OCS Mikumi inabidi ujitathmini kabla hujafanyiwa tathmini na viongozi wako

Norton82

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
721
620
Tarehe 01 Oktoba 2019 , mlifanya mkutano na wanakijiji kata ya Malolo wilaya ya kilosa, na wanakijiji hao walikusanywa na Diwani wa kata ya Malolo na afisa mtendaji wa kata ya Malolo, zikaibuliwa tuhuma na mkulima mmoja kuwa ng'ombe za wafugaji zinakula kwenye mashamba ya wakulima, lakini cha ajabu zaidi hao waliowakusanyia watu muongee nao ndiyo umetoa amri wakae ndani,

Ndugu zao wakifika kituo cha polisi, polisi hawatoi ushirikiano, wanajifanya wako busy, na miongoni mwa wafugaji waliokamatwa wanasema waliotakiwa kukamatwa wameachwa wamekamatwa wasiostahili , lakini cha kusikitisha zaidi mkatoa madai ya kwamba kituo cha polisi mikumi kimejaa na wanatakiwa wapelekwe Kituo cha polisi K1Ruaha, lakini askari waaminifu, wamesema hapo kituoni nafasi bado ipo,

Jambo la kuzingatia fanya kazi kwa kufuata misingi ya kazi yako, vinginevyo dunia sasa hivi ni kama kijiji,usifikiri kwa kufanyia kazi katika maeneo ya pembeni ya nchi ndiyo mwanya wa kujifanyia mambo unavyoona wewe inafaa, hao wafugaji kama wana makosa wapelekeni mahakamani ila kama hawana makosa muwaachie kwa amani.

Na katika hili ifahamike hatuitaji migogoro ya wakulima na wafugaji ila kuonekane haki ikitendeka baina ya pande hizo mbili.

Ni mimi mwanakijiji mtiifu
 
Tarehe 01 Oktoba 2019 , mlifanya mkutano na wanakijiji kata ya Malolo wilaya ya kilosa, na wanakijiji hao walikusanywa na Diwani wa kata ya Malolo na afisa mtendaji wa kata ya Malolo, zikaibuliwa tuhuma na mkulima mmoja kuwa ng'ombe za wafugaji zinakula kwenye mashamba ya wakulima, lakini cha ajabu zaidi hao waliowakusanyia watu muongee nao ndiyo umetoa amri wakae ndani, ndugu zao wakifika kituo cha polisi, polisi hawatoi ushirikiano, wanajifanya wako busy, na miongoni mwa wafugaji waliokamatwa wanasema waliotakiwa kukamatwa wameachwa wamekamatwa wasiostahili , lakini cha kusikitisha zaidi mkatoa madai ya kwamba kituo cha polisi mikumi kimejaa na wanatakiwa wapelekwe Kituo cha polisi K1Ruaha, lakini askari waaminifu, wamesema hapo kituoni nafasi bado ipo, jambo la kuzingatia fanya kazi kwa kufuata misingi ya kazi yako, vinginevyo dunia sasa hivi ni kama kijiji,usifikiri kwa kufanyia kazi katika maeneo ya pembeni ya nchi ndiyo mwanya wa kujifanyia mambo unavyoona wewe inafaa, hao wafugaji kama wana makosa wapelekeni mahakamani ila kama hawana makosa muwaachie kwa amani.Na katika hili ifahamike hatuitaji migogoro ya wakulima na wafugaji ila kuonekane haki ikitendeka baina ya pande hizo mbili.
Ni mimi mwanakijiji mtiifu
Nilifikiri jnaongea jambo la maana pumbavu kabisa.Mnaua wanakijiji wazawa mchana kweupe na kulisha mifugo yenu mwenye mashamba yao halafu mnataka muangaliwe tu.Mlizoea kutoa rushwa sasa huyo ndata yeye ni mwendo wa Ibada tu ukiua ukidhurumu unakutendea haki hataki pesa haramu.Kuhamishiwa K1 bado anawatendea haki mahabusu ili wasirundikane mahabusu moja mkafa kwa kukosa hewa.Hawa wafugaji huko mkoani Morogoro wamekuwa tatizo kubwa hata ukimuona live analishia mifugo shambani kwako ukimwambia atoe anakuua au kukujeruhi vibaya sasa wanakijiji wamebuni mbinu nyepesi tu kwenye mimea yao wanaweka dawa za kimila tu kwenye mashamba mifugo ikila tu mimea ianakufa.Sasa kilio kimegeuka.Mwenyewe umeona huku ndiyo chimbo la kujificha kuongea huo uozo wako Napendekeza Huyo OCS apandishwe cheo kwa roho yake yenye haki na kusimamia sheria kagusa hata wasiogusika.IGP pandisha cheo huyo OCS makini anayekataa rushwa nono nono hata kwenye mazingira ya maficho.
 
Ugomvi wa wakulima na wafugaji haujawahi kuisha kama humu ndani na singo mamaz
 
Back
Top Bottom