Nyuma yako - Riwaya ya SteveMollel

*NYUMA YAKO -- 05*

*Simulizi za series*


Nikamuuliza, "lakini mbona wewe ni wa tofauti na wenzako? Umejuaje lugha yetu?"
Akaniuliza, "hayo ndiyo maneno yako ya mwisho ukielekea kufa?" Kisha akatikisa kichwa. "Nilidhani wewe ni mwerevu."
ENDELEA
Na asiendelee kuongea nami, akashika njia aende zake. Nikamwita asijali. Akaendelea kuondoka akipiga mluzi. Lakini nilipomwambia maneno haya, akasimama.
"Nina kitu kwa ajili yako!"
Akanitazama na kisha akakunja sura kama atiaye shaka alafu akanijongea na kuniambia, "sina muda wa kupoteza nawe ewe bwana wa manjano. Ni nini hiko wataka kuniambia?"
"Kama unataka nikuambie niweke huru toka kwenye nyara hizi!" Nikamsihi. Akatabasamu na kisha kucheka kidogo kana kwamba mtu mwenye utumbo mtupu. "Unadhani mimi ni mjinga kama wewe?" Akaniuliza.
"Ujinga wangu uko wap?"
Akatahamaki, "hujioni ulivyo mjinga? Uliwaua watu wa kijiji hiki alafu ukaja tena ukiwa hujiwezi. Unadhani wewe ni mwerevu?"
"Sikuwahi kuj--"
"Ishia hapo! Siko kuskiza ngonjera zako. Kama huna cha kuniambia, acha niende kwa amani nawe ubaki hapa kutafunwa na mti!"
"Ninacho ... ninacho cha kukuambia. Na najua utafurahi ukikisikia."
Akabaki akin'tazama kwa macho ya mchoko. Hakutaka tena kusema kitu bali asikie hicho ambacho nataka kumwambia.
"Umeona ewe bwana mdogo, nina namna ya kukufanya uishi chini ya maji!"
Nikamwaona akikunja ndita za umakini kwa mbali. Hapa nikajua mada yangu imemgusa.
"Kama afanyavyo samaki, nawe utaishi, kuona na kuzamia. Je, hiko si kitu cha maana kukwambia?"
Nilitazamia jambo hilo litakuwa geni kwake. Niliomba iwe hivyo, kwani kama ingelikuwa tofauti, basi ningeambulia kuachwa nijifie. Hapana. Nilikuja hapa kumsaka Raisi na si kifo.
Akanicheka. "Unamaanisha mtungi wa hewa na mawani ya kuziba macho?" Akaniuliza akibinua mdomo. Akacheka tena mpaka akidaka magoti yake na kushikilia tumbo lake.
"Skiza ewe mtu wa manjano. Mimi si mjinga kama unavyofikiri kichwani mwako. Unadhani sijui unavyovizungumza?"
Akanipa maswali juu yake, mbona ni mwerevu kiasi hiki? Kumbe mtu huyu si tu kwamba anajua lugha yetu, bali pia na teknolojia! Hapa ilinibidi nifanye kazi ya ziada.
"Sawa, basi nitakupa cha kukufanya uone nyakati za usiku!" Nikasema kwa kujivuna. "Utatembea kama mchana usijikwae kisiki au kudumbukia shimoni!"
Hapa akanyamaza kwa muda, macho yakiwaza, alafu akaniuliza, "sasa umeona unidanganye?"
Nikajua hili kwake ni geni.
"Nidanganye ya nini na wakati naomba kubakiziwa uhai tena nikiwa nimezingirwa na maji pande zote?"
Akabinua mdomo na asiseme chochote, akaenda zake. Nikamwita asigeuke nyuma abadani mpaka anatokomea. Nikalaani sana. Nikajiuliza ni nini nitafanya na wakati mikono na miguu yangu imefungwa kwa kamba kiasi kile?
Tukio hilo likanikumbusha mbali sana. Mbali ya mwaka juzi ambapo niliagizwa kwenda kuwakomboa baadhi ya mateka wa kimarekani waliokuwa wanashikiliwa na wanamgambo wa Boko Haram huko nchini Nigeria.
Nakumbuka, nikiwa nimeambatana na wanaume wanne , wamarekani weusi, wa kikosi maalum (special forces), tukiwa mgahawani, tulizingirwa na kuwekwa chini ya ulinzi na watu sita ambao walikuwa wameficha nyuso zao na kubebelea bunduki aina ya ak 47.
Watu hawa kwa namna tulivyowatazama walikuwa ni wanamgambo wa Boko Haram, haswa kutokana na mitandio waliyokuwa wamejivika nayo usoni mbali na kombati walizovaa.
Walituamrisha tunyooshe mikono juu na kututaka tuendee gari walizokuja nazo. Tukafanya hivyo pasipo ubishi. Wakatusweka na kutimka tukielekea mahali tusipopajua kwa maana walitia vichwa vyetu ndani ya mifuko meusi.
Wakiwa wanatupeleka huko, wakawa wanateta kwa lugha ya kiarabu ambayo tulikuwa tunaisikia, wakifurahia kukamatwa kwetu na namna ambavyo wao watanufaika kwa kuongeza mateka wa kimarekani kwenye ghala.
Lakini walijuaje kama sisi ni wamarekani? Ilikuwa ni rahisi sana, na 'in fact' ni sisi ndiyo tulifanya wakatujua hivyo. Hapo mgahawani tulikuja na gari, Nissan double cabin nyeupe, yenye chapa ya USAID ubavuni. USAID ni shirika la Marekani.
Tukiwa mgahawani, tukawa tukizungumza kiingereza chetu, kiingereza cha lafudhi ya Marekani. Na zaidi mgahawa huo ulikuwa ukipatikana katika moja ya kanda ambazo ni mhanga wa mashambulizi ya mara kwa mara ya Boko Haram, kaskazini mashariki wa Nigeria, hivyo kutokea kwa wale wajamaa kilikuwa ni kitu cha kutegemewa. Kitu ambacho unaweza kukibashiri!
Wakiwa wanazungumza hayo yao, tena sisi tukiwa tunawaelewa, nasi tukawa tunazungumza kwa ishara, 'sign language' pasipo wao kuhisi wala kuelewa.
'Sign language' ama 'paralinguistic language' ni lugha isiyo na maandishi ama sauti. Ni utaalamu wa kufikisha ujumbe kwa namna ya kupeana ishara 'signals' na mwenzako akakuelewa na kujibu.
Hiki ni miongoni mwa vitu tujifunzavyo tuwapo mafunzoni kwaajili ya kujiandaa na mazingira mbalimbali ukiwa mhitaji wa kuwasiliana.
Kwa kutumia miguu yetu, tukaminyana, na pia kwa kutumia mikono yetu ambayo ilikuwa imefungwa, tukagusana kwa vidole tukifikishiana ujumbe.
Baada ya hapo, tukangoja. Mwendo wa kama nusu saa tukiwa kimya, ila sio tukiwa malofa. Mmoja wetu tulimpatia kazi ya kuhesabu majira na zoezi la kutushtua pale atakapokuwa ameona mahesabu tuliyoyapanga yametimia.
Kwa muda wa kawaida, kama tulivyokuwa tukiwaza kuwa watu hawa watakuwa wanatupeleka msitu wa Sambisa ambao ni moja ya ngome ya Boko Haram, ilikuwa yachukua kama lisaa limoja na dakika kumi na mbili endapo gari ikienda kwa mwendo wa kilomita themanini kwa lisaa.
Na kama halitoenda kwa mwendo huo, basi tena linakuwa jukumu na mpanga mahesabu kupiga mahesabu hayo kutokana na mwendo ulivyo. Kwa nilivyokuwa nahisi, gari lilikuwa linaenda kilomita mia na ishirini kwa lisaa. Sikuwa mbali na ukweli. Kidogo mahesabu yangu yalikaribiana na mkokotoaji yakiachana kwa kama sekunde kumi na sita tu!
Nikabinywa pajani. Hiyo ilikuwa ni ishara kuwa muda uliokuwa umetengwa sasa umekaribia, zimebaki sekunde nne tu. Nikabinywa na vidole vinne, vitatu, viwili, mwishowe kimoja! Kidogo gari likazama kwa korongo barabarani, hapo hapo, ndani ya dakika chache, tukanyanyuka na kutupa miili yetu mahali tulipokuwa tukisikia sauti za watu na kuhisi uwepo wao!
Ilikuwa ni kitu cha upesi na kushtukiza!
Kule kwenye bodi mulikuwa na wanamgambo sita, watatu wakikalia kushoto na watatu kulia, na basi kwasababu sisi tulikuwa watano kwa idadi, ilikuwa rahisi kuleta shambulizi lenye tija kwa kufuata mipango tuliyopanga kuwa wawili wataenda huku na watano wataenda upande mwingineo.
Ilikuwa pia rahisi kwasababu wanamgambo wale hawakuwa kwenye balansi muda mfupi baada ya gari kupitia mtikisiko. Hivyo, baada ya kufanya hivyo, nikawahisha kichwa changu kwenye mikono ya mwenzangu, akanivua mfuko kichwani.
Kutazama, nikawaona wanamgambo wawili wakiwa wanajiweka tenge kushambulia kwa risasi. Wawili walidondoka chini barabarani, wawili wengine wakiwa wameshikilia bomba la gari kutafuta balansi!
Haraka nikajitupa samasoti kwa chini kuwafuata. Nikamtengua mmoja miguu, na yule mwingine alipotaka kunishambulia, nikajikinga na mwili wa mwenzake, alafu nikampokonya bunduki yule niliyemtumia kama ngao na kisha mwili wake nikamtupia mwenziwe, wote wakadondoka chini!
Nikasikia ti-ti-ti-ti! Haraka nikajilaza chini. Kutazama nikaona mwenzetu mmoja akiwa amedondoka kwa kushindiliwa risasi! Tulikuwa tukishambuliwa na dereva.
Nikatulia na kufyatya risasi moja, ikamdungua kichwa na kummaliza papo hapo, gari likaanza kwenda mrama, lakini kabla halijaleta madhara, mmoja wetu akaliwahi na kuliweka kimyani, kisha tukaendeleza na safari kwenda huko msituni.
Basi kwakuwa wale wenzangu walikuwa na ngozi nyeusi wakajivika nguo za wale wanamgambo na kisha kuigiza kuwa wameniteka kwa lengo la kuzama ndani ya ngome.
Kwa kufupisha habari hiyo, ambayo pengine nitakuja kuisimulia vema siku nyingine, kilichonifanya niikumbuke ni namna tulivyokuta mateka wakiwa wamefungwa kamba mitini, wamarekani na wengine toka nchi za Ulaya. Na kwasababu za kioparesheni, nami nikatiwa kambani kama wale mateka wengine, lakini kamba yangu ilikuwa legevu kwa maana kwamba punde mambo yatakapoharibiwa nitoke hapo.
Ilikuwa ni tofauti na oparesheni ya Raisi kule kisiwani kwani kamba ya kisiwani ilikuwa imekazwa haswa na hakukuwa na namna ya mimi kuchoropoka isipokuwa kwa msaada. Na tofauti kabisa na Nigeria, siku hiyo wenzangu wote walikuwa hawajiwezi. Hawakupewa tiba kama ilivyokuwa kwangu, hivyo siku hiyo mimi ndo' nilikuwa na jukumu la kuwaokoa.
Muda ukaenda na giza la usiku likafika. Punde kidogo, baada ya giza hilo kuingia, nikaanza kutambua kwanini tulifungiwa kwenye miti ile mipana. Nilianza kuhisi mgongo wangu unafinywa kuzamia ndani, na kadiri muda ulivyokuwa unaenda, nikawa nahisi maumivu makali ya mgongo.
Nikajitahidi kujichoropoa, wapi! Zaidi nikajiongezea maumivu zaidi. Niliporusha macho kuwatazama wenzangu, nikawaona wakiwa wametulia tuli. Hawakuwa na fahamu!
Nikahisi usiku huu ndiyo mwisho wetu.

**
 
*NYUMA YAKO -- 06*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA
Nikajitahidi kujichoropoa, wapi! Zaidi nikajiongezea maumivu zaidi. Niliporusha macho kuwatazama wenzangu, nikawaona wakiwa wametulia tuli. Hawakuwa na fahamu!
Nikahisi usiku huu ndiyo mwisho wetu.
ENDELEA
Hata nikainamisha kichwa changu kama kristo msalabani, sasa nimekwisha. Mwanaume miliyeshiriki kwenye misheni kadhaa za hatari, nakuja kuuawa na hawa washamba wa msituni. Aibu iliyoje?
Ila, nikajadili na nafsi yangu, haikuwa kama nilivyokuwa nawaza. Hamna mtu aliyedhani hapa kuna watu, na zaidi ya yote, kwenye shambulio la kushtukizwa, hamna mjanja. Atakayemuwahi mwenziwe basi ndo anakuwa mshindi. Hata simba akiwa mbugani, anawezwa wahiwa na nyoka, akamalizwa!
Hapa tulikuwa tumewahiwa, na japo lilikuwa jambo chungu kwangu, ila ndiyo ulikuwa uhalisia. Sikuwa na ujanja wa ziada.
Nikiwa nimejikatia tamaa, nangoja sasa 'nimezwe' na ule mti kama tulivyonenewa, nikahisi kitu huko msituni! Masikio yangu yakasimama na macho yangu yakang'aza. Ilikuwa ni kama kishindo cha mtu au mnyama ila sikuona kitu!
Kishindo hicho hakikukoma, kikaendelea tena na tena na kunijaza hofu huenda akawa mnyama wa mwituni. Endapo akitokea hapo tutajiteteaje? Nikapata mawazo yaliyonipa tena nguvu ya ajabu kupambana na kamba nilizofungiwa.
Nikapambana kujisukuma na kusukuma, waapi! Zaidi nikajitia alama nyekundu mwilini, pia majeraha na maumivu tu! Sikufanikiwa wala kwa dalili!
Kishindo kikaendelea kusikika huko gizani msituni na mara sauti ikasema, "ewe mtu wa manjano, bado upo?"
Nikaitambua sauti hiyo kuwa ya bwana yule mdogo. Bwana azungumzaye lugha yetu. Yeye alitokea upande wangu wa kushoto baada ya punde na kisha kunisogelea kwa karibu.
Akanitazama machoni. "Naona bado upo. Vipi, unaendeleaje?"
"Hali inazidi kuwa mbaya," nikamjibu na kumsihi, "naomba uniweke huru!"
"Si kwa haraka hivyo," akasema akitikisa kichwa chake, kisha akahema akinitazama kama mtu anayefurahia mateso yangu. Akaniuliza, "kwanini mlivamia kijiji chetu? Ni nini tuliwakosea?"
Nikamtazama kwa macho yangu malegevu. Uso wake ulikuwa unang'azwa na mwanga wa mbalamwezi. Nikafungua kinywa changu kikavu na kumwambia, "sijawahi kuja hapa, hii ni mara yangu ya kwanza. Nikuambieje unielewe?"
Mara akatoa kijiwe fulani nyuma ya mgongo wake. Kilikua ni kijiwe kidogo kimachong'aa. Kwa mwanga ule uliokuwepo nilikiona ni kijiwe chenye rangi nyekundu, sikujua mwangani mwa jua kingeonekanaje.
Akaniuliza akinionyeshea kijiwe hicho, "ni hichi ndicho mnatafuta?"
"Hapana!" Nikajikakamua kukanusha. "Sina shida na chochote toka kwenu. Nimefika hapa kumtafuta mtu aliyepotea, na si vijiwe!"
"Mtu gani huyo? Yule aliyedondoka toka kwenye nyota?" Akaniuliza akishika kidevu chake.
Nikamkazia, "Ndio huyohuyo! Je, umemwona?"
"Ndio. Nimemwona."
Hapa nikatoa macho. "Yupo wapi? ... tafadhali nipatie mtu huyo nasi tutaondoka msituone tena!"
Akatulia kidogo. Akanitazama kwa mafikirio alafu akaniuliza, "nikikuonyesha utanipatia nini?"
"Chochote kati ya tulivyokuja navyo!"
"Mi' nataka kile cha kuonea usiku. Mimi ni mwindaji. Nahisi kitanisaidia sa--"

