Nyerere: Tunataka mtu anayejua kuwa huko ni upumbavu na ni hatari

mku

Member
Mar 27, 2011
88
9
Baada ya juhudi za CCM za kutaka kudhihirisha kuwa wanataka mtu asiyejua huko wanakolipeleka taifa ni kwenye upambavu na hatari kama alivyosema mwalimu kwenye hii hotuba fupi, leo hii wamefanikiwa kummvua LEMA uongozi. Tunaweza kusema kuwa mahakama imetenada haki kwa wote washiriki wa kesi hiyo, na kama ndo hivyo basi mahakama hiyo hiyo itende haki kwa kesi ya Mpendazoe na Makongoro yenye naked evidences. Kila nikijirazimisha kuamini kuwa CCM wanachekelea ushindi huo wa kuvuliwa LEMA ubunge, nashindwa maanake taswira ya mji wa Arusha hasa kwenye nyanja hii ya siasa inasema CCM walisahau hilo jimbo kwa sasa. Nasema na itadhirika kuwa CCM hawatashinda ARUSHA na wanazidi kuipa wigo CHADEMA wa kujitanua zaidi. Ni wakati muafaka sasa wa CHADEMA kuizika CCM kwenye kaburi la sahau.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom