mchajikobe
JF-Expert Member
- Aug 14, 2009
- 2,652
- 1,238
Salaam,nina dukuku kubwa linalonisumbua kila siku ninaposikiliza vipindi toka kituo cha hii redio clouds,hivi lengo la hii steshen ni kuponda shughuli za watu au?kwa maana nilisikitishwa sana niliposikia jana wanamponda mbongo flava ambaye ametoa nyimbo yake mpya inayoenda kwa jina la PASTOR,msanii anayeitwa ROMA,amepoteza muda wake mwingi kutafiti na kuandika alichokiona,matokeo yake kituo cha redio kinaanza kumponda,je,ndio taaluma yenu inavyoruhusu?kama mlikuwa hamkuipenda hiyo nyimbo kwanini mliipokea?mimi binafsi sioni kosa la mtu kuelezea anachokiona,au kunafungu la kumi mnapata ktk kuponda kazi za wenzenu?Sio safi hiyo kumbukeni hao ndio wanawafanya nanyi mshine hapa mjini!!