Nyimbo za Dini sehemu za Starehe

Nyimbo za Dini sehemu za Starehe

black abdu

Senior Member
Joined
Dec 2, 2022
Posts
157
Reaction score
214
Kusema ukweli huwa nakereka sana kusikia nyimbo za dini, zinapigwa kwenye sehemu za starehe, hasa Bar. Sehemu hizi ni sehemu Shetani na jeshi lake wanafanya kazi zao kwa ufanisi, na anaona ni kama kuikosea heshima dhana ya kuwa nyimbo za dini ni sehemu ya kuabudu.

Kwenye hizi Bar, zinapopigwa nyimbo hizi wakati watu wamelewa, naona ni kama kumkebehi Mungu.

Na pia ni kuzikosesha heshima nyimbo hizi, ambazo zilipaswa kuzikumbusha nyoyo Utukufu wa Mungu.
 
Dunia na vyote vilivyomo ni vya Mungu....utasemaje bar ni sehemu ya shetani.

Kuna ule wa "Yesu unipende leo kuliko jana", ukipigwa halafu vyombo tayari vimekolea unatamani hadi kumpa dj hug.
Wewe binti wa kisukuma umenishinda tabianimecheka sana, nimepiga picha jinsi mtu kalewa...halafu anaimba Yesu nipende leo kuliko jana
 
Wewe binti wa kisukuma umenishinda tabianimecheka sana, nimepiga picha jinsi mtu kalewa...halafu anaimba Yesu nipende leo kuliko jana
Mara ya mwisho hili songi nimepigiwa pale mianzini A town december mwaka jana sijui baa gani ile....aseee vyombo vimekolea yani niliinuka kwa utamu niliinjoi mnoo halafu akamalizia na mkono wa bwana alooooo acha tu.
 
Mara ya mwisho hili songi nimepigiwa pale mianzini A town december mwaka jana sijui baa gani ile....aseee vyombo vimekolea yani niliinuka kwa utamu niliinjoi mnoo halafu akamalizia na mkono wa bwana alooooo acha tu.
Mianzini mataa pale?
Mbona hakuna bar ya maana pale au kale ka mianzini club?
Siku hizi kamefungwa
 
Mianzini mataa pale?
Mbona hakuna bar ya maana pale au kale ka mianzini club?
Siku hizi kamefungwa
🤣🤣🤣🤣Kaka nlikuwa naload hapa mianzini mataa itakua bar gani? huyu itakua kaingia tu sehemu
 
Kusema ukweli huwa nakereka sana kusikia nyimbo za dini, zinapigwa kwenye sehemu za starehe, hasa Bar. Sehemu hizi ni sehemu Shetani na jeshi lake wanafanya kazi zao kwa ufanisi, na anaona ni kama kuikosea heshima dhana ya kuwa nyimbo za dini ni sehemu ya kuabudu...
Wacha magugu na ngano yamee pamoja. Wakati wa mavuno magugu yatatengwa na kupigwa kiberiti
 
Kaka nlikuwa naload hapa mianzini mataa itakua bar gani? huyu itakua kaingia tu sehemu
Pale mataa kama unapanda kale ka rough road kulikuwaga na Mianzini club kaliwika sana, kalivuta wengi lakini hivi karibuni kamefungwa
 
Ndugu mtoa mada ww kama sio mlevi ulifata nini bar mpaka ukaskia wanapiga nyimbo za dini?

Tuseme unapiga kinywaji lkn hupendi kuskia hzo nyimbo, kwanini usiwe unaenda bar ambazo hawapigi hzo nyimbo za dini?

Mtaji niwekeze mimi, wateja wafurahie nyimbo, we ukereke serious? husaidii kumlipa DJ, hulipi umeme huna mchango wowote zaidi ya kuanzisha thread tu
 
Back
Top Bottom