Nyie wenzangu mnawapataje au mnawapata wapi?

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,471
23,742
Sijajua sababu ni nini. maana leo nimewaza kuwa pengine nina nyota ya Buzi. Kila nikifahamiana na msichana nikatamani tuanze mahusiano hazipiti siku mbili utasikia anaomba pesa ya kodi.

Simu imeharibika au ada ya chuo. tatizo langu nini lakini? Maana inanifanya nihisi pengine sipendwi. Why kuna wenzangu wana enjoy mapenzi wanatoa pesa wenyewe kwa mapenzi na si kwa kulipia.

Nikijicheck nipo handsome kabisa na very fresh. mambo mambo yapo mengi tu na Unyakyusa flani hivi. Unyama mwingi sana kwa kwei. Ila nikitia tu mguu kifuatacho demu ana kuwa na shida ya pesa ya chini sana kaomba 100,000 ya chini sana. Maana kuna ambaye alitaka nimpatie 1,400,000 tumeonana naye ndani ya siku 5 tu.

Nikawaza hii ni kwa sababu gani? Hili jambo linanikatisha tamaa sana limekuwa kilio changu cha muda mrefu humu ndani. Ninyi wenzangu mnafanyaje? Maana pengine huku kuwapeleka hotels nzuri nzuri wanaona kama mimi ni tajiri. Mimi siyo tajiri sema napenda tu mambo mazuri. Tusifanyiane hivyo wajameni.
 
Akiombaa helaa achana naeeee...!!
97DCF89A-5E9E-47C2-8352-83294CF35394.jpeg
 
Back
Top Bottom