Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO -- 09*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Hakunijibu. Akanitazama na macho yake kama ya paka kisha akaweka kikaratasi mezani na kwenda zake. "Yani mwanamke huyu ana matatizo kweli!" Nikalalama nikiokota kile kikaratasi.
Niliposoma nikakutana na ujumbe, "NITAFUTE" kisha chini yake kuna namba za simu na anwani ya eneo.
ENDELEA
Nilitaka kumwita Jolene nimuulize kuhusu huo ujumbe ila nikaona si staha. Kwanza kwa namna nilivyomuona ni kama vile amechoshwa, lakini zaidi ya hapo, anaweza akawa hana majibu ninayotaka. Nikafikiri kidogo kisha nikanyanyua simu yangu na kupiga simu ile iliyoandikwa karatasini.
Ikaita mara mbili na kupokelewa. Kabla sijanena, nikaulizwa, "Marshall?" Sauti ilikuwa 'moderate', si nzito wa nyepesi. Ila ndani yake ilikuwa na mkazo.
"Ndio, ni mimi. Wewe ni--"
"Fanya tuonane," sauti ikanikatisha. "Fuata anwani iliyoandika hapo, fika." Kabla sijanema tena, simu ikakatwa. Hapo nikabakia na maswali. Ni nani huyu mwenye kuniamuru kiasi hiki?
Niliweka simu yangu mezani nikiwaza. Sikutaka kwenda huko. Lakini pia kwanini nisiende? Huwezi jua ... ila nitabainishaje kuwa si mtu mbaya? ... kapata wapi namba yangu ya simu?
Niliona sasa nina haja ya kwenda kuonana na Jolene kwa maswali haya, lakini sikunyanyuka ujumbe ukaingia kwenye simu yangu, "nina jambo la kukuambia kuhusu Raisi!" Nilipotazama namba, ilikuwa ni ileile niliyotoka kuwasiliana nayo hapo awali.
Nikanyanyuka na kuweka koti begani, nikatoka ofisini. Kurusha macho kumtafuta Jolene, sikumwona. Sikujibughudhi, nikaelekea nje na kujipaki kwenye gari langu kisha nikatimka kwenda huko kulikoelekezwa kwenye anwani. Kimahesabu haikuwa mbali sana na mahali pangu pa kazi, kama vile kilomita kumi tu.
Nikiwa barabarani, nikapata wazo la kumshirikisha Daniele kuhusu hili. Kiutaratibu hii ilikuwa ni kazi ya FBI agent, yaani Daniele, ila kwasababu nalipokea wito, sikuona haja ya kuuvuka.
Nikanyanyua simu na kumpigia. Kwa umbali, toka kule Washington DC mpaka hapa Langley, Virginia, ni maili mia moja sabini na tisa. Kwa mujibu wa taarifa za GPS waweza kutumia masaa matatu kasoro kufika hapa endapo ukitumia usafiri wa gari, kama ndege ni dakika arobaini tu, ndiyo maana haiwii ugumu sana kuonana na Daniele, huko Washington DC.
Simu iliita kidogo akapokea. Nikamsihi aje huku mikimwelekeza eneo na sababu. Nikahisi kabisa amejawa na hamu. Habari hiyo ilimpa msukumo uliomfanya upesi aniambie, "nakuja!" Kisha akakata simu.
Nilifanya hivyo si tu kwasababu ya utaratibu, la hasha, bali pia usalama wangu na kesi ile mezani. Endapo basi litakapotokea lolote lile, kuwapo na mtu atakayeweza kutoa taarifa nyuma yangu.
Basi nikaendesha baada ya hapo, kwa kama dakika kadhaa tu, nikawa nimefika kwenye nyumba elekezi. Ilikuwa ni nyumba ya ukubwa wa wastani, mbele yake kukiwa na bustani ndogo ya majani na maua.
Kabla sijashuka na kwenda, nikaikagua kwa macho ya wepesi. Nilipojiridhisha, nikatoka garini na kugonga mlango mara mbili. Kidogo ukafunguliwa na mtoto mdogo wa kike, makadirio ya kama miaka nane, tisa ama kumi hivi. Akanitazama kwa kunikagua.
"Hey, upo na yeyote ndani?" Nikamuuliza. Hakunijibu. Akaendelea kunitazama na kisha akaufungua mlango kwa upana. Nikazama ndani. Hapo nikiwa nimejikamilisha kwa kubebelea bunduki yangu ndogo ndani ya koti kwa dharura ya ulinzi.
Nikaketi sebuleni. Yule mtoto akaenda chumbani, pasipo kuniongelesha, na punde akarejea akiwa na mwanaume mwenye makamo ya umri wa miaka hamsini hivi kama sijakosea.
Mrefu na mwenye mwili mpana. Uso wake kama mstatili na kidevu chake ni pacha. Akanitazama kwanza kisha akajongea na kuketi.
"Anthony Marshall?"
"Ndio, ni mimi."
"Karibu. Naitwa O'neil," akanipatia mkono.
"Nashukuru kukufahamu bwana O'neil. Nimeitikia wito wako."
Kabla hajaendelea akarusha macho yake dirishani na kisha akaniuliza, "una uhakika umekuja peke yako?"
"Nadhani ..."
"Inabidi uwe na uhakika."
"Sijaangaza kama kuna mtu ananifuata. Hukuniambia hilo hapo awali."
"Yah! Nilifanya makosa. Hapa unatakiwa kuja mwenyewe, Marshall." Alisema hayo akiwa ananitazama kwa umakini sana kana kwamba mtu anayecheza mchezo wa 'chess'. "Sitaki mtu yeyote aanze kunifuatafuata. Nina mjukuu wa kumtazama. Na maisha yangu napenda yakiwa yangu binafsi."
Nikatulia na kumuuliza, "Ulitoa wapi mawasiliano yangu?"
"Kutoka kwa mkuu wako," akanijibu kwa kujiamini kisha akasema, "sikia Marshall, unaweza ukawa haunijui, ila mimi ni mtu ambaye nimetumikia taifa kwa miongo mingi. Inaweza ikawa haina haja sana ya kusema hivyo, ila lililo kuu ni kwamba mimi ni rafiki wa mtu huyo aliyepotea. Huyo ambaye unamtafuta kama nipo sahihi."
Nikanyamaza kimya nimsikize.
"Pengine naweza nikawa nahusika na upoteaji wa Raisi. Sasa nalijua na kujilaumu sana kwa hilo. Kama ningelichukua hatua mapema, huenda hivi sasa ningekuwa naye hapa badala yako. Najuta sana..."
Akanyamaza kidogo. Bado sikuongea. Nilimpa nafasi aendelee kujieleza pasipo kuhukumu kwa wepesi ama kuingilia alimradi alikuwa ameniita kunieleza jambo.
"Siku mbili kabla ya Raisi hajasafiri, nilionana naye. Hakuwa na muda wa kukaa na mimi sana kwani alikuwa ametingwa na kuna mahali anaenda. Ilikuwa ni upesi tu, na hata alipokuja hapa, hakuwa akiongozana na watu wengi kama mjuavyo, bali na watu wanne tu ambao walikuwa wamevalia suti nyeusi.
Alifika na ndani ya dakika akawa ameondoka! Mkononi mwangu aliniachia ujumbe huu," akaingiza mkono mfukoni na kutoa kipande kidogo cha karatasi ngumu nyeupe, akanikabidhi.
Nilipokisoma kilikuwa na ujumbe ulioandikwa kwa kalamu nyeusi ukisema, "NIPO SHIDANI." Nikamtazama yule mwanaume mwenyeji wangu, yeye akaendelea kunena.
"Sikupata muda wa kumuuliza ni shida gani hiyo ... kama unavyojua, si rahisi kuwasiliana na Raisi. Huwa ni mpaka yeye anitafute. Mara ya mwisho alipon'tafuta, ikawa ni siku yake ya kusafiri. Alimtuma mtu mmoja ambaye hakunieleza jina, na mtu huyo akaja kunifikishia ujumbe mwingine."
Akaweka kituo alafu akatoa tena karatasi toka kwenye mfuko wa pili. Mara hii huu ujumbe alikuwa ameuandika mwenyewe kwa mwandiko wake akiwa amenakili ujumbe aliopewa na mtu huyo.
"MUNICH, 2345," ujumbe ulisomeka hivyo. Nilipomuuliza maana yake, akaniambia hajui. Na hata huyo mtu aliyemletea, hakumwona tena tangu hapo.
"Unaweza ukamtambua mtu huyo ukimwona?"
Akanitikisia kichwa. "Hata picha zake ninazo."
"Naomba nizione."
Akageuza uso wake na kumtazama yule binti aliyenifungulia mlango. Akamtikisia kichwa kwa ishara na binti huyo akaenda chumbani. Kidogo, akarejea na picha mkononi, akanikabidhi.
Nikazitazama picha hizo. Nikagundua zilikuwa zimetolewa kwenye CCTV camera. Hazikuwa na ubora mkubwa ila angalau ziliweza kutambulika.
"Ni ajenti wa Secret service," akaniambia bwana yule. Nikazihifadhi picha hizo na kumuuliza, "sasa kwanini wahofia na kuishi hivi kama swala?"
"Nishakuambia mwanzoni," akanijibu. "Sitaki kuharibu maisha yangu. Hata wewe nimekutafuta kwasababu nahisi rafiki yangu atakuwa anahitaji msaada huko aliko!"
"Wapi?"
"Sijui! Na ndiyo maana nikafanya utaratibu wa kukutafuta. Huenda taarifa zangu zikakusaidia! ... na kwa usalama wangu, sitaonana na wewe tena baada ya hapa."
"Vipi kama nikihitaji taarifa nyingine toka kwako?"
"Sina taarifa ya zaidi na hiyo, Marshall. Kama nikiipata, basi nitakutafuta kama nilivyofanya leo. Kwani ulijua kama kuna mtu kama mimi?"
Basi nikamuaga na kwenda zangu, kichwani nikiwa nimepanga kumtafuta ajenti yule wa Secret Service na kisha, kama itawezekana, maana ya ujumbe ule wa MUNICH.
Nilipozama ndani ya gari na kuendesha kidogo, Daniele akanipigia. Nikapokea na kumwelekeza wapi tukutane. Ndani ya muda mfupi tukawa ndani ya gari langu. Nikamweleza yale niliyoyapata kwa mwanaume yule.
Maelezo hayo yakamfanya atamani sana kumwona yule bwana O'neil. Akanisihi huenda akawa anamfahamu mtu huyo na hivyo basi nimpeleke akahakikishe. Japo nilimwambia bwana huyo hatapendezwa na hilo, hakunisikia. Sikuwa na namna bali kumpeleka.
Tukachukua kama robo saa kufika. Nikagonga mlango na kuita. Kimya. Nikagonga tena na kuita kwanguvu, bado kimya! Kidogo mbeleni tukagundua kuwa bwana huyo hakuwapo tena hapo.
Tulivunja mlango na kusaka. Hakukuwa na kitu.