"Nitakupatia, usijali!" Nikamkatiza. "We twende nionyeshe wapi alipo mtu huyo!"
Basi akanifungua kamba na tukaanza safari. Lakini hakuwa mjinga, aliniweka mbele yeye akiwa nyuma yangu. Mkononi alibebelea mkuki na kinywani alikuwa ameshikilia filimbi kwa lips zake. Filimbi hii, kwa alivyoniambia, ingemwamsha kila mtu kijijini aje kunitafuta endapo ningejitia ukaidi.
Sikupanga kuwa mkaidi. Lah! Hamu yangu ya kuuona mwili wa mtu ambaye nilihisi ndiye namtafuta ilikuwa kubwa kuliko kufanya njama za kutoroka.
Tukasonga, akiwa ananielekeza, mpaka eneo fulani ambapo alinitaka nisimame na kutulia. Nikafanya hivyo. Hapo toka kwenye kibanda kimoja kidogo kilichotengenezwa kwa matawi ya miti, akapenyeza mkono wake na kutoa mti mmoja mrefu, sikujua wa nini, akatoa pia na dude fulani kama rungu kisha akaniambia tuendelee na safari.
Tulipotembea kwa muda kidogo akaniamuru nisimame na kisha akaniambia, "mwili huo upo humo shimoni, utazama humo uangaze, nami nitakuvuta kwa mti utoke nje!"
Alipoyasema hayo akaniwashia lile dude nililodhani ni rungu, tena kwa haraka akitumia mawe, alafu akanishikisha ule mti mrefu nami nikazama na ginga la moto ndani ya shimo.
Lilikuwa ni shimo refu, na kadiri nilivyokuwa nazama nikawa nahisi harufu ya mzoga puani mwangu. Zaidi na zaidi. Na nikiwa sasa nimefikia nchani mwa fimbo ile ambayo nimeishikilia, nikawa nimefika chini kabisa! Kumbe ile fimbo ilikuwa na vipimo sawia kulingana na shimo.
Nikaangaza kutazama na ginga langu la moto, humo nikaona miili kadhaa, na mmoja kati yao, ambao ulikuwa mpyampya tuseme, ukawa umekamata macho yangu. Mwili huo ulikuwa mpana na wenye kuvalia suti nyeusi. Ulikuwa umelala kifudifudi.
Nikachuchumaa na kuugeuza niutazame. Haukuwa wa Raisi! Nikawaza utakuwa ni miongoni mwa wale maajenti wasiokuwepo kule ndani ya ndege. Sasa mwili wa Raisi utakuwa wapi? Nikajiuliza nikiendelea kuangazaangaza. Sikuuona!
Nilishika kiuno changu na kushusha pumzi ndefu.
"Vipi? Si huo?" Akaniuliza yule bwana mdogo juu ya shimo.
"Hapana, si wenyewe!"
Nikamwomba mti, anivute juu. Nilipopanda nikakung'uta mwili wangu na kumuuliza, "hakuna mwingine ninaoweza kutazama?"
Nikamwona akibinua mdomo wake. "Hapana, hili ndilo shimo pekee lililopo hapa."
Nikanyamaza nikiwaza. Akan'tazama na kunitahadharisha, "lakini makubaliano yetu si yapo palepale?"
Sikumjibu. Mimi nilikuwa na mawazo yangu kichwani. Akili yangu yote ilikuwa inawaza namna gani ambavyo naweza kuupata ama kuuona mwili wa Raisi. Hali hiyo ikampatia hofu yule bwana mdogo, nadhani akahisi nitamgeuka. Akanionyeshea mkuki wake na kuniambia tena, "makubaliano yetu si yapo palepale?"
"Ndio," nikamjibu kumtoa hofu. "Makubaliano yetu yapo palepale!"
Kidogo akatulia. Kwa muda huu nikawa nimemtengeneza rafiki. Nikapata mwanya wa kumuuliza kwanini aliniamini akanifungulia pale mtini ilhali mwanzoni walin'tilia shaka.
Akanitazama kwanza. Akatabasamu kwa mbali na kuniambia, "wewe sio kama wale! ... wale waliokuja kutuvamia na kuwaua wenzetu!"
"Umejuaje kuwa sisi sio wale?"
"Kwasababu ya kile kijiwe!" Akanijibu aking'aza macho. "Watu wale waliokuja na kuwaua wenzetu hawakuwa wanataka kingine zaidi ya mawe! ... wewe nilikuona upo tofauti. Sikuona tamaa ndani ya macho yako punde nilipokuonyesha kile kijiwe."
"Lakini tuliwaambia mwanzoni kuwa sisi tunamtafuta mwenzetu!"
"Ndio, ila si rahisi kuamini ... poleni."
"Basi naomba ukawasaidie wale wenzangu kama ulivyofanya kwangu."
"Siwezi!"
"Kwanini?"
"Mimi sina ile dawa waliyokupa wewe."
"Nani anayo?"
"Yule aliyekupa wewe. Anaitwa Toliso."
"Hauwezi kwenda mwomba? ... hauwezi ukamwambia kuwa sisi si kama wale waliokuwa wanawadhania?"
Bwana yule akanyamaza. Akausimika mkuki wake ardhini na kisha kidevu chake akakiweka juu ya kitako cha mkuki. "Si rahisi kama unavyodhani," akanijibu akiwa ameng'ata meno yake.
"Bwana yule, Toliso, ni mkatili na mkali. Hawezi kunielewa."
Nikamsogelea karibu na kumshika bega. "Tafadhali, sisi hatuna hatia. Hakukuwa na haja ya kutuadhibu namna ile. Kama kuna namna yoyote ambayo naweza kukusaidia kupata hiyo dawa, nambie nami nitafanya kwa moyo wote!"
Akatikisa kichwa kisha akafungua kiganja chake. "Kabla hatujaendelea na majadiliano yoyote, nipe kwanza kile ulichoniahidi."
"Nitakupatia il--"
"Nipe!" Akasisitiza akinikazia macho , basi nikaona si tabu, nikaongozana naye mpaka kule upande tulioingilia kisiwani. Huko tukute vile vitu tulivyoviacha, mitungi ya hewa na hata hiyo miwani ya kutazamia usiku.
Bahati tukavikuta, nikamkabidhi. Akajaribisha na kuona ni vema, imempendeza. Akafurahi sana. "Hii nitaitumia kuwindia nyakati kama hizi!" Akasema akitabasamu. Hata meno yake yaling'aa kinyume na kiza.
Nikamkumbusha, "fanya basi tukapate ile dawa!"
Akaiweka ile miwani kibindoni alafu akanitazama, "ewe bwana wa manjano, mbona wewe mbishi sana! Huoni kheri nimekusaidia ukaenda zako?"
"Nitaendaje pasipo wenzangu? Moyo wangu utakuwa mzito!"
"Sikia ... si kwamba sitaki kukusaidia. Namwogopa sana Toliso. Mkono wake ni mwepesi sana kutoa adhabu. Si mtu anayejishauri mara mbilimbili kummaliza mtu!"
"Nitakusaidia dhidi yake."
Akatabasamu, "wewe? ... unadhani unaweza kupambana na Toliso?"
"Kwanini nisiweze?"
Akashindwa kujibana na kicheko. Alipomaliza kucheka akaniambia, "mwili wako unaingia mara mbili na nusu ya Toliso. Akikudaka na mikono yake kama mibuyu, atakukamua mpaka hayo macho yatoke nje. Hujionei huruma?"
"Bwana mdogo," nikamwita nikimtazama. "Nitafanya lolote lile, nitapita kwenye hatari yoyote ile kuwasaidia wenzangu. Naomba tusipoteze muda, tuelekee huko haraka!"
Akanitazama katika namna ya kunionea huruma. Kwa namna hiyo nikajua ni kwanini anamzungumzia Toliso katika namna ya hofu. Ila nadhani bado nami hakuwa ananijua vema. Hakuwa anajua mimi ni mtu wa namna gani. Tangu tuingie kwenye mikono yao, hajaona vumbi langu. Sikushangaa kwanini alikuwa ananitilia shaka.
Hakuwa anajua japo mimi si nyani mzee, nimekwepa ncha nyingi za mishale!
Basi kwakuwa nimemlazimisha na kumsihi sana, tukaenda huko.

**
 
Aise safi sana hii ukituma tena usiache kunitag
*NYUMA YAKO -- 06*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA
Nikajitahidi kujichoropoa, wapi! Zaidi nikajiongezea maumivu zaidi. Niliporusha macho kuwatazama wenzangu, nikawaona wakiwa wametulia tuli. Hawakuwa na fahamu!
Nikahisi usiku huu ndiyo mwisho wetu.
ENDELEA
Hata nikainamisha kichwa changu kama kristo msalabani, sasa nimekwisha. Mwanaume miliyeshiriki kwenye misheni kadhaa za hatari, nakuja kuuawa na hawa washamba wa msituni. Aibu iliyoje?
Ila, nikajadili na nafsi yangu, haikuwa kama nilivyokuwa nawaza. Hamna mtu aliyedhani hapa kuna watu, na zaidi ya yote, kwenye shambulio la kushtukizwa, hamna mjanja. Atakayemuwahi mwenziwe basi ndo anakuwa mshindi. Hata simba akiwa mbugani, anawezwa wahiwa na nyoka, akamalizwa!
Hapa tulikuwa tumewahiwa, na japo lilikuwa jambo chungu kwangu, ila ndiyo ulikuwa uhalisia. Sikuwa na ujanja wa ziada.
Nikiwa nimejikatia tamaa, nangoja sasa 'nimezwe' na ule mti kama tulivyonenewa, nikahisi kitu huko msituni! Masikio yangu yakasimama na macho yangu yakang'aza. Ilikuwa ni kama kishindo cha mtu au mnyama ila sikuona kitu!
Kishindo hicho hakikukoma, kikaendelea tena na tena na kunijaza hofu huenda akawa mnyama wa mwituni. Endapo akitokea hapo tutajiteteaje? Nikapata mawazo yaliyonipa tena nguvu ya ajabu kupambana na kamba nilizofungiwa.
Nikapambana kujisukuma na kusukuma, waapi! Zaidi nikajitia alama nyekundu mwilini, pia majeraha na maumivu tu! Sikufanikiwa wala kwa dalili!
Kishindo kikaendelea kusikika huko gizani msituni na mara sauti ikasema, "ewe mtu wa manjano, bado upo?"
Nikaitambua sauti hiyo kuwa ya bwana yule mdogo. Bwana azungumzaye lugha yetu. Yeye alitokea upande wangu wa kushoto baada ya punde na kisha kunisogelea kwa karibu.
Akanitazama machoni. "Naona bado upo. Vipi, unaendeleaje?"
"Hali inazidi kuwa mbaya," nikamjibu na kumsihi, "naomba uniweke huru!"
"Si kwa haraka hivyo," akasema akitikisa kichwa chake, kisha akahema akinitazama kama mtu anayefurahia mateso yangu. Akaniuliza, "kwanini mlivamia kijiji chetu? Ni nini tuliwakosea?"
Nikamtazama kwa macho yangu malegevu. Uso wake ulikuwa unang'azwa na mwanga wa mbalamwezi. Nikafungua kinywa changu kikavu na kumwambia, "sijawahi kuja hapa, hii ni mara yangu ya kwanza. Nikuambieje unielewe?"
Mara akatoa kijiwe fulani nyuma ya mgongo wake. Kilikua ni kijiwe kidogo kimachong'aa. Kwa mwanga ule uliokuwepo nilikiona ni kijiwe chenye rangi nyekundu, sikujua mwangani mwa jua kingeonekanaje.
Akaniuliza akinionyeshea kijiwe hicho, "ni hichi ndicho mnatafuta?"
"Hapana!" Nikajikakamua kukanusha. "Sina shida na chochote toka kwenu. Nimefika hapa kumtafuta mtu aliyepotea, na si vijiwe!"
"Mtu gani huyo? Yule aliyedondoka toka kwenye nyota?" Akaniuliza akishika kidevu chake.
Nikamkazia, "Ndio huyohuyo! Je, umemwona?"
"Ndio. Nimemwona."
Hapa nikatoa macho. "Yupo wapi? ... tafadhali nipatie mtu huyo nasi tutaondoka msituone tena!"
Akatulia kidogo. Akanitazama kwa mafikirio alafu akaniuliza, "nikikuonyesha utanipatia nini?"
"Chochote kati ya tulivyokuja navyo!"
"Mi' nataka kile cha kuonea usiku. Mimi ni mwindaji. Nahisi kitanisaidia sa--"

"Nitakupatia, usijali!" Nikamkatiza. "We twende nionyeshe wapi alipo mtu huyo!"
Basi akanifungua kamba na tukaanza safari. Lakini hakuwa mjinga, aliniweka mbele yeye akiwa nyuma yangu. Mkononi alibebelea mkuki na kinywani alikuwa ameshikilia filimbi kwa lips zake. Filimbi hii, kwa alivyoniambia, ingemwamsha kila mtu kijijini aje kunitafuta endapo ningejitia ukaidi.
Sikupanga kuwa mkaidi. Lah! Hamu yangu ya kuuona mwili wa mtu ambaye nilihisi ndiye namtafuta ilikuwa kubwa kuliko kufanya njama za kutoroka.
Tukasonga, akiwa ananielekeza, mpaka eneo fulani ambapo alinitaka nisimame na kutulia. Nikafanya hivyo. Hapo toka kwenye kibanda kimoja kidogo kilichotengenezwa kwa matawi ya miti, akapenyeza mkono wake na kutoa mti mmoja mrefu, sikujua wa nini, akatoa pia na dude fulani kama rungu kisha akaniambia tuendelee na safari.
Tulipotembea kwa muda kidogo akaniamuru nisimame na kisha akaniambia, "mwili huo upo humo shimoni, utazama humo uangaze, nami nitakuvuta kwa mti utoke nje!"
Alipoyasema hayo akaniwashia lile dude nililodhani ni rungu, tena kwa haraka akitumia mawe, alafu akanishikisha ule mti mrefu nami nikazama na ginga la moto ndani ya shimo.
Lilikuwa ni shimo refu, na kadiri nilivyokuwa nazama nikawa nahisi harufu ya mzoga puani mwangu. Zaidi na zaidi. Na nikiwa sasa nimefikia nchani mwa fimbo ile ambayo nimeishikilia, nikawa nimefika chini kabisa! Kumbe ile fimbo ilikuwa na vipimo sawia kulingana na shimo.
Nikaangaza kutazama na ginga langu la moto, humo nikaona miili kadhaa, na mmoja kati yao, ambao ulikuwa mpyampya tuseme, ukawa umekamata macho yangu. Mwili huo ulikuwa mpana na wenye kuvalia suti nyeusi. Ulikuwa umelala kifudifudi.
Nikachuchumaa na kuugeuza niutazame. Haukuwa wa Raisi! Nikawaza utakuwa ni miongoni mwa wale maajenti wasiokuwepo kule ndani ya ndege. Sasa mwili wa Raisi utakuwa wapi? Nikajiuliza nikiendelea kuangazaangaza. Sikuuona!
Nilishika kiuno changu na kushusha pumzi ndefu.
"Vipi? Si huo?" Akaniuliza yule bwana mdogo juu ya shimo.
"Hapana, si wenyewe!"
Nikamwomba mti, anivute juu. Nilipopanda nikakung'uta mwili wangu na kumuuliza, "hakuna mwingine ninaoweza kutazama?"
Nikamwona akibinua mdomo wake. "Hapana, hili ndilo shimo pekee lililopo hapa."
Nikanyamaza nikiwaza. Akan'tazama na kunitahadharisha, "lakini makubaliano yetu si yapo palepale?"
Sikumjibu. Mimi nilikuwa na mawazo yangu kichwani. Akili yangu yote ilikuwa inawaza namna gani ambavyo naweza kuupata ama kuuona mwili wa Raisi. Hali hiyo ikampatia hofu yule bwana mdogo, nadhani akahisi nitamgeuka. Akanionyeshea mkuki wake na kuniambia tena, "makubaliano yetu si yapo palepale?"
"Ndio," nikamjibu kumtoa hofu. "Makubaliano yetu yapo palepale!"
Kidogo akatulia. Kwa muda huu nikawa nimemtengeneza rafiki. Nikapata mwanya wa kumuuliza kwanini aliniamini akanifungulia pale mtini ilhali mwanzoni walin'tilia shaka.
Akanitazama kwanza. Akatabasamu kwa mbali na kuniambia, "wewe sio kama wale! ... wale waliokuja kutuvamia na kuwaua wenzetu!"
"Umejuaje kuwa sisi sio wale?"
"Kwasababu ya kile kijiwe!" Akanijibu aking'aza macho. "Watu wale waliokuja na kuwaua wenzetu hawakuwa wanataka kingine zaidi ya mawe! ... wewe nilikuona upo tofauti. Sikuona tamaa ndani ya macho yako punde nilipokuonyesha kile kijiwe."
"Lakini tuliwaambia mwanzoni kuwa sisi tunamtafuta mwenzetu!"
"Ndio, ila si rahisi kuamini ... poleni."
"Basi naomba ukawasaidie wale wenzangu kama ulivyofanya kwangu."
"Siwezi!"
"Kwanini?"
"Mimi sina ile dawa waliyokupa wewe."
"Nani anayo?"
"Yule aliyekupa wewe. Anaitwa Toliso."
"Hauwezi kwenda mwomba? ... hauwezi ukamwambia kuwa sisi si kama wale waliokuwa wanawadhania?"
Bwana yule akanyamaza. Akausimika mkuki wake ardhini na kisha kidevu chake akakiweka juu ya kitako cha mkuki. "Si rahisi kama unavyodhani," akanijibu akiwa ameng'ata meno yake.
"Bwana yule, Toliso, ni mkatili na mkali. Hawezi kunielewa."
Nikamsogelea karibu na kumshika bega. "Tafadhali, sisi hatuna hatia. Hakukuwa na haja ya kutuadhibu namna ile. Kama kuna namna yoyote ambayo naweza kukusaidia kupata hiyo dawa, nambie nami nitafanya kwa moyo wote!"
Akatikisa kichwa kisha akafungua kiganja chake. "Kabla hatujaendelea na majadiliano yoyote, nipe kwanza kile ulichoniahidi."
"Nitakupatia il--"
"Nipe!" Akasisitiza akinikazia macho , basi nikaona si tabu, nikaongozana naye mpaka kule upande tulioingilia kisiwani. Huko tukute vile vitu tulivyoviacha, mitungi ya hewa na hata hiyo miwani ya kutazamia usiku.
Bahati tukavikuta, nikamkabidhi. Akajaribisha na kuona ni vema, imempendeza. Akafurahi sana. "Hii nitaitumia kuwindia nyakati kama hizi!" Akasema akitabasamu. Hata meno yake yaling'aa kinyume na kiza.
Nikamkumbusha, "fanya basi tukapate ile dawa!"
Akaiweka ile miwani kibindoni alafu akanitazama, "ewe bwana wa manjano, mbona wewe mbishi sana! Huoni kheri nimekusaidia ukaenda zako?"
"Nitaendaje pasipo wenzangu? Moyo wangu utakuwa mzito!"
"Sikia ... si kwamba sitaki kukusaidia. Namwogopa sana Toliso. Mkono wake ni mwepesi sana kutoa adhabu. Si mtu anayejishauri mara mbilimbili kummaliza mtu!"
"Nitakusaidia dhidi yake."
Akatabasamu, "wewe? ... unadhani unaweza kupambana na Toliso?"
"Kwanini nisiweze?"
Akashindwa kujibana na kicheko. Alipomaliza kucheka akaniambia, "mwili wako unaingia mara mbili na nusu ya Toliso. Akikudaka na mikono yake kama mibuyu, atakukamua mpaka hayo macho yatoke nje. Hujionei huruma?"
"Bwana mdogo," nikamwita nikimtazama. "Nitafanya lolote lile, nitapita kwenye hatari yoyote ile kuwasaidia wenzangu. Naomba tusipoteze muda, tuelekee huko haraka!"
Akanitazama katika namna ya kunionea huruma. Kwa namna hiyo nikajua ni kwanini anamzungumzia Toliso katika namna ya hofu. Ila nadhani bado nami hakuwa ananijua vema. Hakuwa anajua mimi ni mtu wa namna gani. Tangu tuingie kwenye mikono yao, hajaona vumbi langu. Sikushangaa kwanini alikuwa ananitilia shaka.
Hakuwa anajua japo mimi si nyani mzee, nimekwepa ncha nyingi za mishale!
Basi kwakuwa nimemlazimisha na kumsihi sana, tukaenda huko.

