Watu kama hao hupatikana mara chache baada ya miaka mingi sana ndani ya taifa. Sisi tulibahatika kumpata huyu mwanzoni kabisa, na huenda ikatuchukua miongo kadhaa kabla ya mwingine wa aina yake kutokea.
Tutofautishe hapa na kuwa bayana tunachokisema hapa. Sio kwamba hakuna watu wa aina yake katika jamii nzima ya waTanzania. Inawezekana wakawepo wengi, lakini hawajitokezi mbele kuongoza kama alivyofanya yeye.