**
 
*NYUMA YAKO -- 10*

*Simulizi za series*



ILIPOISHIA

Tukachukua kama robo saa kufika. Nikagonga mlango na kuita. Kimya. Nikagonga tena na kuita kwanguvu, bado kimya! Kidogo mbeleni tukagundua kuwa bwana huyo hakuwapo tena hapo.

Tulivunja mlango na kusaka. Hakukuwa na kitu.

ENDELEA

“Atakuwa ametoroka,” akasema Daniele.

“hapana,” nikakataa. “sidhani kama huku ni kutoroka bali kujiepusha. Kama nilivyokuambia hapo awali, hakutaka haya mambo?”

“Kwani ni nini anachoficha?” Daniele akauliza akinishikia kiuno.

“Anaficha uhai na usalama wake,” nikamjibu na kisha nikatembea kuelekea gari. Naye Daniele akanifuata. Alipoingia tukajadili maswala kadhaa na kunifunza kuwa “Secret Service” hawakuwa wakihusika na upelelezi wa swala hili la upotevu wa Raisi.

“Kwa sababu za kiuwajibikaji, hawakuhusishwa ili kutoa mwanya wa mkono wa ziada kuwapeleleza hata wao endapo kutakuwa na mahusiano yoyote yale,” Daniele alisema akiwa anatazama mbele kana kwamba gari lipo kwenye mwendo.

Kisha akanitazama na kuniambia kiudadisi, “tunaweza kwenda Washington?” Sikujibu akaongezea, “inabidi tukatafute taarifa za huyo ajenti wa Secret Service ambaye akimletea ujumbe huyo mzee!”

Secret Service ni taasisi ya kiintelijensia inayohusika na ulinzi wa Raisi, Makamu wa Raisi na familia zao kwa ujumla. Wao ni chombo shurutishi cha kisheria kama ilivyo kwa FBI japo majukumu hutofautiana. Kwa ufupi taasisi hiyo huitwa USSS.

