Nyoni hayuko ofisini, yuko kazini

Pinda for president 2015! safi sana funika kombe mwanaharamu apite MADOKTA MPO!mama kama kawa ofisini kweli inzi hufia kwenye kidonda.
 
Hivi pinda naye ni mtu wa kumuamini!! Akiongea maneno 50 chukua 1.
 
Nimepoteza imani 100% na pinda..he's such a good liar..mbona ana tudhalilisha watu wenye nyota simba?? sisi ni wakali na wachapa kazi..amuone mwenzake lowassa..anatia kinyaa kwakweli..nasikia mwanasheria ..sijui kama kuna kesi hata moja alishinda,,kutwaaa kudanganya tu aibu hata haoni..

Sasa umepoteza imani na Pinda kivipi? kwani Pinda ndiye aliyemteua Nyoni? Aibu ya nn.
 
Mwaka huu naweza kufanya tukio moja la Ki-arabu dhidi ya kiongozi yeyote wa Serikali aliyesimamishwa au anayegoma kujiuzuru.Subirini muone
 
Musipoteze muda kumfikiria huyu mam, Blind Nyoni will never come back. Sana sana fungukeni kuanza kuwaleta mafisadi wengine kama William Erio wa PPF au Emmanuel Humba wa NHIF
 
Sheria za kazi na serikali inavyofanya kazi ni kwamba mtu akisimamishwa kazi LAZIMA
apewa barua ya kusimamishwa kazi. Na wakati amesimamishwa kazi atapokea NUSU
mshahara. Serikali haifanyi kazi kwa kufuata matamko ya wanasiasisa yanayotolewa
majukwaani. Sasa kama Blandina Nyoni na Dr. Mtasiwa kama hawajepewa barua za
kusimamishwa kazi basi wanatakiwa wawepo wizarani wakiendelea na majukumu yao.
Hilo litakuwa kosa la Pinda (serikali) na wala sio Nyoni au Mtasiwa.
 
Inakuhusu nini? Hata kama akiachaia ngazi bado atapatakazi kwenye international org. You should be having better things to do than wasting time looking for majungu.
Kwa kuwa atapata kazi kwenye international org basi tumwache aendelee tu kufisadi au naona wewe ni mnufaika wa huyo mdada(simuiti mmama sababu akina mama ni watu wazima wenye uchungu na maisha ya watu,mdada ni msichana mdogo hajui maisha na hajali ),sasa anang'ang'ania nini si aende huku kwenye Inter org tuone kama atajichukulia tenda za catering na kuuza nguo za Tsh 100,000 kuwa Tsh 500,000
 
tamko manake nini tena kutoka kwa waziri mkuu
ingekuwa kwa wenzetu waarabu hawa wangeshapigwa mawe huko ofisini
inakuwaje wanafanya kazi hadi leo huku wakitumia rasilimali za taifa.
watanzania wote tunachukuliwa hatuna akili ila wao vionngozi ndio wana akili
 
Diamod bonds ni NGUMU stable sana, which make Diamond one of the hardest stones on earth...........so is CCM katika kusikiliza mambo ya maana na kyatenda...........Kigmu sana hiki chama.

images


Mkuu kwa kuilinganisha CCM na diamond unakipa hicho chama cha magamba magumu hadhi ya kuwa stable ambayo siyo stahiki yake. Inatosha tu kusema kuwa CCM wana moyo mgumu kama wa Farao maana sote tunajua mwisho halisi wa Farao. Na hicho ndicho kitakachoikuta CCM!
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Blandina Nyoni aliyetangazwa kusimamishwa kazi na Waziri Mkuu,Mizengo Pinda bado yuko kazini.Ziara yangu ya 'kiintelijensia' Wizarani hapo asubuhi ya leo imebainisha hayo.Nikijifanya ni mtu mwenye 'appointment' na msimamishwa huyo ili nimletee nyaraka zake toka kwenye Kampuni yetu ya Uwakili,nilielezwa kuwa ingawa Nyoni hapatikani ofisini tangu tarehe ya tamko la Waziri Mkuu,bado anaendelea kufanya kazi zake zinazoambatana na posho na marupurupu stahiki,akiwa nyumbani kwake au mahali popote pengine.

'Hatakiwi kuonekana hapa Ofisini ili vuguvugu la mgomowa Madaktari liishe' alieleza mmoja wa wasaidizi wa Nyoni. Imebainika kuwa hadi leo,si Nyoni wala Mtasiwa(Mganga Mkuu wa Serikali-Deo Mtasiwa) aliyepokea barua rasmi ya kusimamishwa kazi.Madaktari na watanzania kwa ujumla wamefanywa mazuzu? Mwenye masikio na asikie...

fanya pia ufutilie aliyeagizwa kuwaandikia barua kulikoni mpaka leo "how does it take? au ndo mwendo wenyewe?
 
Musipoteze muda kumfikiria huyu mam, Blind Nyoni will never come back. Sana sana fungukeni kuanza kuwaleta mafisadi wengine kama William Erio wa PPF au Emmanuel Humba wa NHIF

kulikoni tena? naomba utujuze maana maisha ya leo movie si movie tena watu wanafanya kweli mshua
 
Kama ni kweli!! Ni jambo linalouzi,kera na kusikitisha....mfumo huu wa kijambazi hautaweza kuwekwa pembeni mpk watanzania waamue kwa dhati na kwa njia yoyote ile kuwanyoosha.Vinginevyo itakuwa ni danganya toto.
 
Nimepoteza imani 100% na pinda..he's such a good liar..mbona ana tudhalilisha watu wenye nyota simba?? sisi ni wakali na wachapa kazi..amuone mwenzake lowassa..anatia kinyaa kwakweli..nasikia mwanasheria ..sijui kama kuna kesi hata moja alishinda,,kutwaaa kudanganya tu aibu hata haoni..

Ha ha ha ha ha..mkuu hapo kwenye black nadhani unahitaji kutupatia upembuzi yakinifu kuwa na uhakika na unachoongelea...vinginevyo itakuwa porojo na maneno yasiyokuwa na faida kwa taifa.
 
Hakuna cha kushangaa hapo.Bunge lliamuru kina hosea na wenzake wachukuliwe hatua za kinidhamu kwani si kila mtu anaona wanaendelea kupeta tu hii tanzania bana nchi ya wenyewe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom