Nyimbo za injili katika majumba ya starehe

Nyimbo za injili katika majumba ya starehe

hosh kosh

JF-Expert Member
Joined
Mar 2, 2017
Posts
748
Reaction score
572
Wadau kwema,

Kuna hili suala la wenzetu wa dini ya pili kwa maana Christians(wakristo) kuhusiana na nyimbo zao za kuabudu au kusifu kupigwa katika majumba ya statehe yenye kila aina ya uchafu mfano, jaribu kupita katika vilabu vya pombe vya mtaani(uswazi) utakutana nalo hili sana au ushakutana nalo sana ili labda.

Sasa huwa najiuliza hivi hizo nyimbo za injili za kusifu zimeruhusiwa kupigwa mahala hapo au na kama si hivyo hawa viongozi wao wa kidini kwanini walikataza au kulikemea ili kupitia katikamikusanyiko yao ya kuabudu au ili jambo kwao ni halali kufanyika hivo.

Sijawahi ona mimi kwa sisi Waislam Qaswida zetu kupigwa mahala kama hapo japo niliwahi sikia Morogoro kuna kilabu kimoja kilijaribu kufanya ivo kueka qaswida katika jumba chafu ilo afu pembeni ya jumba hilo la starehe kuna packing ya magari ya mizigo walitoka vijana kazaa na kumfuta DJ nakumshushia kipigo kizito tena mpaka polisi kufika jamaa yupo hoi.

Sasa kwanini nanyi msifate misingi kama hii yetu haiwezekani watu wanafanya uchafu huku wakiburudika kwa nyimbo zenu za kuabudu au kusifu, je hili suala viongozi au waumini wa kawaida mmeshindwa kulizuia au ni vipi?

Tafadhali nimelizungumzia hili kwa uzuri na si kwa kukashifu dini nyingine.
 
Pilipili ya shamba yakuwashia nini?

Zikipigwa wanakulazimisha kusikiliza?

Nyimbo za injili ni Uinjilisti na ni njia ya kusambaza injili.

Injili ni kwa watu wote hasa waliopotea.

Kwanini unafikiri kuna haja ya Watumishi wa kikristo kukemea hilo?
 
Pilipili ya shamba yakuwashia nini?

Zikipigwa wanakulazimisha kusikiliza?

Nyimbo za injili ni Uinjilisti na ni njia ya kusambaza injili.

Injili ni kwa watu wote hasa waliopotea.

Kwanini unafikiri kuna haja ya Watumishi wa kikristo kukemea hilo?
Kweli kabisa umemjibu vizuri
 
Civilization mkuu. Tunatofautiana level za civilization.
 
Injili inahubiriwa kwa njia mbalimbali, nyimbo ni mojawapo na injili sharti ihubiriwe kwa kila kiumbe. So sidhani kama kuna tatizo .
 
Pilipili ya shamba yakuwashia nini?

Zikipigwa wanakulazimisha kusikiliza?

Nyimbo za injili ni Uinjilisti na ni njia ya kusambaza injili.

Injili ni kwa watu wote hasa waliopotea.

Kwanini unafikiri kuna haja ya Watumishi wa kikristo kukemea hilo?
Injili haitukuzi usharati, ulevi ama aina yoyote ya uchafu. Japo sio mkiristo lakini najua kwamba dini ina mafunzo mazuri na yenye heshima.