**
 
*NYUMA YAKO --- 07*
*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Hakuwa anajua japo mimi si nyani mzee, nimekwepa ncha nyingi za mishale!
Basi kwakuwa nimemlazimisha na kumsihi sana, tukaenda huko.
ENDELEA
Ilikuwa ni safari iliyotuchukua muda wa dakika kama kumi na tano hivi, tukawasili mbele ya kijumba kidogo, mbavu za mbwa. Nyumba iliyotindwa na majani na kusimikwa na miti minene. Haikuwa na madirisha, mlango ulikuwa wazi.
Kutoka humo, mtu alikuwa akikoroma sana kana kwamba simba au mtu aliyekabwa. Bwana mdogo yule, ambaye sasa njiani aliniambia jina lake, aitwa Buyu, akaniambia huyo akoromaye ni Toliso. Kijiji kizima wamfahamu kwa tabia yake hiyo, lakini kisitupumbaze kwani amekuwa akisemwa kuwa hulala macho!
Yaani japo anakoroma hivyo, huwa macho, na kitu kidogo tu chaweza kumwamsha na kumdaka mvamizi wake. Nilijifunza kuwa Toliso ni mtu mwenye kupewa mawazo mengi ya kutisha. Mtu anayeogopwa na kudhaniwa si wa kawaida. Niliendelea kulithibitisha hilo kadiri tulivyozidi kusonga, ila kwangu mimi halikunijengea woga hata kidogo.
Sikuona kama mtu wa kunifanya nihofie. Nimepita sehemu nyingi nikakutana na wengi wa kunihofisha na wote nikawalaza chini. Atanishindaje huyu wa kwenye ulimwengu wa nyuma?
Bwana mdogo akanitazama na kuniambia, "sasa nazama ndani, niombee nitoke salama. Na kama si hivyo, usidiriki kujitokeza ukapambana, we nenda zako!"
Sikutaka kubishana naye hapa, nikamkubalia kazi iende kwa wepesi. Akazama ndani na kwa uangalifu, nikiwa namchungulia mlango akasonga akinyata.
Alipozidi kuzama ndani nikawa simwoni sasa kutokana na giza, na ndani hakukuwa na mwanga hata kidogo kutokana na ukosefu wa madirisha. Sasa nikawa nategemea masikio yangu kusikia kinachoendelea japo nayo muda fulani yalikosa taarifa kutokana na ukimya wa hatua za bwana mdogo yule, Buyu.
Zikapita sekunde kama kumi hivi, nadhani alikuwa akiangaza kutafuta ile dawa. Kwenye sekunde ya kumi na moja, kwa mujibu wa makadirio yangu, nikahisi sauti ya kitu kikidondoka! Moyo wangu ukafanya pah! Nilihofu huenda Toliso akaamka na kumsababishia matatizo Buyu, ila haikuwa hivyo, nikaendea kusikia sauti ya mtu akikoroma. Angalau nikapata afueni.
Nikaendelea kutulia nikiskiza. Zikapita tena sekunde tano, hapo ndiyo nikapata jaka la moyo! Sauti ya mtu akikoroma ilikata ghafla na mara sauti nzito ikavuma kusema, "Taris khanje?"
Na kabla sijasikia chochote, nikaona mwanga umewaka ghafla mule ndani. Hapo nikamwona Toliso akiwa chini ameshikilia taa mkono wake wa kushoto! Taa hiyo haikuwa kama ambayo waijua wewe. Lah! Ilikuwa ni kama buyu lililozungushiwa utepe unaopitisha mwanga, ndani yake kulikuwa na wadudu wadogowadogo wengii ambao mikiani mwao walikuwa wakitoa mwanga.
Nilishangazwa na sayansi hii! Baadae nilikuja kujifunza kuwa, kuwasha taa hiyo, ni kwa kutikisa hao wadudu waliomo ndani, wakiamka hujiwasha kama ni kiza. Ukiweka buyu chini, basi nao hulala na kujizima!
Basi kuamka kwa Toliso hakukuwa jambo la kawaida kwa Buyu, hata kwangu pia. Bwana huyo, mzito mrefu na mpana, alisimama akimtazama Buyu ambaye alikuwa amesimama pembeni ya shelfu yake nyeusi. Buyu akahofu sana, nilimwona akitetemeka. Aliwahi kuomba msamaha na kuomba abakiziwe uhai wake. Japo sikuwa najua lugha anayoizungumza, matendo yake yalionyesha hayo niyasemayo.
Nikamwona Toliso akiweka taa yake chini, kisha akabinjua vidole vyake na kuviliza mifupa. Akanguruma akisema lugha yao ya ajabu kisha akamnyaka Buyu na kumnyanyua juu kwa mkono mmoja!
Hapo nikamwona Buyu akibadili sura. Hakuwa mwenye huruma tena bali aliyefura hasira. Na akiwa amekabiwa juu, akawa anarusharusha mateke na ngumi ambazo hazikusaidia chochote kwa Toliso! Zaidi mwanaume huyo akacheka na kukodoa macho yake ya kutisha! Akamminya zaidi Buyu.
Hapo ndiyo nikaona ni muda wangu muafaka wa kujongea kumwokoa Buyu. Nikazama kwa fujo!
"Mwache!" Nikaropoka. Bwana yule akanitazama na kisha akasema kwa lugha yake nisiyoielewa, akamtupia Buyu chini na kunisogelea. Akanitazama na kutabasamu.
"Usidhani kama mimi nakuogopa," nikamwambia nikimnyooshea kidole na kumtazama machoni. Alikuwa ni mrefu kuliko mimi. Alinitazama kana kwamba mtoto mdogo!
Ghafla akanisukumia nje ya jengo lake, nikipaa nikatua chini na kujibamiza mgongo! Mgongo uleule ambao ulikuwa na maumivu ya pale mtini!
Akanisongea kwa hatua zake nzito, kisha akasimama karibu na mimi. Hapo akajivuna kwa lugha na sauti yake ya kukoroma. Kidogo nikasikia sauti kali ya filimbi! Aliipuliza Buyu. Sikujua ni kwasababu gani. Basi bwana yule, Toliso, akaninyanyua juu na kunisogeza usoni mwake, akanitazama kwa sura ya kebehi.
Hakuwa anajua 'anadeal' na mtu wa aina gani. Bila shaka alidhani mimi na wale watu anaowatawala tuko sawa. Nikaona sasa ni muda wa kumwonyesha utofauti.
Hataka nikamkita kwenye 'angle' dhaifu ya shingo, akaniachia na kudaka shingo yake. Hajakaa sawa, nikazunguka na kumzaba teke kali la uso, akadondoka chini kama mzigo!
Kutazama nikaona watu wakiwa wamejongea hapo. Walikuwa wamebebelea mikuki mikononi mwao, ila hawakunidhuru. Wakawa wamesimama wakinitazama mimi na Toliso. Hapo ndiyo nikajua maana ya ile filimbi ya Buyu!
Kidogo Toliso akajikusanya na kuamka. Akanyoosha shingo yake kah-kah! Alafu akanguruma na kunifuata kwa hatua pana. Hatua moja tu akawa amenifikia, akarusha ngumi yake, nikaikwepa kisha haraka nikakwea kifua chake na kumtifua na goti la kidevu! Akazubaa kwa maumivu. Nikapaa juu na kumzika na teke la kisogo, akadondoka chini asiamke tena!
Hapo Buyu akanisogelea na kunitazama kwa mshangao. "Umemmaliza!" Akatahamaki. Akanikumbatia kwanguvu na kunishukuru sana kisha akawageukia watu wake na kuwaongelesha maneno nisiyoyelewa. Baadae ndipo nikaja kujua kuwa Toliso alimwambia Buyu kuwa yeye ndiye aloyewamaliza wazazi wake kwakuwa walikuwa wakaidi.
Na baada ya kufanya hivyo, akasingizia mateka wa kizungu waliokuja kuvamia kijiji hicho. Basi, katika namna hiyo, nikawa mkombozi! Wanakijiji wakaninyanyua juu kwa shangwe wakiimba nyimbo zao, lakini mimi nikawasihi kwanza wakawasaidie wale wenzangu kule msituni mitini!
Upesi wakachukua dawa na taa ya Toliso, tukaelekea huko msituni na kuwapatia dawa wale wenzangu. Angalau wakapata ahueni, wakapatiwa pumziko maana walikuwa wamechoka mno! Tuliwakuta wakiwa wamebabuka migongoni. Migongo imekuwa mekundu kama bendera.
Hivyo usiku huo ukawa umepita hivyo. Nililala kwa uzito sana maana nilikuwa nimechoka sana kwa purukushani, lakini hata hivyo, kama ilivyo kawaida, nikajitahidi kuamka mapema, japo si mapema yangu iliyozoeleka. Niliamka jua likiwa limeshang'aza.
Kutazama nikaona wanakijiji wakiwa wanaendelea na shughuli zao. Wengine walikuwa wanatwanga, wengine wanakata nyama, wengine wanakata matawi na magome ya miti, wengine wakiwasha moto na kadhalika.
Mimi nilikuwa ndani ya chumba kidogo, sikujua ni cha nani, tangu nilipoingia usiku mpaka muda huo wa asubuhi sikuona mtu humo, nadhani walinipatia kwa heshima. Nilitoka humo na kuangaza angaza pia kujinyoosha mwili wangu alafu nikamtafuta bwana yule mdogo na kumweleza haja yangu, "naombeni mnisaidie kumsaka Raisi wangu. Naamini atakuwapo maeneo haya."
Basi kwa kushirikiana na watu wao, tukaanza kusaka kila eneo. Wale wenzangu walikuwa bado wapo mapumzikoni, bado hawakuwa wanajiweza kuzungumka. Tukazunguka kisiwa kizima na baada ya hapo tukazunguka na baharini kwa kutumia mitumbwi yao. Hatukuona kitu kabisa!
Sasa imani yangu ikaanza kunitoka. Raisi hakudondokea huku. Au Raisi hakuwa kwenye ndege! Sikudhani kama kazi hii ingeanza kwa ugumu mapema hivi ...

**
 
*NYUMA YAKO --- 08*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA
Basi kwa kushirikiana na watu wao, tukaanza kusaka kila eneo. Wale wenzangu walikuwa bado wapo mapumzikoni, bado hawakuwa wanajiweza kuzungumka. Tukazunguka kisiwa kizima na baada ya hapo tukazunguka na baharini kwa kutumia mitumbwi yao. Hatukuona kitu kabisa!
Sasa imani yangu ikaanza kunitoka. Raisi hakudondokea huku. Au Raisi hakuwa kwenye ndege! Sikudhani kama kazi hii ingeanza kwa ugumu mapema hivi ...
ENDELEA
Saa nne asubuhi, jengo la J. Edgar Hoover, makao makuu ya FBI.

Nilikuwa hapa nikiwa na shida ya kumwona Miss Daniele James, mpelelezi wa ndani wa swala hili la kupotea kwa Raisi. Alikuwa mtu aliyetingwa sana, alikuwa akitoka hapa na kuingia kule, kule na hapa, alipokuja kutulia ilikuwa ni kama baada ya dakika kumi tangu niingie hapo.
Akanitazama kwanza alafu akachukua faili toka kwenye shelfu, akalipekua upesi na kisha kama mtu anayenidhihaki kwa mbali, akaniuliza, "umepata nini huko, Anthony?"
Nikashusha kwanza pumzi ndefu, nikatikisa kichwa changu na kubinua lips pasipo kusema kitu. Akatabasamu kwa mbali. Akatazama tena faili lake kwa ukimya kidogo, nikamuuliza,
"Ni nini wewe umepata?"
Akanitazama kwanza, akafunga faili lake na kunitazama kwa macho ya kichovu ila yaliyo imara. Akaniuliza, "nikikuambia Raisi ametekwa, utasemaje?"
"Kwanini unasema hivyo?" Nikamuuliza. Sentensi yake hii ilinivuta na kunifanya niwe makini zaidi. Akakuna kwanza kichwa chake.
"Anthony, kwa namna nilivyofuatilia na kutazama baadhi ya matukio, natokea kuamini kuwa huenda Raisi akawa ametekwa, tena kabla ya ndege kupaa!"
"Lakini imewezekanaje hilo?"
"Sijajua, badi sijalikamilisha jambo hilo. Lakini kwa ushahidi nilioupata, naona niko sahihi kusema ninayoyasema."
"Naomba basi unijuze," nikamsihi.
"Usijali, wewe ni mshirika wangu kwenye hili, ila ..." akanitazama akinikodolea. "Unajua hivi sasa upo kwenye ardhi ya Marekani, I am the boss here, sawa? Utafuata yale nitakayokuwa nakuambia na kukuelekeza."
Kabla sijajibu, akaendelea kumwaga maneno. "Kutokana na utafiti mdogo nilioufanya, nikisaidiwa na Secret services, nimebaini kuwa Raisi alikuwa anaumwa hapa karibuni. Hali yake kiafya haikuwa nzuri sana, tuseme hivyo. Na kama utakuwa ulifuatilia vema utakuwa umegundua hakuwa akihudhuria baadhi ya office matters kwa sometimes."
"Sikuwa nafuatilia," nikawahi kumhabarisha. "Nilikuwa zangu likizo, na kidogo nikajitenga na mambo haya ya kuumizana vichwa."
Lengo langu la kumweka bayana ni kumtengenezea mazingira ya yeye kunihabarisha juu ya kila kitu anachokijua. Nilitaka adhanie kuwa mimi ni pipa tupu na hivyo basi anijaze na kila taka anayoijua yeye.
"Basi kama haukuwa unajua, ndo' nakujuza. Swala hili lilinifanya nifuatilie kidogo hili jambo na kuona ni kwa namna gani linaweza likawa na mahusiano na kupotea kwa Raisi, ila bado sikuona mahusiano ya moja kwa moja."
"Sasa mbona ukasema Raisi huenda akawa ametekwa?" Nikamuuliza. Akafungua droo yake na kutoa chupa fulani aitumiayo kuhifadhia vikorokoro, humo akatoa mashine ya kumsaidia mtu mwenye pumu kuhema.
Mashine hiyo ilikuwa imehifadhiwa ndani ya kifuko kidogo kilaini. Akanionyeshea, "unaona hii? Ni ya Raisi!"
Nikakidaka na kukitazama vema. "Umekipata wapi?"
"Uwanja wa ndege!" akanijibu akifunga droo yake. "Kilikutwa kikiwa chini. Haingii akilini kuwa kitu hicho kitakuwa kimedondoka kwa bahati tu. Raisi huwa nacho muda wote, aidha mkononi au mfukoni. Na hatua nne toka kilipookotwa, kuna alama mbili za tairi ya gari!"
Akanitolea picha na kunionyesha. Kwa namna alama hizo zilivyo, ilionyesha wazi kuwa usafiri ulotumika hapo ulikuwa ni mdogo. Kwa mahesabu ya upesi, ni vile vigari vidogo viwavyowandawanda uwanja wa ndege.
Ina maana kimojawapo kitakuwa kilihusika na kumsafirisha Raisi? Lilikuwa fumbo. Nikiwa natazama picha hiyo, simu yangu ikaita mfukoni. Nikaitoa na kutazama. Ni Jack Pyong! Nikapokea na kumuuliza, "nini shida?'
"Njoo ofisini mara moja. Una mgeni!" Aliniambia hivyo kisha akakata simu. Nikafiriki kidogo juu ya alichoniambia kabla sijarudisha kichwa changu kwenye ile picha na kisha usoni mwa Daniele.
"Kuna kingine ulikipata?"
"Hapana, si rahisi kama unavyowaza, Anthony."
"Najua. Vipi umefanya mawasiliano na watu wake wa karibu?"
"Mkewe hayupo kwenye mood ya kuongea. Tangu mumewe aliporipotiwa kupotea, amekuwa wa kulia na kujitenga. Sijajua kwa sasa kama atakuwa radhi."
"Ni muhimu kuongea naye."
"Najua, Anthony. Nataka sana kufanya hilo ila siwezi kumlazimisha. Yuko depressed hivi sasa, nadhani muda unaweza kumtuliza."
"Vipi kuhusu makamu wa Raisi?"
"Nimeongea naye mara moja. Unajua hivi sasa amekuwa busy sana maana ni yeye ndiye aliyekaimu kiti cha Uraisi. Natazamia kuonana naye hapa karibuni kwa mazungumzo zaidi."
"Basi utakapoenda huko, usisite kunihabarisha twende wote. Sawa?"
Akanitazama kwanza kisha ndiyo akasema, "sawa, usijali." Kidogo nikahisi sauti ya mngurumo mfukoni. Ilikuwa ni simu. Nikaitoa na kuitazana, nikaona ishara ya ujumbe toka kwa Jack Pyong. Sikuusoma, nikanyanyuka na kumuaga Daniele.
"Tutaonana muda wowote!"

**

"Kama utakuwa hujaniitia la maana wewe macho manne, nitakumaliza!" Niliropoka nikiingia ofisi ya Jack Pyong. Ofisi yake na yangu hutenganishwa kwa umbali wa hatua thelathini za mtu mzima. Kwenye upande wa kuingilia ndani ya jengo, ofisi yake i karibu na mlango, ila kwa upande wa kutokea, yangu i karibu. Kama hujalelewa, achana nayo isikuumize kichwa.
Nilimkuta Jack Pyong akiwa amerelaksi kwenye kiti chake, miguu ameweka juu ya meza na mikono yake ameifanya mto kulazia kichwa. Ana 'swing' kutoka kushoto kwenda kulia, kulia kwenda kushoto. Mezani hapo kuna kopo kubwa la kahawa nyeusi.
Akanitazama na kutabasamu.
"Nawe ukaja upesi, sio?" Kisha akacheka na kugonga vivanja vyake. "Mjinga kweli wewe. Mgeni gani huyo wa kuja kukufuata huku?" Hapo nikachomoa simu yangu na kuutazama ule ujumbe alionitumia nikiwa na Daniele,
'Yule dada wa Hong Kong yupo hapa!'
Laiti ningeusoma ujumbe huu nikiwa kule kwa Daniele, nisingesumbuka kuja kwa huyu lofa. Ningejua ananidanganya wazi kwani mwanamke yule hakuwa anatambua kama mimi nafanya kazi CIA. Sikumwambia hilo.
Nikamzaba Jack Pyong kofi la kichwa na kumwambia, "hivi unajua nilikuwa kwenye mambo ya maana?"
"Yapi?" Akaniuliza kwa masikhara. "Hata hili nililokuitia ni la maana!"
"Lipi hilo?"
"Si la huyo mgeni! Huyo mwanamke! ... kuwa mkweli, Anthony. Bado unamkumbuka, sio?"
Nikavuta kiti na kuketi. Nikamtazama Jack Pyong na kumwambia, "kama kuna kitu nitakuwa nakumbuka kuhusu huyo mwanamke, ni simu yangu tu. Si vinginevyo. Nahisi yeye ndo' alichukua simu yangu."
"Hapana, Tony," Jack akatikisa kichwa. "Ni moyo wako ndio aliuchukua, si simu!"
"Jack, hivi kuna muda unaacha masikhara na kuwa serious?"
Akanyamaza. Akanitolea simu yake mfukoni na kisha kuifungua. Akanipatia. "Ebu tazama!"
Nilipoangaza nikaona 'chatting' zake na mtu fulani kwenye mtandao wa whatsapp. Nilipotazama picha ya mtu huyo anayechat naye, nikagundua ni yule mwanamke mzungu wa kule Hong Kong! Nikamtazama Jack nikimtumbulia,
"We macho manne, kumbe ulikuwa na namba yake!"
"Sikuwa nayo. We huoni mwanzo wa text? ... ni yeye kanitafuta. Hata jina bado sijamtunzia."
"Amekupataje?"
Akapandisha mabega juu, "sijui!"
Nikatazama tena zile jumbe. Walikuwa tu wamejuliana hali na kukumbushiana ile siku. Nikamuuliza, "Kwanini hukumuuliza juu ya simu yangu?"
"Simu ipi, Tony? ... unadhani ana simu yako?" Jack akaniuliza akinitazama. Akanipokonya simu yake na kuendelea kutext.
"Anaweza akawa anajua. Jaribu kumuuliza."
Hakunijibu, kidogo akatulia kisha akasema, "Usijali, anakuja Marekani. Utamuuliza hayo yote."
"Are you serious?"
Akanionyeshea simu yake. "Yes, I am."
Niliposoma hizo texts nikaona ahadi ya mwanamke huyo kuja Marekani mwisho mwa juma. Kidogo nikatahamaki.
"Sasa ushindwe mwenyewe!" Jack Pyong akasema na kunikonyeza. Pasipo kumuaga, nikanyanyuka na kutoka ndani ya ofisi yake. Huko nyuma akapayuka, "baadae saa tatu tukutane dinner!"
Sikumjibu, nikaenda zangu. Nilipofika ofisini nikaketi na kuwaza juu ya mambo yale ambayo Daniele alinieleza. Mosi, Raisi kuumwa. Pili, kifaa chake cha kupumulia kuokotwa uwanja wa ndege. Kidogo nikawa nimepotezwa fikirani mpaka pale ambapo mlango wangu uligongwa.
"Nani?"
Sikujibiwa, mlango ukafunguliwa. Alikuwa ni mwanamke mrefu mwembamba mwenye miwani mikubwa ya kumsaidia kuona. Mwanamke huyu aitwa Jolene, ni mfanyakazi mwenzangu, yeye akijihusisha kama secretary.
"Nina ujumbe wako," alisema akinijongea.
"Sasa Jolene si uwe unabisha hodi?"
Hakunijibu. Akanitazama na macho yake kama ya paka kisha akaweka kikaratasi mezani na kwenda zake. "Yani mwanamke huyu ana matatizo kweli!" Nikalalama nikiokota kile kikaratasi.
Niliposoma nikakutana na ujumbe, "NITAFUTE" kisha chini yake kuna namba za simu na anwani ya eneo.

**
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom