimio unaokabiliwa na kuzinduliwa upya, unasalia imara na kupata kiti cha juu.