Nyumba 5,600 kubomolewa Dar

Nyumba 5,600 kubomolewa Dar

Yawezekana watawala wetu wamefuata sheria, lakini hawakutumia busara na hekima. Nawatakia kila la kheri katika kazi yao nzuri ya kuwabomolea nyumba wananchi wao, nayo yaweza kuwa ni ubunifu.
Wakitumia sheria mnapiga kelelewakitumia hiyo busarapia mtapiga kelele
 
Say nyumba moja ina watu 7 hapo ni zaidi ya watu 35,000 bila makazi
 
Kwakweli watu wengi wataathirika jamani....sio mchezo
In fact kwa dar idadi hiyo ya nyumba inaweza kuwa sawa na kaya zaidi ya elfu 20 (kila nyumba kaya au familia zaidi ya 4) na watu zaidi ya elfu 70 (kila kaya ina zaidi ya wanafamilia wa4).
 
Haitii huruma kwani ni shida yao wenyewe kwa sababu hawa wote walishapewa notice ya kuhama miaka kibao iliyopita na hela wakalipwa lakini hawakuhama kutokana na srikali ya kipindi kile kuwa bize na massage na safari za hajabu nje ya nchi.

ok, walipewa notis miaka 3 iliyopita, hivi kabla ya kuja wakatoa siku 3 watakua wameokoa mali nyingi kiasi gani na wao watakua wamepata hasara kiasi gani kwa kuwakumbusha? jibu ni kua hasara ya kuwakumbusha na hasara ya kubomoa ghafla hasara ya kubomoa ghafla ndio kubwa
 
ukitafakari kwa busara hapa, utaona hao waliokua na jukumu la kusimamia mipango miji walikua hawafanyi kazi yao au walihongwa, nyumba 5,600 kubomolewa is not good for anyone,kwa serikali inaonekana inanyanyasa na kwa wananchi ni hasara kubwa sana, hadi nyumba nyingi kiasi hiki zijengwe walikua wapi?

Kwani zinabomolewa na nani ndugu....!
Si ni nemc?
Wale watu wa mazingira? Maeneo hayo ni hatarishi, serekele haiwezi kuhudumia watu wanojenga na kupata maafa yanayozuilika ndugu....!!!!

Kujenga raisi, mengine huyajui .....!!! Kukiwa na mafuriko mtu ana hamia juu ya paa la nyumba au kusubiri siku kadhaa ili maji yakauke
 
wasiishie hapo bali waende mbali zaidi kuziwajibisha mamlaka zilizofanya uzembe huu wa kuwasababishia wananchi adha isiyokifani.

Nyumba 5,600 Dar es Salaam zipo katika mpango wa kubomolewa katika mpango wa bomoabomoa unaoendelea sasa hivi.

Mpaka sasa nyumba zilizokwisha bomolewa ni nyumba 200 ambayo ni sawa na 3% ya lengo.
 
ok, walipewa notis miaka 3 iliyopita, hivi kabla ya kuja wakatoa siku 3 watakua wameokoa mali nyingi kiasi gani na wao watakua wamepata hasara kiasi gani kwa kuwakumbusha? jibu ni kua hasara ya kuwakumbusha na hasara ya kubomoa ghafla hasara ya kubomoa ghafla ndio kubwa


Hivi unaelewa unachosema? Hawa watu walishapewa hela zao za kutoka ile sehemu, kwa kifupi walisha malizana na serikali ilichobaki tu ni kwa serikali kubomoa ile sehemu. Mbona wenzao walishaondoka siku nyingi na hawana tena habari za kurudi mabondeni? Nikuulize, wewe unaniuzia nyumba na mimi nakupa notisi ya kuondoka ikifika tarehe fulani, siku imefika nakuja kubomoa nyumba yangu uliyoniuzia ili nikarabati sehemu/kiwanja changu, je....wewe una haki ya kunidai tena ikiwa umeishi hiyo sehemu kwa kujuwa kuwa siku yeyote utabomolewa? Cha kushangaza, wengine waliolipwa na serikali walirudi pale na kujenga upya, si ujinga huu?
 
Inaumiza sana lakini inabidi iwe hivyo ili mambo yaende mfano vingunguti kule watu wamejenga mpaka mtoni kabisa yani maji hayajui ata yatililike wapi. Sasa mtu kama huyu unaanzaje kutumia busara maana kwa akili ya kawaida serikali ata iwe corrupt kiasi gani aiwezi kutoa kibali cha ujenzi kwenye mto bora ata ingekuwa pembeni ya mto. Jk aliendesha nchi kwa busara kuliko sheria ndio mkafanya mnavyojiskia sasa hii ni awamu ya kazi tu na sheria zinafatwa.
 
nyie simliikataa ccm, uwezi ukaikataa ccm ukabaki salama hivi hivi haiwezekani.
Sasa tuisome namba.
 
Pia hata hivyo watanzania wenzangu tuna matatizo ya kufanya mazoea kuwa sheria, na siku akitokea mtu atakaeamua kufuata sheria basi nalo linakuwa tatizo,
Wa tanzania tumezoea vibaya tujifunze kuzingatia sheria licha ya kwamba wakati mwingine inauma. Nafuta usemi wa mwanzo kwamba uwezi ukaikataa ccm ukabaki salama,
Naweka lugha sawa unaweza kuikataa ccm na bado ukabaki salama, iwapo tuu utafuata sheria na taratibu zilizopo.
Nawakilisha.
 
nyumba 5,600 dar es salaam zipo katika mpango wa kubomolewa katika mpango wa bomoabomoa unaoendelea sasa hivi.

Mpaka sasa nyumba zilizokwisha bomolewa ni nyumba 200 ambayo ni sawa na 3% ya lengo.

mkajifanya mnapenda chadema nyinyi, its pay back now. Vunjaaa zote tusipolizika mtachapwa viboko woteeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

hapa ccm tu baaaassss pumbavu
 
Hivi hayo maeneo walikuwa hawajawapa hati zile za makazi???
 
mkajifanya mnapenda chadema nyinyi, its pay back now. Vunjaaa zote tusipolizika mtachapwa viboko woteeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee

hapa ccm tu baaaassss pumbavu

haihusiani na kuikataa ccm bali mipango miji, hata mwanza hili litafika
 
Acha zivunjwe tu, hela wamekula halafu wanaendelea kuishi kwenye hizo nyumba. Sheria lazima ifatwe ili iwe mfano kwa wengine. Wewe unapewa notice miaka halafu siku wanakuja wazee wa kazi unasema sijatoa vitu vyangu. Ulikua wapi miaka yote hiyo?

Kuna vijana wa CDM wanataka kuligeuza hili kuwa ni la kisiasa lakini hawata fanikiwa. Miji lazima ikae sawa, vifo vya mabongeni ni basi sasa.
 
Kwahiyo unatenda kosa,ukiona huzuiwi unaendelea?

Hivi Na Zile Office Za DARTS Pale Jangwani Jirani Na Kajima, Magodauni Yaliopo Bonde La Msimbazi Tokea SUKITA Ya CCM Hadi Mandera Road Na Matumbi Na Buguruni Ally Hamza!! Yatuvunjwa Au Watayaacha Tu!? Huku Wakibomoa Vibanda Vya Makabwela Tu!!!!!?? Mi Nasubiria Kuona Hilo, Hapo Ndio Nitawapongeza NEMC, JIJI Na Wakurugenzi Kwa KAZI Nzuri!! Lkn Wakiyaruka Hayo Magodauni, Magereji, Mayadi Na Maofisi!!! Sitaweza Kuikubali Hiyo Operesheni Yao!!! Nasubiria Kuona!!!

Natamani siku moja Serikali wabomoe na eneo hili kwani hawa Wazungu wamejenga kituo na ofisi za mabasi ya mwendo kasi katikati ya njia ya maji pale Jangwani. Na serikali inawaangalia tu wanaendelea kujenga na majuzi Waziri Mkuu ameendaa na yeye kuwaangalia tu wakiendelea kujenga!!!!!.

Lazima tutende haki, tubomoe na hapa:-



Mafuriko Jangwani.JPG


Mafuriko Jangwani 4.jpg


Mafuriko Jangwani 3.jpg


Mafuriko jangwani 6.jpg


Mafuriko Jangwani 5.jpg

Tuangalie na kati kati ya jiji maeneo karibu na shule ya sekondari ya Tambaza - barabara ya Umoja wa Mataifa, mvua zikinyesha kunavyokuwa:-


Mafuriko DSM 1.jpg


Ukifuatilia kwa makini na kutenda haki, inabidi DSM watu wote wahamishwe kwani ni maeneo hatarishi mvua kidogo tu mafuriko, hadi Posta ambako ni karibu na IKULU mvua kidogo kunajaa maji hakufai.

TUTENDE HAKI TUWAHAMISHE WOTe, DSM NI ENEO HATARISHI KWA UJUMLA. HAKUUNA ENEO SALAMA DSm



MIZAMBWA
INANIUMA SANa!!!
 
Fateni sheria hiyo huruma huruma ndo imetufuikisha hapa, kama umejenga hazard area unataka huruma ya nn, watu wanatoka mikoani wanakua wastaarabu wameacha maeneo ya wazi wapumikie ww kwa kuwa umetoka mkoani hujui maana ya OPEN SPACE unajenga nyumba na kama ukiona haitoshi unaenda kwa wale wala rushwa wa manispaa unapewa kibari fake na mtendaji wa mtaa una mpa rushwa kidogo unajenga una tuzibia hewa safi na upepo then leo mji unasafishwa unamkuja na hoja mfu hapa eti waonewe huruma ipi hiyo wao mbona hawakutoenea huruma kutukinga na hewa safi na sehemu za kupumzika cc na faamilia zetu , hizo nyuma 5600 ni nn au zina thamani gani kama zimejengwa sehemu sio sahihi. ngoja watoke watafute sehemu sahihi
 
Back
Top Bottom