“Ni sawa,” nikamjibu Daniele. Niliona wazo lake linapendeza. Inawezekana kumpata ajenti huyo wa Secret Service ikawa ni hatua ya muhimu kwenye zoezi letu. Basi tukaenda huko kwa kutumia ndege. Tulipowasili, tukanyookea moja kwa moja kwenye makao makuu ya United States Secret Service (USSS). Huko tukakutana na Director, bwana Owen Allen, mwanaume mwembamba mwenye masikio mapana, macho madogo na lips nyembamba. Tukamweleza shida yetu.

Akiwa ameshikilia picha ya mtu tumtakaye, akasema, “huyu alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa zamu ya kumlinda Raisi.” Kisha akaminya lips na kufinya macho. “ila siku ambayo Raisi alipotea, hakuwa zamu. Hakuambatana naye.”

“Sasa yupo wapi?” akauliza Daniele akimtazama Director kwa umakini.

“Amefariki,” Director akajibu kisha akatupatia picha tatu toka kwenye droo yake. Zilikuwa ni picha za jengo linaloungua kuelekea majivuni.

“Tunaamini alifia humo. Mwili wake ulipatikana ukiwa umejeruhiwa sana, ngumu kutambulika. Hatukuwa na namnna zaidi ya kuufanyia taratibu za kuuzika.”

“Na vipi kuhusu familia yake?” nikamuuliza. “hana mke wala watoto?”

“Hakuwa na mtoto. Alikuwa anaishi na mwanamke ambaye aliachana naye muda mrefu kidogo kabla ya ajali hiyo kutokea.”

“Una picha ya mwanamke huyo?”

“Hapana.”

“Kuna habari yoyote ambayo aliwahi kufikisha kuu ya usalama wa Raisi?”

“Hamna habari ya kushtua. Zilikuwa ni habari za kawaida kutokana tu na majukumu yake.”

“Nino chanzo cha ajali yake hiyo? Mmechunguza mkajua?”

“Kwa mujibu wa wataalamu, ni ajali ya gesi. Bwana huyo alikuwa akitumia gesi kupikia.”

“Kabla ya ajali hiyo, hakuna dalili au mabadiliko yoyote ambayo bwana huyo aliyaonyesha?”

Director akabinua mdomo na kutikisa kichwa. Akaongezea, “alikuwa ni mfanyakazi mzuri sana. Sidhani kama anastahili kutiliwa shaka.”

“Vipi kuhusu bwana ---” nikasita. Niliona si stara kuntambulisha bwana O’neil. Kwa namna hiyo niliona ni kheri nikanyamaza kama ambavyo yeye alivyokuwa anahitaji. Faragha ya maisha yake.

Basi tukaaga na kwenda zetu.



***



Saa tatu usiku, Mgahawa wa Lemaire, Virginia.



Mezani nilikuwa na Jack Pyong na mchumba wake, Violette. Tulifika hapo muda si mrefu na hata bado hatukuwa tumeagiza chochote toka kwa mhudumu. Wakati Jack anaangaza macho yake, nikamuuliza, “kwanini mgahawa huu, Jack?”

“mzuri!” akanijibu kifupi na kisha akaniuliza, “kwani kuna tatizo bwana Tony?”

“Hapana, ila ni kama vile hamna mgahawa mwingine ndani ya jiji hili.”

“Tony, hapa kakuita nani?”

“Wewe!”

“Na mimi ndiye ntalipia bills, shida yako nini?”

“Kwani nilikuomba uniite?”

“Sasa mbona ukaja?”

Kabla sijajibu, jibu ambalo natumai lingemkera, mhudumu akawa amefika hapo. Mdada mrembo mwenye tabasamu usoni.

“Naweza kuwasaidia?”

Tukamuagiza chakula, nami angalau kinyongo changu kifuani dhidi ya Jack kikawa kimekauka.

“Nadhani sasa hivi ungekuwa kwenye kitanda chako cha baridi umejikunyata. Si ndiyo Tony?” Jack akan’chokoza. Sikutaka kumjibu. Chakula kilikuwa kitamu kuliko maneno yake ya kijinga. Huenda hii ndo’ ikawa sababu yake kupendelea mgahawa huu, chakula cha moto na kitamu.

“Maisha ya upweke mabaya sana Jack,” akaendelea kuhororoja. “inabidi ufanye namna uwe na pa kupumzikia!” hapa Violette akamwonya juu ya mdomo wake lakini nikijua ni kazi bure maana Jack hatosikia.

Uzuri sikujali, na kulikuwa na sababu nyingine ya kunifanya nimpuuzie. Chakula. Niliujaza mdomo wangu chakula, nikatafuna nikitazama wateja wengine waliofika hapo.

Sikukaa muda mrefu, nikasikia sauti ya mtu akikokota viatu vyake. Kabla sijageuka, sauti hiyo ikakoma na mara kutazama, mtu akaniangukia, nikawahi kumdaka! Naye Jack Pyong akainama kama aliyetaka kumdaka. Kumtazama mtu huyo, nikamkumbuka! Alikuwa ni yule mwanamke niliyekutana naye kule Hong Kong!

Nikiwa katika mshangao huo, mara nikashuhudia Jack Pyong akipiga magoti na kufunua kidude kidogo cha rangi ya zambarau. Akiwa amemtazama Violette, akamwambia, “Utakubali kuwa mke wangu?”

Violette alikuwa amepigwa na duwaa. Hakutegemea kile kitu. Hata mimi sikutaraji kabisa. Na hapa ndipo nilipofahamu ya kuwa mwanamke yule ambaye tulikutana naye Hong Kong, ndiye aliyeleta pete ile. Kwahiyo, Jack alikuwa ametufanyia surprise watu wawili kwa mpigo!

Akakumbatiana na Violette na sisi, mimi na yule mwanamke mgeni, tukaishia kupiga makofi na kuwapongeza.

“Jack, uliwezaje kuliweka siri hili hata kwangu?”

Akatabasamu. “Nilipanga kukwambia, ila niliona nawe uwe ni miongoni mwa watakaoshangazwa. Vipi? Nadhani umependa wazo langu sio?”

Nikamtazama yule mwanamke kando yangu. Alikuwa ndiye yuleyule. Macho makubwa, nywele nyeusi. Hakika alikuwa anavutia. Na kwa namna alivyokuwa ananitazama alinifanya nihisi maungio yangu ya mwili hayafanyi kazi.

“Umekuja kufanya nini Marekani?” nikamuuliza. Akan’tazama na kutabasamu.

“Kutalii.”

“Kweli?”

“Ndio! Kwani haiwezekani? Au Marekani si sehemu ya kutalii kama Hong Kong?”

“Ni majuzi tu umetoka Hong Kong, itawezekanaje uwe huku kutalii?”

Akamtazama mhudumu aliyekuwa amefika hapo, akamwagiza kinywaji na kisha akan’tazama kuendeleza soga.

“Nimekuja kusoma, Tony.”

“Na unajua jina langu!”

Akacheka kidogo akifunika kinywa chake. “kwanini nisijue. Uliniambia mwenyewe? .. aah sasa naamini siku ile ilikuwa ni pombe ipo kichwani sio?”

“Siku gani?”

“Kule Hong Kong kwenye party!”

“Tulitambushana mimi na wewe?”

“Maskini Tony. Ilikuwa ni mara yako ya kwanza kunywa?”

“Yah! Kama si huyu fala, nisingegusa kilevi!” nikasema nikimtazama Jack Pyong.

“Kwahiyo haukumbuki hata kama ulinibusu na kunikumbatia?”

“Nilifanya hivyo?” Nikauliza nikikodoa. Akacheka tena akifumba mdomo wake kwa kiganja. “Kipi sasa wakumbuka Tony?”

“Nadhani ni sura yako tu. Hiko kitu hakikutoka kichwani.”

“Kweli, naona.” Alisema hivyo kisha akanitazama akiwa kimya. Kwa muda nikahangaika kutafuta kauli yangu mdomoni. Na kama vile mtu aliyefahamu ‘struggle’ ninayopitia akatabasamu kwambali kisha akaniuliza, “vipi Tony, kuna kitu unataka sema?”

Kabla sijasema jambo, mhudumu akampatia juisi na mrija. Ilikuwa ni juisi baridi ya tufaha. Hapo akanywa mafundo kadhaa kabla hatujaendelea na maongezi yetu machache. Alijitambulisha kwa jina la Kelly na kama alivyoniambia hapo awali, yeye alikuwapo hapo kwa ajili ya kusoma, chuo kikuu cha Harvard kitivo cha sheria.

Nilipotaka kufahamu juu ya wapi alipotokea, akanisihi nisiwe na haraka. Kila kitu kitajulikana taratibu.

“Maisha yangu yapo ‘simple’ and ‘straight’, Tony. Utajua kila kitu ndani ya muda mfupi. Lakini ukiwa ‘interested’.”

Baada ya hapo, Jack Pyong na Violette hawakukaa sana, wakatuaga wanaenda zao. Jack akanikonyeza akiwa anaenda zake.

“Sasa,” Kelly akachokoza mada. “Wewe hauondoki? Unalala hapa nini?”

Nikatabasamu kisha nikatazama saa yangu. Yalikuwa ni majira ya saa tano sasa usiku. Kweli muda ulikuwa umeenda. Nilimtazama Kelly na kumuuliza juu ya makazi yake, akaniambia kuwa amefikia kwenye apartment moja ndani ya Virginia.

“Kwanini Virginia na si Massachusetts huko karibu na chuo cha Harvard?”

Akatabasamu pasipo kuonyesha meno. Mashavu yake yalituna na macho yake kujifinya.

“Kwasababu ndo’ sehemu ambapo nina mwenyeji!”

“Mwenyeji? Hapa Virginia?”

“Ndio.”

“Wapi huko?”

Kabla hajajibu akaingiza mrija mdomoni mwake na kufyonza juisi.



**
 
Ngoma ipo poa sana hii
*NYUMA YAKO -- 10*

*Simulizi za series*



ILIPOISHIA

Tukachukua kama robo saa kufika. Nikagonga mlango na kuita. Kimya. Nikagonga tena na kuita kwanguvu, bado kimya! Kidogo mbeleni tukagundua kuwa bwana huyo hakuwapo tena hapo.

Tulivunja mlango na kusaka. Hakukuwa na kitu.

ENDELEA

“Atakuwa ametoroka,” akasema Daniele.

“hapana,” nikakataa. “sidhani kama huku ni kutoroka bali kujiepusha. Kama nilivyokuambia hapo awali, hakutaka haya mambo?”

“Kwani ni nini anachoficha?” Daniele akauliza akinishikia kiuno.

“Anaficha uhai na usalama wake,” nikamjibu na kisha nikatembea kuelekea gari. Naye Daniele akanifuata. Alipoingia tukajadili maswala kadhaa na kunifunza kuwa “Secret Service” hawakuwa wakihusika na upelelezi wa swala hili la upotevu wa Raisi.

“Kwa sababu za kiuwajibikaji, hawakuhusishwa ili kutoa mwanya wa mkono wa ziada kuwapeleleza hata wao endapo kutakuwa na mahusiano yoyote yale,” Daniele alisema akiwa anatazama mbele kana kwamba gari lipo kwenye mwendo.

Kisha akanitazama na kuniambia kiudadisi, “tunaweza kwenda Washington?” Sikujibu akaongezea, “inabidi tukatafute taarifa za huyo ajenti wa Secret Service ambaye akimletea ujumbe huyo mzee!”

Secret Service ni taasisi ya kiintelijensia inayohusika na ulinzi wa Raisi, Makamu wa Raisi na familia zao kwa ujumla. Wao ni chombo shurutishi cha kisheria kama ilivyo kwa FBI japo majukumu hutofautiana. Kwa ufupi taasisi hiyo huitwa USSS.

“Ni sawa,” nikamjibu Daniele. Niliona wazo lake linapendeza. Inawezekana kumpata ajenti huyo wa Secret Service ikawa ni hatua ya muhimu kwenye zoezi letu. Basi tukaenda huko kwa kutumia ndege. Tulipowasili, tukanyookea moja kwa moja kwenye makao makuu ya United States Secret Service (USSS). Huko tukakutana na Director, bwana Owen Allen, mwanaume mwembamba mwenye masikio mapana, macho madogo na lips nyembamba. Tukamweleza shida yetu.

Akiwa ameshikilia picha ya mtu tumtakaye, akasema, “huyu alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa zamu ya kumlinda Raisi.” Kisha akaminya lips na kufinya macho. “ila siku ambayo Raisi alipotea, hakuwa zamu. Hakuambatana naye.”

“Sasa yupo wapi?” akauliza Daniele akimtazama Director kwa umakini.

“Amefariki,” Director akajibu kisha akatupatia picha tatu toka kwenye droo yake. Zilikuwa ni picha za jengo linaloungua kuelekea majivuni.

“Tunaamini alifia humo. Mwili wake ulipatikana ukiwa umejeruhiwa sana, ngumu kutambulika. Hatukuwa na namnna zaidi ya kuufanyia taratibu za kuuzika.”

“Na vipi kuhusu familia yake?” nikamuuliza. “hana mke wala watoto?”

“Hakuwa na mtoto. Alikuwa anaishi na mwanamke ambaye aliachana naye muda mrefu kidogo kabla ya ajali hiyo kutokea.”

“Una picha ya mwanamke huyo?”

“Hapana.”

“Kuna habari yoyote ambayo aliwahi kufikisha kuu ya usalama wa Raisi?”

“Hamna habari ya kushtua. Zilikuwa ni habari za kawaida kutokana tu na majukumu yake.”

“Nino chanzo cha ajali yake hiyo? Mmechunguza mkajua?”

“Kwa mujibu wa wataalamu, ni ajali ya gesi. Bwana huyo alikuwa akitumia gesi kupikia.”

“Kabla ya ajali hiyo, hakuna dalili au mabadiliko yoyote ambayo bwana huyo aliyaonyesha?”

Director akabinua mdomo na kutikisa kichwa. Akaongezea, “alikuwa ni mfanyakazi mzuri sana. Sidhani kama anastahili kutiliwa shaka.”

“Vipi kuhusu bwana ---” nikasita. Niliona si stara kuntambulisha bwana O’neil. Kwa namna hiyo niliona ni kheri nikanyamaza kama ambavyo yeye alivyokuwa anahitaji. Faragha ya maisha yake.

Basi tukaaga na kwenda zetu.



***



Saa tatu usiku, Mgahawa wa Lemaire, Virginia.



Mezani nilikuwa na Jack Pyong na mchumba wake, Violette. Tulifika hapo muda si mrefu na hata bado hatukuwa tumeagiza chochote toka kwa mhudumu. Wakati Jack anaangaza macho yake, nikamuuliza, “kwanini mgahawa huu, Jack?”

“mzuri!” akanijibu kifupi na kisha akaniuliza, “kwani kuna tatizo bwana Tony?”

“Hapana, ila ni kama vile hamna mgahawa mwingine ndani ya jiji hili.”

“Tony, hapa kakuita nani?”

“Wewe!”

“Na mimi ndiye ntalipia bills, shida yako nini?”

“Kwani nilikuomba uniite?”

“Sasa mbona ukaja?”

Kabla sijajibu, jibu ambalo natumai lingemkera, mhudumu akawa amefika hapo. Mdada mrembo mwenye tabasamu usoni.

“Naweza kuwasaidia?”

Tukamuagiza chakula, nami angalau kinyongo changu kifuani dhidi ya Jack kikawa kimekauka.

“Nadhani sasa hivi ungekuwa kwenye kitanda chako cha baridi umejikunyata. Si ndiyo Tony?” Jack akan’chokoza. Sikutaka kumjibu. Chakula kilikuwa kitamu kuliko maneno yake ya kijinga. Huenda hii ndo’ ikawa sababu yake kupendelea mgahawa huu, chakula cha moto na kitamu.

“Maisha ya upweke mabaya sana Jack,” akaendelea kuhororoja. “inabidi ufanye namna uwe na pa kupumzikia!” hapa Violette akamwonya juu ya mdomo wake lakini nikijua ni kazi bure maana Jack hatosikia.

Uzuri sikujali, na kulikuwa na sababu nyingine ya kunifanya nimpuuzie. Chakula. Niliujaza mdomo wangu chakula, nikatafuna nikitazama wateja wengine waliofika hapo.

Sikukaa muda mrefu, nikasikia sauti ya mtu akikokota viatu vyake. Kabla sijageuka, sauti hiyo ikakoma na mara kutazama, mtu akaniangukia, nikawahi kumdaka! Naye Jack Pyong akainama kama aliyetaka kumdaka. Kumtazama mtu huyo, nikamkumbuka! Alikuwa ni yule mwanamke niliyekutana naye kule Hong Kong!

Nikiwa katika mshangao huo, mara nikashuhudia Jack Pyong akipiga magoti na kufunua kidude kidogo cha rangi ya zambarau. Akiwa amemtazama Violette, akamwambia, “Utakubali kuwa mke wangu?”

Violette alikuwa amepigwa na duwaa. Hakutegemea kile kitu. Hata mimi sikutaraji kabisa. Na hapa ndipo nilipofahamu ya kuwa mwanamke yule ambaye tulikutana naye Hong Kong, ndiye aliyeleta pete ile. Kwahiyo, Jack alikuwa ametufanyia surprise watu wawili kwa mpigo!

Akakumbatiana na Violette na sisi, mimi na yule mwanamke mgeni, tukaishia kupiga makofi na kuwapongeza.

“Jack, uliwezaje kuliweka siri hili hata kwangu?”

Akatabasamu. “Nilipanga kukwambia, ila niliona nawe uwe ni miongoni mwa watakaoshangazwa. Vipi? Nadhani umependa wazo langu sio?”

Nikamtazama yule mwanamke kando yangu. Alikuwa ndiye yuleyule. Macho makubwa, nywele nyeusi. Hakika alikuwa anavutia. Na kwa namna alivyokuwa ananitazama alinifanya nihisi maungio yangu ya mwili hayafanyi kazi.

“Umekuja kufanya nini Marekani?” nikamuuliza. Akan’tazama na kutabasamu.

“Kutalii.”

“Kweli?”

“Ndio! Kwani haiwezekani? Au Marekani si sehemu ya kutalii kama Hong Kong?”

“Ni majuzi tu umetoka Hong Kong, itawezekanaje uwe huku kutalii?”

Akamtazama mhudumu aliyekuwa amefika hapo, akamwagiza kinywaji na kisha akan’tazama kuendeleza soga.

“Nimekuja kusoma, Tony.”

“Na unajua jina langu!”

Akacheka kidogo akifunika kinywa chake. “kwanini nisijue. Uliniambia mwenyewe? .. aah sasa naamini siku ile ilikuwa ni pombe ipo kichwani sio?”

“Siku gani?”

“Kule Hong Kong kwenye party!”

“Tulitambushana mimi na wewe?”

“Maskini Tony. Ilikuwa ni mara yako ya kwanza kunywa?”

“Yah! Kama si huyu fala, nisingegusa kilevi!” nikasema nikimtazama Jack Pyong.

“Kwahiyo haukumbuki hata kama ulinibusu na kunikumbatia?”

“Nilifanya hivyo?” Nikauliza nikikodoa. Akacheka tena akifumba mdomo wake kwa kiganja. “Kipi sasa wakumbuka Tony?”

“Nadhani ni sura yako tu. Hiko kitu hakikutoka kichwani.”

“Kweli, naona.” Alisema hivyo kisha akanitazama akiwa kimya. Kwa muda nikahangaika kutafuta kauli yangu mdomoni. Na kama vile mtu aliyefahamu ‘struggle’ ninayopitia akatabasamu kwambali kisha akaniuliza, “vipi Tony, kuna kitu unataka sema?”

Kabla sijasema jambo, mhudumu akampatia juisi na mrija. Ilikuwa ni juisi baridi ya tufaha. Hapo akanywa mafundo kadhaa kabla hatujaendelea na maongezi yetu machache. Alijitambulisha kwa jina la Kelly na kama alivyoniambia hapo awali, yeye alikuwapo hapo kwa ajili ya kusoma, chuo kikuu cha Harvard kitivo cha sheria.

Nilipotaka kufahamu juu ya wapi alipotokea, akanisihi nisiwe na haraka. Kila kitu kitajulikana taratibu.

“Maisha yangu yapo ‘simple’ and ‘straight’, Tony. Utajua kila kitu ndani ya muda mfupi. Lakini ukiwa ‘interested’.”

Baada ya hapo, Jack Pyong na Violette hawakukaa sana, wakatuaga wanaenda zao. Jack akanikonyeza akiwa anaenda zake.

“Sasa,” Kelly akachokoza mada. “Wewe hauondoki? Unalala hapa nini?”

Nikatabasamu kisha nikatazama saa yangu. Yalikuwa ni majira ya saa tano sasa usiku. Kweli muda ulikuwa umeenda. Nilimtazama Kelly na kumuuliza juu ya makazi yake, akaniambia kuwa amefikia kwenye apartment moja ndani ya Virginia.

“Kwanini Virginia na si Massachusetts huko karibu na chuo cha Harvard?”

Akatabasamu pasipo kuonyesha meno. Mashavu yake yalituna na macho yake kujifinya.

“Kwasababu ndo’ sehemu ambapo nina mwenyeji!”

“Mwenyeji? Hapa Virginia?”

“Ndio.”

“Wapi huko?”

Kabla hajajibu akaingiza mrija mdomoni mwake na kufyonza juisi.



**
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom