Evarist Massawe
JF-Expert Member
- Jul 4, 2012
- 666
- 853
Jamani nimekumis mpaka naumwa
Ahsante Tivu wetu naamini kitu kitakuwa mwake kama dawa kama kawa
Ahsante Tivu wetu naamini kitu kitakuwa mwake kama dawa kama kawa
*NYUMA YAKO -- 06*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Nikajitahidi kujichoropoa, wapi! Zaidi nikajiongezea maumivu zaidi. Niliporusha macho kuwatazama wenzangu, nikawaona wakiwa wametulia tuli. Hawakuwa na fahamu!
Nikahisi usiku huu ndiyo mwisho wetu.
ENDELEA
Hata nikainamisha kichwa changu kama kristo msalabani, sasa nimekwisha. Mwanaume miliyeshiriki kwenye misheni kadhaa za hatari, nakuja kuuawa na hawa washamba wa msituni. Aibu iliyoje?
Ila, nikajadili na nafsi yangu, haikuwa kama nilivyokuwa nawaza. Hamna mtu aliyedhani hapa kuna watu, na zaidi ya yote, kwenye shambulio la kushtukizwa, hamna mjanja. Atakayemuwahi mwenziwe basi ndo anakuwa mshindi. Hata simba akiwa mbugani, anawezwa wahiwa na nyoka, akamalizwa!
Hapa tulikuwa tumewahiwa, na japo lilikuwa jambo chungu kwangu, ila ndiyo ulikuwa uhalisia. Sikuwa na ujanja wa ziada.
Nikiwa nimejikatia tamaa, nangoja sasa 'nimezwe' na ule mti kama tulivyonenewa, nikahisi kitu huko msituni! Masikio yangu yakasimama na macho yangu yakang'aza. Ilikuwa ni kama kishindo cha mtu au mnyama ila sikuona kitu!
Kishindo hicho hakikukoma, kikaendelea tena na tena na kunijaza hofu huenda akawa mnyama wa mwituni. Endapo akitokea hapo tutajiteteaje? Nikapata mawazo yaliyonipa tena nguvu ya ajabu kupambana na kamba nilizofungiwa.
Nikapambana kujisukuma na kusukuma, waapi! Zaidi nikajitia alama nyekundu mwilini, pia majeraha na maumivu tu! Sikufanikiwa wala kwa dalili!
Kishindo kikaendelea kusikika huko gizani msituni na mara sauti ikasema, "ewe mtu wa manjano, bado upo?"
Nikaitambua sauti hiyo kuwa ya bwana yule mdogo. Bwana azungumzaye lugha yetu. Yeye alitokea upande wangu wa kushoto baada ya punde na kisha kunisogelea kwa karibu.
Akanitazama machoni. "Naona bado upo. Vipi, unaendeleaje?"
"Hali inazidi kuwa mbaya," nikamjibu na kumsihi, "naomba uniweke huru!"
"Si kwa haraka hivyo," akasema akitikisa kichwa chake, kisha akahema akinitazama kama mtu anayefurahia mateso yangu. Akaniuliza, "kwanini mlivamia kijiji chetu? Ni nini tuliwakosea?"
Nikamtazama kwa macho yangu malegevu. Uso wake ulikuwa unang'azwa na mwanga wa mbalamwezi. Nikafungua kinywa changu kikavu na kumwambia, "sijawahi kuja hapa, hii ni mara yangu ya kwanza. Nikuambieje unielewe?"
Mara akatoa kijiwe fulani nyuma ya mgongo wake. Kilikua ni kijiwe kidogo kimachong'aa. Kwa mwanga ule uliokuwepo nilikiona ni kijiwe chenye rangi nyekundu, sikujua mwangani mwa jua kingeonekanaje.
Akaniuliza akinionyeshea kijiwe hicho, "ni hichi ndicho mnatafuta?"
"Hapana!" Nikajikakamua kukanusha. "Sina shida na chochote toka kwenu. Nimefika hapa kumtafuta mtu aliyepotea, na si vijiwe!"
"Mtu gani huyo? Yule aliyedondoka toka kwenye nyota?" Akaniuliza akishika kidevu chake.
Nikamkazia, "Ndio huyohuyo! Je, umemwona?"
"Ndio. Nimemwona."
Hapa nikatoa macho. "Yupo wapi? ... tafadhali nipatie mtu huyo nasi tutaondoka msituone tena!"
Akatulia kidogo. Akanitazama kwa mafikirio alafu akaniuliza, "nikikuonyesha utanipatia nini?"
"Chochote kati ya tulivyokuja navyo!"
"Mi' nataka kile cha kuonea usiku. Mimi ni mwindaji. Nahisi kitanisaidia sa--"
"Nitakupatia, usijali!" Nikamkatiza. "We twende nionyeshe wapi alipo mtu huyo!"
Basi akanifungua kamba na tukaanza safari. Lakini hakuwa mjinga, aliniweka mbele yeye akiwa nyuma yangu. Mkononi alibebelea mkuki na kinywani alikuwa ameshikilia filimbi kwa lips zake. Filimbi hii, kwa alivyoniambia, ingemwamsha kila mtu kijijini aje kunitafuta endapo ningejitia ukaidi.
Sikupanga kuwa mkaidi. Lah! Hamu yangu ya kuuona mwili wa mtu ambaye nilihisi ndiye namtafuta ilikuwa kubwa kuliko kufanya njama za kutoroka.
Tukasonga, akiwa ananielekeza, mpaka eneo fulani ambapo alinitaka nisimame na kutulia. Nikafanya hivyo. Hapo toka kwenye kibanda kimoja kidogo kilichotengenezwa kwa matawi ya miti, akapenyeza mkono wake na kutoa mti mmoja mrefu, sikujua wa nini, akatoa pia na dude fulani kama rungu kisha akaniambia tuendelee na safari.
Tulipotembea kwa muda kidogo akaniamuru nisimame na kisha akaniambia, "mwili huo upo humo shimoni, utazama humo uangaze, nami nitakuvuta kwa mti utoke nje!"
Alipoyasema hayo akaniwashia lile dude nililodhani ni rungu, tena kwa haraka akitumia mawe, alafu akanishikisha ule mti mrefu nami nikazama na ginga la moto ndani ya shimo.
Lilikuwa ni shimo refu, na kadiri nilivyokuwa nazama nikawa nahisi harufu ya mzoga puani mwangu. Zaidi na zaidi. Na nikiwa sasa nimefikia nchani mwa fimbo ile ambayo nimeishikilia, nikawa nimefika chini kabisa! Kumbe ile fimbo ilikuwa na vipimo sawia kulingana na shimo.
Nikaangaza kutazama na ginga langu la moto, humo nikaona miili kadhaa, na mmoja kati yao, ambao ulikuwa mpyampya tuseme, ukawa umekamata macho yangu. Mwili huo ulikuwa mpana na wenye kuvalia suti nyeusi. Ulikuwa umelala kifudifudi.
Nikachuchumaa na kuugeuza niutazame. Haukuwa wa Raisi! Nikawaza utakuwa ni miongoni mwa wale maajenti wasiokuwepo kule ndani ya ndege. Sasa mwili wa Raisi utakuwa wapi? Nikajiuliza nikiendelea kuangazaangaza. Sikuuona!
Nilishika kiuno changu na kushusha pumzi ndefu.
"Vipi? Si huo?" Akaniuliza yule bwana mdogo juu ya shimo.
"Hapana, si wenyewe!"
Nikamwomba mti, anivute juu. Nilipopanda nikakung'uta mwili wangu na kumuuliza, "hakuna mwingine ninaoweza kutazama?"
Nikamwona akibinua mdomo wake. "Hapana, hili ndilo shimo pekee lililopo hapa."
Nikanyamaza nikiwaza. Akan'tazama na kunitahadharisha, "lakini makubaliano yetu si yapo palepale?"
Sikumjibu. Mimi nilikuwa na mawazo yangu kichwani. Akili yangu yote ilikuwa inawaza namna gani ambavyo naweza kuupata ama kuuona mwili wa Raisi. Hali hiyo ikampatia hofu yule bwana mdogo, nadhani akahisi nitamgeuka. Akanionyeshea mkuki wake na kuniambia tena, "makubaliano yetu si yapo palepale?"
"Ndio," nikamjibu kumtoa hofu. "Makubaliano yetu yapo palepale!"
Kidogo akatulia. Kwa muda huu nikawa nimemtengeneza rafiki. Nikapata mwanya wa kumuuliza kwanini aliniamini akanifungulia pale mtini ilhali mwanzoni walin'tilia shaka.
Akanitazama kwanza. Akatabasamu kwa mbali na kuniambia, "wewe sio kama wale! ... wale waliokuja kutuvamia na kuwaua wenzetu!"
"Umejuaje kuwa sisi sio wale?"
"Kwasababu ya kile kijiwe!" Akanijibu aking'aza macho. "Watu wale waliokuja na kuwaua wenzetu hawakuwa wanataka kingine zaidi ya mawe! ... wewe nilikuona upo tofauti. Sikuona tamaa ndani ya macho yako punde nilipokuonyesha kile kijiwe."