Mtu anakwenda kulewa na kuzini alafu anaidhalilisha imani na mambo mazuri yanayofundishwa na injili hayapasi kuungwa mkono. Nawewe huna hati kamili ya ukristo kuwashinda wengi.
 
wadau kwema.
kuna hili suala la wenzetu wa din ya pil kwa maana Christians(wakiristo) kuhusiana na nyimbo zao za kuabudu au kusifu kupigwa ktk majumba ya statehe yenye kila aina ya uchafu mfno.. jaribu kupita katika vilabu vya pombe vya mtaan(uswaz) utakutana nalo hil sana au ushakutana nalo sana ili labda...

sasa huwa najiuliza hiv izo nyimbo za injil za kusifu zimeruhusiwa kupigwa mahala hpo au na km si hivo hawa viongoz wao wa kidin kwann hawalikataz au kulikemea ili kupitia ktk mikusanyiko yao ya kuabudu.. au ili jambo kwao ni halal kufanyika hivo..
sijawah ona mim kwa sisi waislam qaswida zetu kupigwa mahala kama hapo.. japo niliwahi sikia morogoro kuna kilabu kimoja kilijaribu kufanya ivo kueka qaswida ktk jumba chafu ilo.. afu pemben ya jumba hilo la starehe kuna packing ya magar ya mizigo walitoka vijana kazaa na kumfuta dj nakumshushia kipigo kizito tena mpk polic kufika jamaa u hoi..

sasa kwann nanyi msifate mising km hii ytu haiwezekan watu wanafanya uchafu uku wakiburudika kwa nyimbo zenu za kuabudu au kusifu je hili suala viongoz au waumin wa kawaida mmeshindwa kulizuia au ni vp?


tafadhal nimelizungumzia hil kwa uzur na si kwa kukashifu din nyingne..
Hebu achana nao hawa jamaa hawana haya kwa lolote.
 
Nendeni mkatangaze injili ktk mataifa yote



MKUU, HIVI MTU ASIYE NA DHAMBI UNAMHUBIRIA MANENO YA MUNGU KWA FAIDA GANI?

MWENYE DHAMBI SHARTI AHUBIRIWE ILI AJUE ANALOFANYA SIVYO, AKIENDELEA KUWA MKAIDI ASIJE KUSEMA SKUJUA WAKATI NYIMBO ALIKUWA ANAZISIKIA HADI VILABUNI, HVYO MOTON MOJA KWA MOJA
 
Mtoa mada si mzima. Nyumba ya starehe inakua na uchafu ?
 
ni mgonjwa tu ndiye anayemuona daktari , kama nina kumbuka vizuri
 
Injili haitukuzi usharati, ulevi ama aina yoyote ya uchafu. Japo sio mkiristo lakini najua kwamba dini ina mafunzo mazuri na yenye heshima.

Mtu anakwenda kulewa na kuzini alafu anaidhalilisha imani na mambo mazuri yanayofundishwa na injili hayapasi kuungwa mkono. Nawewe huna hati kamili ya ukristo kuwashinda wengi.
Usharati ndio nini?

Injili ni ujumbe, baada ya mtu kupata ujumbe ndipo ataamua kuudigest na kufanya maamuzi au lah.

Kwani Qaswida inaondoa?
 
Nendeni mkatangaze injili ktk mataifa yote



MKUU, HIVI MTU ASIYE NA DHAMBI UNAMHUBIRIA MANENO YA MUNGU KWA FAIDA GANI?

MWENYE DHAMBI SHARTI AHUBIRIWE ILI AJUE ANALOFANYA SIVYO, AKIENDELEA KUWA MKAIDI ASIJE KUSEMA SKUJUA WAKATI NYIMBO ALIKUWA ANAZISIKIA HADI VILABUNI, HVYO MOTON MOJA KWA MOJA
Achana nao mkuu
 
Tena mimi napenda zaidi zipigwe huko zaidi kwasababu ndiko watu wanaupata ukweli kuhusiana na matendo yao.
YESU alikuja kuwaokoa waliopotea na wenye dhambi, sio tatizo nyimbo za injili kupigwa sehem za starehe kwasababu ni sehem ya injili.
Wakipigiwa nyimbo za kuhamasisha ngono, ulevi nk, ndio furaha yako?
LET GOSPEL OF JESUS CHRIST GO ON, USIIZUIE KWA FIKRA ZAKO
 
Back
Top Bottom