Nyie clouds nyinyi!!!

mchajikobe

JF-Expert Member
Aug 14, 2009
2,652
1,238
Salaam,nina dukuku kubwa linalonisumbua kila siku ninaposikiliza vipindi toka kituo cha hii redio clouds,hivi lengo la hii steshen ni kuponda shughuli za watu au?kwa maana nilisikitishwa sana niliposikia jana wanamponda mbongo flava ambaye ametoa nyimbo yake mpya inayoenda kwa jina la PASTOR,msanii anayeitwa ROMA,amepoteza muda wake mwingi kutafiti na kuandika alichokiona,matokeo yake kituo cha redio kinaanza kumponda,je,ndio taaluma yenu inavyoruhusu?kama mlikuwa hamkuipenda hiyo nyimbo kwanini mliipokea?mimi binafsi sioni kosa la mtu kuelezea anachokiona,au kunafungu la kumi mnapata ktk kuponda kazi za wenzenu?Sio safi hiyo kumbukeni hao ndio wanawafanya nanyi mshine hapa mjini!!
 
ninavyoijua mimi, Clouds FM ni Entertainment Radio, imeanzishwa kwa ajili hio. kwa hio hayo uliyoyasikia yachukulie kama Entertainment buraza.
 
Chukulia powa bro....ktk life tunahitaji kukosorewa "constructive critisms" ili kupiga hatua mbele!!
 
Ndugu yangu hiyo sio issue kabisa. kuiponda nyimbo nadhani inamjenga msanii ili akiandaa nyimbo nyingine arekebishe makosa.
Clouds hawana kosa katika hilo labda kosa lao wameiponda nyimbo ambayo wewe unaipenda sana.
Take easy broda.
 
Mwana,unajua kuna jinsi ya kumrekebisha mwanadamu,lakini hakuna njia iliyo mbaya kama ya kumtangaza kwa kumsagia,maana zaidi ya kurekebishika,pia anakuwa muoga kwa siku zijazo kufanya mambo mazuri,sijui wenzangu mnalionaji hili.:angry:
 
ninavyoijua mimi, Clouds FM ni Entertainment Radio, imeanzishwa kwa ajili hio. kwa hio hayo uliyoyasikia yachukulie kama Entertainment buraza.
Swadakta Braza K, ni viburudisho hao, wanajitahidi sana kukosoa kwa kuponda. Wako vizuri na wana fursa kubwa ya kusikika popote watakapo. Redio bwana, watakutangaza kisha ukitaka kujisafisha hawakupi muda.
Hivi? hakuna njia ya kuwakosoa hawa jamaa? Wana upogo mwingi sana, JF wanaiangalia kwa mbali, napendekeza ianzishwe redio ya kuwakosoa watangazaji wa Redio wanaopitiliza mipaka katika kutoa au kutangaza habari.
 
Hamna lolote kuponda nyimbo wana vigezo gani? Hapo issue ni kuwa siku hizi Clouds ni rredio ya CCM sasa yule kijana alitoa nyimbo ya Mr. President jamani mistari hiyo wote tumeishudia juzi kuwa ni mizito na inatia hamasa kwa watanzania sasa wana m discourage yule bwana kwa kila jinsi. Unajua kumkosoa mtu mkosea kwa kumjenga na kum encourage huwezi kumkosoa mtu kwa kumtupia maneno kama vile "kama bobngo flavor haiuwezi si akapumzike" hapo unasema unamkosoa mtu? Kibonde weeee!
 
Swadakta Braza K, ni viburudisho hao, wanajitahidi sana kukosoa kwa kuponda. Wako vizuri na wana fursa kubwa ya kusikika popote watakapo. Redio bwana, watakutangaza kisha ukitaka kujisafisha hawakupi muda.
Hivi? hakuna njia ya kuwakosoa hawa jamaa? Wana upogo mwingi sana, JF wanaiangalia kwa mbali, napendekeza ianzishwe redio ya kuwakosoa watangazaji wa Redio wanaopitiliza mipaka katika kutoa au kutangaza habari.

Majala kimolo, sio mchezo hilo wazo lako limeenda shule. Redio itakayokuwa inapitia sehemu ambazo watangazaji wanachemsha. Maana redio nyingi ni upupu mtupu. Zile za kuaminika kama TBC ziko selective na habari zake.
 
Back
Top Bottom