"Lakini tuliwaambia mwanzoni kuwa sisi tunamtafuta mwenzetu!"
"Ndio, ila si rahisi kuamini ... poleni."
"Basi naomba ukawasaidie wale wenzangu kama ulivyofanya kwangu."
"Siwezi!"
"Kwanini?"
"Mimi sina ile dawa waliyokupa wewe."
"Nani anayo?"
"Yule aliyekupa wewe. Anaitwa Toliso."
"Hauwezi kwenda mwomba? ... hauwezi ukamwambia kuwa sisi si kama wale waliokuwa wanawadhania?"
Bwana yule akanyamaza. Akausimika mkuki wake ardhini na kisha kidevu chake akakiweka juu ya kitako cha mkuki. "Si rahisi kama unavyodhani," akanijibu akiwa ameng'ata meno yake.
"Bwana yule, Toliso, ni mkatili na mkali. Hawezi kunielewa."
Nikamsogelea karibu na kumshika bega. "Tafadhali, sisi hatuna hatia. Hakukuwa na haja ya kutuadhibu namna ile. Kama kuna namna yoyote ambayo naweza kukusaidia kupata hiyo dawa, nambie nami nitafanya kwa moyo wote!"
Akatikisa kichwa kisha akafungua kiganja chake. "Kabla hatujaendelea na majadiliano yoyote, nipe kwanza kile ulichoniahidi."
"Nitakupatia il--"
"Nipe!" Akasisitiza akinikazia macho , basi nikaona si tabu, nikaongozana naye mpaka kule upande tulioingilia kisiwani. Huko tukute vile vitu tulivyoviacha, mitungi ya hewa na hata hiyo miwani ya kutazamia usiku.
Bahati tukavikuta, nikamkabidhi. Akajaribisha na kuona ni vema, imempendeza. Akafurahi sana. "Hii nitaitumia kuwindia nyakati kama hizi!" Akasema akitabasamu. Hata meno yake yaling'aa kinyume na kiza.
Nikamkumbusha, "fanya basi tukapate ile dawa!"
Akaiweka ile miwani kibindoni alafu akanitazama, "ewe bwana wa manjano, mbona wewe mbishi sana! Huoni kheri nimekusaidia ukaenda zako?"
"Nitaendaje pasipo wenzangu? Moyo wangu utakuwa mzito!"
"Sikia ... si kwamba sitaki kukusaidia. Namwogopa sana Toliso. Mkono wake ni mwepesi sana kutoa adhabu. Si mtu anayejishauri mara mbilimbili kummaliza mtu!"
"Nitakusaidia dhidi yake."
Akatabasamu, "wewe? ... unadhani unaweza kupambana na Toliso?"
"Kwanini nisiweze?"
Akashindwa kujibana na kicheko. Alipomaliza kucheka akaniambia, "mwili wako unaingia mara mbili na nusu ya Toliso. Akikudaka na mikono yake kama mibuyu, atakukamua mpaka hayo macho yatoke nje. Hujionei huruma?"
"Bwana mdogo," nikamwita nikimtazama. "Nitafanya lolote lile, nitapita kwenye hatari yoyote ile kuwasaidia wenzangu. Naomba tusipoteze muda, tuelekee huko haraka!"
Akanitazama katika namna ya kunionea huruma. Kwa namna hiyo nikajua ni kwanini anamzungumzia Toliso katika namna ya hofu. Ila nadhani bado nami hakuwa ananijua vema. Hakuwa anajua mimi ni mtu wa namna gani. Tangu tuingie kwenye mikono yao, hajaona vumbi langu. Sikushangaa kwanini alikuwa ananitilia shaka.
Hakuwa anajua japo mimi si nyani mzee, nimekwepa ncha nyingi za mishale!
Basi kwakuwa nimemlazimisha na kumsihi sana, tukaenda huko.
**
Umeona eenhDaaaaah utamu kolea
Kama nini madame
Kama nini madame
walaDuh hujawaza ujinga kweli
Duh hujawaza ujinga kweli
Hutuangushi...ila ukiamua kutikisa mbuyu mzee baba ...unatikisha kweli na mabuyu kuanguka..!sijui wachaga ..hao...huwa wanapanda??Kwani huwa nawaangusha wapendwa?
Nimekuja mzee.Hutuangushi...ila ukiamua kutikisa mbuyu mzee baba ...unatikisha kweli na mabuyu kuanguka..!sijui wachaga ..hao...huwa wanapanda??